Showing posts with label Kutoka pembe ya Afrika. Show all posts
Showing posts with label Kutoka pembe ya Afrika. Show all posts
Ngome nyengine ya Al-Shabaab yaanguka

Ngome nyengine ya Al-Shabaab yaanguka

Mwanajeshi wa AU akiweka doria
Mji wa bandari wa Barawe nchini Somalia ambao ulikuwa umetajwa kuwa ngome ya mwisho ya kundi la Al shabaab umethibitiwa na vikosi vya serikali vikisaidiwa na wanajeshi wa muungano wa Afrika.
Mji wa Barawe ulio umbali wa kilomita 200 Kusini Mashariki mwa mji mkuu wa Mogadishu umekuwa chini ya udhibiti wa wanagambo wa Al Shabaab kwa miaka sita.
Muungano wa Afrika unasema kuwa wanamgambo wamekuwa wakiutumia mji huo kama kituo cha kupanga mashambulizi dhidi ya mji mkuu Mogadishu.
Wapiganaji wa Al-Shabaab walianza kuondoka katika mji huo siku chache zilizopita.
Al-Shabaab wapata pigo Somalia

Al-Shabaab wapata pigo Somalia

Wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab
Wanajeshi nchini Somali wameidhibiti milima ya Galgala kutoka kwa wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab,kulingana na utawala wa eneo hilo.
Wanamgambo hao walikuwa wakiidhibiti milima hiyo ya Kaskazini mwa taifa hilo kwa miaka kadhaa.
Waziri wa habari wa Puntland amesema kuwa kamanda wa Alshabaab katika eneo hilo alisalimu amri miezi minne iliopita.
Kundi hilo linaloshirikiana na lile la Al-Qaeda lina makao yake makuu kusini na katikati mwa somalia ambapo vikosi vya Umoja wa Afrika vinafanya mashambulizi.
Abdiweli Hirsi Abdille,ambaye ni waziri wa habari wa jimbo la kaskazini mashariki mwa Somalia Puntland amesema kuwa vikosi vya serikali vimeliteka jimbo hilo la Glagala katika mashambulizi yaliotekelezwa alfajiri.
Hatahivyo hakutoa maelezo yoyote kuhusu wafungwa ama waliojeruhiwa.
Lakini kituo cha redio cha Al Furqan,kinachojulikana kwa kuwapendelea wapiganaji wa Al-Shabaab kimeripoti kwamba magari mawili ya kijeshi yaliharibiwa na wanajeshi 16 kuuawa.
Galgala ni eneo la kipekee la Puntland ambalo limekuwa chini ya udhibiti wa Alshabaab.
Kamanda wa Al-Shabaab katika eneo hilo Said Atom alijiunga na vikosi vya serikali mwaka huu na kuwawacha wapiganaji wake katika jimbo la Puntland.
Wapiganaji wa Al-Shabaab wamefurushwa kutoka miji mikuu katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni ,lakini bado wanadhibiti miji midogo katika maeneo ya mashambani.
 Mwandishi wa BBC Ann Waithera afariki

Mwandishi wa BBC Ann Waithera afariki

Marehemu Ann Waithera
Shirika la habari la BBC limempoteza mwandishi wa habari Ann Waithera.
Ann alikuwa anafanya kazi na BBC katika ofisi za Nairobi na amekuwa akiugua Saratani ya Ubongo kwa karibu miaka miwili.
Ann aliwahi kuwa ripota wa BBC mjini Addis Ababa Ethiopia. Mazishi yake yatafanyika siku ya Alhamisi mjini Nairobi.
Kabla ya kujiunga na BBC Ann alifanya kazi na shirika la habari la Nation Media Group nchini Kenya na Citizen TV kama mtangazaji. Ann alikuwa na umri wa miaka 39.
Wandishi wenza wa Ann BBC wameelezea watakavyomkumbuka Ann katika enzi zake alipokuwa anafanya kazi nao.
Razvan Scortea mmoja wa wakuu wa BBC amesema : "Nimeshtushwa sana na kifo cha Ann. Alikuwa mtu mzuri , mwerevu mpenda watu na mwenye matumaini kwa kila jambo. Mungu ambariki.''
Mkuu wa BBC Afrika Solomon Mugera ameelezea kuwa ni jambo la kuhuzunisha sana kumpoteza Ann.
''Nimehuzinika sana. Anne alikuwa mwandishi mahiri . Kila nilipomtembelea nilivutiwa sana na matumaini ya Ann kupona. Hata katika mkesha wa krismasi, nilipozungumza na Ann alikuwa mcheshi sana. Nakumbuka Ann ndiye alikuwa mwandishi wetu wa kwanza mwenye uwezo wa kuripoti katika lugha zaidi ya moja mjini Addis Ababa Ethiopia,'' alisema Solomon
Mkuu wa idhaa ya kiswahili ya BBC Ali Saleh naye pia ameelezea kushtushwa kwake na kifo cha Ann akimkumbuka kama mwandishi mahiri na mwenye kujitolea kwa kazi zake.
'Nakumbuka kufanya naye kazi kabla ya yeye kwenda Addis Ababa, na kufanya mipango ya kila alichotarajiwa kufanya. Matumaini mengi ila yamekatizwa mapema mno.'' alisema Elizabeth Blunt aliyekuwa mwandishi wa BBC mjini Addis Ababa kabla ya Ann kuchukua usukani kutoka kwake.
"Anne alikuwa mmoja wa waandishi mahiri wa BBC nchini Kenya . Kifo kimetupokonya mmoja wa waandishi wenye talanta kuu Afrika Mashariki.'' Kauli ya David Okwemba mhariri mkuu wa ofisi ya BBC Nairobi Kenya.
Mhariri mkuu wa idhaa ya Hausa mjini London Mansur Liman, ametuma rambi rambi kwa familia ya Ann, akiwaombea utulivu wakati huu mgumu
Na BBCSwahili
Kimataifa Asubuhi hii: Serikali yatwaa miji kutoka kwa waasi

Kimataifa Asubuhi hii: Serikali yatwaa miji kutoka kwa waasi


Wiki jana wanajeshi wa serikali walifanikiwa kukomboa miji kadhaa iliyokuwa imetekwa na waasi.
Rais Obama
Jamii ya Kimataifa imeafiki mkataba wa kusitisha mapigano kati ya waasi na serikali ya Sudan Kusini uliosainiwa hiyo jana mjini Addis Ababa Ethiopia.
Marekani imesema, mkataba huo ni sehemu muhimu ya kurejesha amani na utawala wa sheria nchini Sudan Kusini.
Rais Obama ametaja kutiwa sahihi kwa mapatano hayo kama hatua muhimu ya kurejelea amani ya kudumu.
Hata hivyo Marekani imeonya kuwa mzozo huo bado haujatatuliwa na kutoa wito kwa pande zinazozozana kutekeleza mkataba huo mara moja.
''Tunatoa wito wa viongozi wa Sudan Kusini kuheshimu mkataba huo na kuhakisha kuwa mazungumzo zaidi kuhusu jinsi ya kutatua mzozo wa kisiasa unaokumba taifa hilo yanaendelea'' Alisema msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani Mary Harf.
Zaidi ya watu 500,000 wamelazimika kutoroka makwao kutokana na vurugu hizo za mwezi mmoja
 Kimataifa asubuhi hii: Waasi na serikali ya Sudan Kusini wasaini mkataba

Kimataifa asubuhi hii: Waasi na serikali ya Sudan Kusini wasaini mkataba

Maelfu ya watu wameachwa bila makao kutokana na vita hivyo
Waakilishi wa serikali ya Sudan Kusini wanasema kuwa serikali imetia saini mkataba wa kusitisha vita na waasi.
Kulingana na mkataba huo uliotiwa saini mjini Addisa Ababa Ethiopia, mapiganao yanapaswa kusitishwa katika muda wa masaa 24.
Wapatanishi kutoka shirika la kikanda la IGAD, wamesema kuwa mkataba huo utatatua swala la kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa ambalo ndilo lilisababisha mazungumzo ya amani kukwama.
Aidha mkataba huo unatarajiwa kusitisha vita vya mwezi mmoja vilivyoanza tarehe 15 Disemba mwaka jana kati ya waasi na serikali.
Mazungumzo ya amani yamekuwa yakikumbwa na matatizo kuhusu swala la wafungwa 11 wa kisiasa ambao bwana Riek Machar anayeongoza waasi alitaka waachiliwe kama sharti la kutia saini mkataba wa amani.
Uchabuzi Online: Rais Kiir asema mji wa Malakal umekombolewa

Uchabuzi Online: Rais Kiir asema mji wa Malakal umekombolewa

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amesema wanajeshi wake wameukomboa mji wa Malakal kutoka mikononi mwa waasi jana.(21.01.2014) Waasi wameikanusha taarifa hiyo.
Sรผdsudans Prรคsident Salva Kiir Mayardit Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir
Rais Kiir ameuambia mkutano wa waandishi wa habari kwamba wanajeshi wake wameuteka mji wa eneo linalozalisha mafuta la Upper Nile, Malakal, na maeneo mengine. Hata hivyo hakusema kama wanajeshi hao walisaidiwa na wanajeshi wa Uganda. Iwapo taarifa hizo zitathibitishwa, utakuwa mji wa pili mkubwa kukombolewa na wanajeshi wa serikali katika kipindi cha siku tatu zilizopita, ambao wamekuwa wakisaidiwa na wanajeshi kutoka nchi jirani ya Uganda.
Msemaji wa waasi wa Sudan kusini aliyeko mjini Addis Ababa, Ethiopia ambako mazungumzo yanayolenga kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano yamekuwa yakisuasua, ametupilia mbali kauli ya rais Kiir. "Ni kweli wamejaribu kuuteka mji wa Malakal mwendo wa saa saba mchana lakini wameshindwa. Tungali tunaudhibiti mji huo," amesema Lul Ruai Koang, wakati alipozungumza na shirika la habari la Reuters.
Azimio lataka mapigano yasitishwe
Wakati hayo yakiarifiwa wapatanishi katika mkutano wa Addis Ababa wanazihimiza pande zinazopigana Sudan kusini kusaini mkataba wa kusitisha mapigano ili kuumaliza mzozo huo na machafuko yaliyoliharibu taifa hilo changa la Afrika. Hayo ni kwa mujibu wa rasimu ya makubaliano yaliyofikiwa kwenye mkutano huo.
Rasimu hiyo iliyoonekana na shirika la habari la AFP na kuwasilishwa kwa wajumbe, linataja kiwango cha mateso yanayowakabili raia, vifo vingi vilivyotokea, uharibifu wa mali na idadi kubwa ya watu kulazimika kuyakimbia makazi yao tangu mapigano yalipozuka Desemba 15 mwaka jana. Rasimu hiyo inapendekeza harakati zote za kijeshi zikome, na kuzitaka pande zote ziache kuwashambulia raia, kuua watu kiholela, kuwatumia watoto kama wanajeshi, ubakaji, udhalilishaji wa ngono na mateso.
Rasimu nyingine ya mapatano inamhimiza rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir awasamehe wafungwa 11 wa kisiasa, mojawapo ya masuala tete yaliyoyakwamisha mazungumzo hayo yanayosimamiwa na shirika la maendeleo la IGAD. Wafungwa hao wanatakiwa waachiwe ili washiriki kwenye mchakato wa maridhiano ya kitaifa.
Nkosazana Dlamini-Zuma Nkosazana Dlamini-Zuma
Hapo jana Mwenyekiti wa Halmashauri ya Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini-Zuma, alikwenda Juba kukutana na rais Kiir katika juhudi za kumshawishi atie saini mkataba wa amani.
Bashir kwenda Juba
Wakati huo huo, rais wa Sudan, Omar Hassan al Bashir, atasafiri kwenda Sudan Kusini Alhamisi wiki hii kuzipa msukumo juhudi za kutafuta amani. Hayo ni kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la serikali, SUNA. Mualiko huo umetoka kwa waziri mkuu wa Ethiopia, Hailermariam Desalegn, mwenyekiti wa shirika la maendeleo la IGAD, ambalo linasimamia mazungumzo ya kusuluhisha mzozo wa Susan kusini. Ziara hiyo ya Bashir itakuwa ya pili kwenda Juba tangu mapigano yalipozuka katikati ya mwezi Desemba mwaka uliopita.
Omar al-Bashir Archivbild 2012 Rais wa Sudan, Omar Hassan al Bashir
Wiki iliyopita Uingereza iliipongeza serikali ya Sudan mjini Khartoum kwa kutoegemea upande wowote katika kuyaunga mkono mazungumzo yanayoongzwa na IGAD. Maelfu ya watu wameuwawa na raia nusu milioni wamelazimika kuyakimbia makazi yao Sudanf Kusini kutokana na mapigano kati ya vikosi vinavyomtii rais Salva Kiir na waasi wanaomuunga mkono makamu wa rais aliyetimuliwa, Riek Machar.
Jimbo la Upper Nile ladhibitiwa na jeshi la serikali

Jimbo la Upper Nile ladhibitiwa na jeshi la serikali

Jeshi la Sudan Kusini limesema hii leo kwamba limeuteka mji mkuu wa jimbo lenye utajiri mkubwa wa mafuta la Upper Nile ambako rais Salva Kiir alikuwa akitafuta  idhini ya bunge kutangaza hali ya hatari katika eneo hilo.
Mji wa Malakal ni njia inayotumiwa kwa ajili ya kufikia vinu vya mafuta upande wa kaskazini.Mapigano yameshuhudiwa kwa muda wa zaidi ya wiki moja kati ya jeshi na waasi katika eneo hilo.
Msemaji wa jeshi Kanali Phillip Aguer akizungumza na shirika la habari la dpa amesema kwamba vikosi vyake vimefanikiwa kuwatimuwa waasi kutoka mji huo wa Malakal mnamo majira ya mchana wa leo.
Aidha amesema waasi hawajulikani walikokimbilia lakini wameshatimuliwa ingawa hakutowa maelezo zaidi kuhusu watu waliojeruhiwa kufuatia mapigano makali yaliyotokea katika operesheni hiyo.
Rais Salva aKiir ametowa muda wa siku 15 bunge liidhinishe hatuwa ya kutangazwa hali ya hatari katika jimbo hilo la Upper Nile
 Jeshi la S.Kusini lakomboa Malakal

Jeshi la S.Kusini lakomboa Malakal


Mazungumzo ya amani kati ya serikali na waasi yamekwama mjini Addis Ababa
Jeshi la Sudan Kusini linasema kuwa limeukomboa mji muhimu wa Malakal kutoka kwa waasi.
Msemaji wa jeshi Phillip Aguer amesema kuwa vikosi vya serikali vimewatimua waasi kutoka mji huo ambao ndio mji mkuu wa jimbo la Unity lenye utajiri mkubwa wa mafuta.
Wakati huohuo mji wa Bor ulikombolewa hivi karibuni na wanajeshi wa Serikari umedaiwa kuharibika kufuatia mapambano na waasi.
Lakini msemaji wa waasi, Brigedia-Generali Lul Ruai, amekanusha ripoti hizo ikisema kuwa waasi wangali wamuteka mji huo.
Ukombozi huu unakuja siku mbili baada ya wanajeshi kukomboa mji wa Bor.
Waandishi wa habari wanasema kwamba ikiwa ni kweli serikali imekomboa Malakal, mji wa mwisho mkubwa uliokuwa umesalia chini ya waasi, huenda hatua hiyo ikakwamua mazungumzo ya amani ya pande zote mjini Addisa Ababa, Ethiopia.
Waasi hata hivyo wangali wanadhibiti baadhi ya sehemu za nchi hiyo hasa maeneo ya vijijini.
Na BBCSwahili
Jeshi la UG vitani na waasi S.Kusini

Jeshi la UG vitani na waasi S.Kusini

Mkutano wa kupatanisha makundi yanayozozana Sudan Kusini unaendelea nchini Ethiopia
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, amesema kuwa jeshi la Uganda linashirikiana na wanajeshi wa Sudan kupambana na waasi nchi Sudan Kusini.
Mapigano hayo ambayo yalizuka mwezi uliopita yanaendelea katika maeneo kadhaa ya Sudan kusini, licha ya kufufuliwa kwa mazungumzo ya amani katika nchi jirani ya Ethiopia.
Baada ya wiki kadhaa za tetesi za wanajeshi wa Uganda kuwa nchini Sudan Kusini, jeshi la Uganda sasa limekiri rasmi kuwa liko katika vita na waasi wa Sudan Kusini.
Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi, Luteni Kanali Paddy Ankunda, Uganda ina takriban wanajeshi elfu moja na mia sita nchini humo.
Serikali ya Uganda imekiri kukabiliana na waasi hao tangu mwanzoni mwa wiki hii,wakati wanajeshi hao waliposhambuliwa na waasi wanaoongozwa na makamu wa zamani wa Rais Riek Machar.
Akisimulia kuhusu tukio hilo kwenye mkutano wa kikanda nchini Angola mnamo Jumatano, Rais Yoweri Museveni, alisema kwamba baadhi ya wanajeshi wake waliuawa au kujeruhiwa.
Jeshi la Uganda hata hivyo halijaeleza idadi kamili ya wanajeshi waliouawa.
Luteni Kanali Paddy Ankunda ametetea hatua ya Uganda kupeleka wanajeshi wake Sudan Kusini ikisema lengo lake ni kulinda raia na kufungua njia kwa misaada kuingizwa nchini humo .
Na BBCSwahili
 S.Kusini: Mazungumzo yakwamuliwa klabuni

S.Kusini: Mazungumzo yakwamuliwa klabuni


Mapigano nchini Sudan Kusini yamewaacha maelfu bila makao na kukimbilia nchi jirani
Wajumbe katika mazungumzo ya kupatanisha pande zinazozozana kwenye mgogoro wa Sudan Kusini, wameachwa vinywa wazi baada ya kupewa klabu ya disco kufanyia mazungumzo kutokana na ukosefu wa vyumba vya kutosha katika hoteli ya kifahari ya Sheraton, mjini Addisa Ababa , Ethiopia.
Klabu ya Gaslight ndiko kunakofanyika mazungumzo hayo.
Na hii ni baada ya chumba walichokuwa wanatumia wajumbe hao katika hoteli ya kifahari ya Sheraton kutumiwa na wanadiplomasia wa Japan.
Duru zinasema kuwa baadhi ya wajumbe waliudhika kutokana na ukosefu wa mwangaza wa kutosha pamoja na kelele nyingi.
Klabu ya The Gaslight iko kwenye chumba cha chini ya hoteli ya Sheraton, na ni klabu mashuhuri ambayo hutembelewa tu na watu mashuri,matajiri pamoja na wasichana vipusa.
Katika siku ya kawaida, wanadiplomasia na wafanyakazi wa mashirika yasiyo ya kiserikali hufurika kwenye klabu hiyo.
Mazungumzo yanayonuiwa kusitisha vita ambavyo vimekuwa vikiendelea kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa, yameanza tena , lakini wajumbe wanakutaka katika chumba cha chini ya hoteli ya Sheraton ambapo kuna kilabu ya disco.
Chumba walichokuwa wanatumia awali kabla ya mzungumzo kukwama, kinatumiwa na waziri mkuu wa Japan, Shinzo Abe ambaye yuko kileleni mwa ziara yake ya kwanza Afrika.
Mazungumzo hayo, hata hivyo yatakuwa yanafanyika nyakati za mchana wakati angalau kelele sio kingi sana.
Mazungumzo hayo yanaongozwa na shirika la Igad.
Wajumbe wanatumai kuwa wataweza kupata mwafaka wa kusitisha vita hivyo ambavyo vimesababisha vifo vya watu, 1,000.
Mogogoro huu kati ya Rais Kiir na aliyekuwa makamu wake wa Rais Riek Machar, ulianza Disemba kumi na tano
Na BBCSwahili
Human Rights Watch yalia na mauaji ya raia Sudan Kusini

Human Rights Watch yalia na mauaji ya raia Sudan Kusini

Human Rights Watch imeuomba pia Umoja wa Mataifa kuzuwia mali na kuwawekea vikwazo wale wote wanaohusika na uhalifu huo.
Shirika la kutetea haki za binaadamu la Human Rights Watch, limesema mauaji ya raia kwa misingi ya ukabila yanayofanywa na vikosi vya serikali na waasi yamesambaa nchini Sudan Kusini.
https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcQGdcgD7Tbh8PY0HMjgZ3ybyuckiBgrgHtdSBG22F7D1TdgXp4tdwRipoti iliyotolewa na shirika hilo jana Alhamisi, ilisema uhalifu wa kutisha umefanywa dhidi ya raia, na kwamba uhalifu huo unaweza kufikia kiwango cha uhalifu dhidi ya ubinaadamu. 
Mgogoro wa Sudan Kusini ulianza mwezi uliopita, baada ya rais Salva Kiir kumtuhumu aliekuwa makamu wake, Riek Machar kwa kufanya jaribio la mapinduzi. 
Watu wanaokadiriwa kufikia 1,000 wameuawa katika mapigano kati ya wanajeshi watiifu kwa rais Kiir, na waasi wanaomuunga mkono Machar. 
Siku ya Jumatano, Uganda ilithibitisha kuwa iliwatuma wanajeshi wake kupigana kwa upande wa vikosi vya serikali ya Sudan Kusini.
Na DW.DESwahili
Mapigano bado yanaendelea Sudani Kusini

Mapigano bado yanaendelea Sudani Kusini

Watu waliokoseshwa makazi kufuatia mapigano huko Sudani Kusini wakiwa kwenye kambi ya ofisi za Umoja wa Mataifa-UNMISS Juba Dec. 22, 2013.
Watu waliokoseshwa makazi kufuatia mapigano huko Sudani Kusini wakiwa kwenye kambi ya ofisi za Umoja wa Mataifa-UNMISS Juba Dec. 22, 2013.

Wanajeshi waasi na majeshi ya serikali huko Sudan Kusini wanapigania udhibiti  wa mji wa Malakal, mji mkuu wa jimbo la Upper Nile lenye utajiri wa mafuta.

Mapambano katika mji huo yalianza Jumanne na kuendelea tena Jumatano, huku maafisa wa serikali wakikiri kuwa jeshi halina udhibiti kamili kwenye mji huo. Jumanne jioni baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lilipiga kura kwa ajili ya kupeleka walinda amani 5,500 wa ziada huko Sudan Kusini ambako ofisa mmoja wa Umoja wa Mataifa, Toby Lanzer alisema inaonekana kuwa maelfu ya watu wameuwawa katika mapigano ya siku 10 zilizopita.

Mashahidi wanasema watu wengi wanalengwa kwa kuwa wanatoka kabila la Dinka au Nuer. Katika ujumbe wa mkesha wa sikukuu ya Krismas, Rais Salva Kiir alitoa wito kwa wa-Sudan Kusini kusitisha ghasia zote za kikabila.

Wakati huo huo  ofisi ya Umoja wa Mataifa huko Sudan Kusini inakanusha ripoti kwamba kaburi moja lenye miili ya watu wengi liligundulika huko Bentiu  mji mkuu wa jimbo la Unity linaloshikiliwa na waasi. Ofisi ya haki za binadamu katika Umoja wa Mataifa ilisema Jumanne kwamba miili ya hadi wanajeshi 75 wa kabila la Dinka iligundulika huko. Lakini ofisi ya Umoja wa Mataifa inasema ripoti ilikuwa inatofautiana na uhalisia ambao ulielezea kuwepo vifo vya kiasi cha watu 15.


John KerryJohn Kerry
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry aliwataka wote Rais Kiir na mpinzani wake  Makamu Rais wa zamani Riek Machar hapo Jumanne akiwasihi kusitisha mapigano na kufanya mazungumzo ya kisiasa.

Viongozi wote wawili wanasema wapo tayari kwa mashauriano lakini serikali inakataa madai ya Machar kwamba kwanza viongozi wa upinzani waliokamatwa waachiwe. Bwana Kiir anayetoka kabila la Dinka anamshutumu Machar kutoka kabila la Nuer kwa kupanga jaribio la mapinduzi mjini Juba hapo Disemba 15. Machar hajadai kuhusika na mapinduzi lakini anasema jeshi linatakiwa kumuondoa bwana Kiir madarakani.

Marekani inasema marine 150 wamepelekwa Djibouti tayari kuingia Sudan Kusini kuwaondoa wa-Marekani na kulinda maslahi ya Marekani. 
Na VOASwahili
Viongozi wa IGAD wajadili mzozo wa Sudan Kusini

Viongozi wa IGAD wajadili mzozo wa Sudan Kusini

Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta (L) akiwa na viongozi wengine katika mkutano wa IGAD uliozungumzia mgogoro wa Sudan Kusini.
Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta (L) akiwa na viongozi wengine katika mkutano wa IGAD uliozungumzia mgogoro wa Sudan Kusini.

Kundi la kieneo barani Afrika linasema serikali ya Sudan  Kusini imekubali kusitisha mapigano hatua ambayo itasaidia kumalizika kwa mapigano ya makabila mbali mbali ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000 mwezi huu.

Jumuiya ya nchi za pembe za Afrika- IGAD ilitangaza uamuzi huo mwishoni mwa mkutano uliofanyika ijumaa mjini Nairobi. Kundi hilo liliwasihi wafuasi wa Makamu Rais wa zamani, Riek Machar  kufanya maamuzi kama hayo.

Mapigano yalianza huko Sudan Kusini mwanzoni mwa mwezi huu baada ya Rais Kiir alipomshutumu Machar kwa jaribio la mapinduzi.

Machar anasema ghasia zilikuwa matokeo ya ulipizaji kisasi wa  mahasimu  wa kisiasa wa bwana Kiir.

Ghasia hizo haraka ziliingia katika mtazamo wa kikabila huku wafuasi wa Rais Kiir wa kundi la kabila la Dinka wakipigana na kundi la wa-Nuer ambalo anatoka bwana Machar.

Katika mkutano wa Ijumaa, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alitoa wito kwa pande zote kufikia muafaka. “Tuna fursa ndogo sana kuhakikisha amani ambapo tunawasihi wadau wote kusitisha mapigano ikiwemo Riek Machar”.

Bwana Kenyatta anasema ghasia zinaweza kutishia uthabiti wa kieneo. “Kama ghasia za hivi sasa zinaendelea na ghasia za huko zinasababisha vifo dhidi ya raia, zitasababisha  mgogoro wa kiulimwengu ambao itakuwa  vigumu zaidi kwa sudan Kusini na eneo kufikia suluhisho”.


Rais Salva KiirRais Salva Kiir
Awali Rais Kiir na Machar wote walisema walikuwa tayari kwa mashauriano lakini serikali ilikataa madai ya Machar kwamba viongozi wa upinzani waliofungwa kwanza waachiwe.

Ijumaa shirika la habari la Reuters lilisema majeshi ya serikali yaliwazidi nguvu wapiganaji wanaomtii Machar huko Malakal, mji mkuu wa jimbo la Upper Nile linalozalisha mafuta.

Alhamisi  Umoja wa Mataifa ulisema ulitarajia  kupeleka jeshi la walinda amani huko Sudan Kusini katika muda wa ndani ya saa 48.

Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa, Hilde Johnson alielezea umuhimu wa haraka wa kuongeza jeshi la Umoja wa mataifa. Alisema zaidi ya raia 50,000 walitafuta hifadhi ya kisiasa kwenye vituo vya Umoja wa Mataifa nchini humo tangu mapigano yalipozuka.Johnson aliwasihi viongozi wa kisiasa nchini humo kuzungumza na majeshi yao na kufanya kazi pamoja ili kuleta amani. 

Na VOASwahili
 Uharamia umetokomezwa Somalia?

Uharamia umetokomezwa Somalia?


Mkondo wa uharamia katika bahari hindi
Uharamia katika pwani ya Somalia umepungua sana katika miaka sita iliyopita.
Ni visa 264 vya utekaji meli pekee vimeripotiwa.
Wataalamu wanasema uharamia umeshuka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na hali ilivyokuwa mwaka 2011.
Mwaka jana ni visa 15 pekee vya meli kutekwa vilivyoripotiwa, kwa mujibu wa shirika la kimataifa la safari za baharini IBM.
Shirika hilo linasema kuwa visa hivyo vimeshuka kutoka 75 mwaka 2012 na 237 mnamo mwaka 2011.
Walinzi waliojihami, manowari za kijeshi zinazoshika doria na uthabiti wa serikali ya Somalia ni miongoni mwa mambo yaliyochangia , kupungua kwa visa vya uharamia.

Pottengal Mukundan, afisaa mkuuu mtendaji wa IMB

"" Sababu mojawapo ya kupungua kwa uharamia duniani ni visa vya uharamia kutosikika kwa wingi katika fuo za pwani ya Afrika Mashariki.''"
Ripoti ya shirika hilo, inasema kuwa zaidi ya watu 300 walitekwa nyara mwaka 2013 huku wengine 21 wakijeruhiwa kwa risasi na visu.
Indonesia ndio iliathirika zaidi na uharamia mwaka jana ikiwa ni asilimia hamsini ya visa vyote vya uharamia vilivyoripotiwa duniani.
Katika kanda ya Afrika Magharibi, ni asilimia 19 pekee ya visa vya uharamia viliripotiwa.
Maharamia nchini Nigeria walitumia nguvu wakati wa mashambulizi yao wakati mwingine hata wakiwaua waathiriwa na kuwateka nyara watu 36.
Mwezi Novemba, ripoti ya Umoja wa Mataifa na benki ya dunia, ilisema kuwa maharamia katika ufuo wa pwani ya Somalia, walipata dola milioni 400 pesa zilizotolewa kama kikombozi kati ya mwaka 2005 na 2012.
Waelimishaji wa Kenya watatizwa juu ya matokeo mabaya ya wanafunzi wa shule za umma

Waelimishaji wa Kenya watatizwa juu ya matokeo mabaya ya wanafunzi wa shule za umma

Waelimishaji wanatatizwa juu ya kuendelea kwa matokeo mabaya ya wanafunzi wa shule za umma kwenye mitihani ya taifa baada ya zaidi ya asilimia 50 ya wale waliofanya mtihani wa masomo ya Cheti cha Elimu ya Msingi cha Kenya (KCPE) mwaka jana kupata alama za chini ya wastani.

  • Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Gitwe katika wilaya ya Eldoret wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya mkutano tarehe 26 Juni, 2009. [AFP]
    Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Gitwe katika wilaya ya Eldoret wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya mkutano tarehe 26 Juni, 2009. [AFP]
"Mwelekeo huu unaleta wasiwasi na kutatiza akili. Kwani wengi wa watoto wanaosoma shule za umma wameendelea kupata alama mbaya, Inakuwa wazi zaidi kwamba mtoto atafanya vizuri kama atakwenda shule binafsin za akademia, ambazo wengi wa watoto maskini hawataweza kumudu," Katibu Mkuu wa Chama cha Wazazi cha Taifa la Kenya Musau Ndunda aliiambia Sabahi.
Kwa mujibu wa data zilizotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia tarehe 31 Disemba, kati ya wanafunzi wa darasa la nane 839,759 ambao walifanya KCPE mwaka wa 2013, ambayo inatumika kama mtihani wa kuingia kidato cha kwanza, 467,353 walipata alama chini ya wastani, wakipata alama chini ya 250 kati ya 500.
Kati ya 467,353 ambao alama zao zilikuwa chini ya wastani, takribani 10,000 walipata chini ya 100 katika masomo matano yaliyofanyiwa mtihani, kwa mujibu wa wizara hiyo.
"Kinachoshangaza ni kwamba wengi wa wale waliopata alama za chini ya wastani ni watoto kutoka shule za umma, ambao wazazi wao hawawezi kumudu kuwapeleka shule binafsi," Ndunda alisema. "Kama mwelekeo huu hautabadilika kwa haraka, tutakuwa tukiwasukuma watoto wa kiume na kike wa maskini kushindwa."
Mpekethu Uniter Riziki, kutoka Shule ya Kulala ya Kathigiri huko Meru, ni mtahiniwa pekee kutoka shule za umma ambaye yumo miongoni mwa wanafunzi bora 100 kitaifa ambao waliopata zaidi ya alama 430. Mwanafunzi bora kabisa katika mtihani huo alipata alama 444. Riziki alipata alama 442.
Ndunda aliwalaumu walimu kwa matokeo mabaya, akiwatuhumu kwa kutotimiza kikamilifu majukumu yao.
"Kushughulikia hili, wizara ya elimu inapaswa kuwa na kozi ya lazima ya msasa kwa walimu wote, pamoja na wakuu wote wa shule kusaini mikataba ya matokeo," alisema.
Ndunda alisema hatua za kinidhamu zinapaswa kuzingatiwa dhidi ya walimu ambao wanafunzi wao wanaendelea kufanya vibaya katika mitihani ya taifa.
"Hatua za kinidhamu zijumuishe kushushwa cheo, kukatwa mshahara, na kuhamishwa kwa wale walimu watakaoshindwa kutoa matoke yanayofaa," alisema.
Matokeo mabaya katika mtihani wa hivi karibuni yalithibitisha utafiti wa Uwezo Kenya, jitihada ya miaka minne kuboresha lugha na ujuzi wa hesabu miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka 6 hadi 16 nchini Kenya.
"Mwaka 2012 utafiti wetu yalionyesha maendeleo kidogo katika uwezo wa kujifunza wa watoto," alisema John Mugo, Mratibu wa Nchi ya Kenya wa Uwezo
"Haiko mbali na ripoti zetu, ambazo zilionyesha kwamba wanafunzi wa darasa la nane hawawezi kufanya hesabu rahisi za darasa la pili, pamoja na kuzungumza na kuandika kwa usahihi Kiingereza na Kiswahili, ujuzi uliopatikana katika elimu ya awali ya msingi, kulikuwa na kuonyeshwa kwa matokeo mabaya katika hesabu na lugha katika mitihani ya KCPE ya 2013" Mugo aliiambia Sabahi.
"Viwango vya mafunzo vinapungua, pamoja na viashirio dhahiri vya [matokeo] mabaya katika shule zote za umma," aliendelea kusema. "Matokeo yetu na mtihani wa mwaka huu yameonyesha kwamba watoto na hususani [wale] wanaotoka katika shule za umma hawapati stadi za msingi katika kusoma na kuandika na katika hesabu."
"Walimu walio wengi katika shule za umma wanachagua kutokwenda shuleni, na kuwashangaza wale wanaoingia madarasani [hawatekelezi majukumu yao] wanapofundisha," Mugo alisema. "Matokeo yake hili limeathiri uwezo wa kujifunza wa wanafunzi kwa kuwa wanapata muda mdogo wa kukamilisha mitaala".
Mugo alitoa wito wa mchakato wa ufuatilia na tathmini kwa makini ambao utawahamasisha walimu kufundisha kutokana na mitaala, na kuwaomba wazazi wa wanafunzi wa shule za umma kujihusisha katika maendeleo ya watoto wao.

Wanafunzi wengi sana, hakuna walimu wa kutosha

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Taifa cha Walimu Kenya (KNUT) Wilson Sossion amewaondolea walimu lawama, akisema kwamba madarasa yaliyojaa sana ndiyo tatizo.
Akikiri kwamba ilikuwa usumbufu kuwa wanafunzi wengi walifeli mitihani na wanaweza wasiende shule za sekondari, Sossion alisema serikali ilaumiwe kwa kutoongeza idadi ya walimu katika shule za umma.
Tangu kuanzishwa kwa elimu ya msingi ya bure mwaka 2002, idadi ya wanafunzi wanaojiunga na shule imeongezeka, wakati ambapo idadi ya walimu imebakia ile ile, Sossion alisema.
"Ni makosa kuwalaumu walimu kwa waliofeli [wakati] serikali imekataa kuajiri walimu zaidi ili kuoanisha kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi," alisema.
Aliongeza kwamba serikali imeshindwa kugharimia kikamilifu sekta ya elimu ya umma.
"[Ugharimiaji] wa serikali kwa kila mwanafunzi umekuwa hautoshi na hii ni moja ya mambo ya msingi ambayo yanashusha matokeo ya shule za umma."
Licha ya kuajiri walimu zaidi na kuongeza ugharimiaji wa shule za umma, Sossion alisema kuna haja ya kuwapa motisha walimu kwa kuwalipa vizuri.
Waziri wa Elimu Jacob Kaimenyi alisema kwamba licha ya matokeo ya wanafunzi katika mitihani, shule za umma kwa ujumla zimeimarika katika matokeo ya jumla.
Kati ya shule 20 za kwanza zilizoimarika vizuri, 18 zilikuwa shule za umma, alisema.
"Kwa ujumla mwaka 2013 ulikuwa mwaka mgumu kwa shule za umma," aliiambia Sabahi, akieleza kwamba kufungwa kwa shule za umma wakati wa uchaguzi mkuu wa 2013 na mgomo wa walimu wa mwezi mmoja wa Julai vingekuwa na athari kubwa kwa matokeo ya wanafunzi.
"Kwa wakati huu hatuwezi kulaumu matokeo hayo mabaya katika jambo lolote," alisema, akiongeza kwamba wizara itafanya mkutano wa wadau mwezi ujao ili kutathmini mambo yote yanayochangia.
Wakati huo huo, Kaimenyi alisema serikali imeanzisha kozi ya ustadi ya walimu ambayo inadhamiria kuongeza ubora na matokeo ya shule kwa kuwataka walimu kuhudhuria kozi ya kupiga msasa na kupimwa katika umahiri wao.
Pia serikali katika wiki tatu zijazo itatekeleza ujumuishaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika [shule] za msingi ambapo tutatoa kwa wanafunzi wote wanaojiunga na shule za msingi za [umma] kompyuta ya mkononi ambayo itatumika kama chombo cha marekebisho ya mtaala ambacho kitabadilisha matokeo ya shule," alisema.
Utekelezaji wa programu ya kompyuta za mkononi ijulikanayo kama laptop, kulipiwa na fedha zilizokusudiwa kwa ajili ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais mwaka 2013, utatimiza moja ya ahadi za Rais Uhuru Kenyatta kwa siku zake100 madarakani.
Kaimenyi alieleza kwamba mradi wa kompyuta za mkononi utaongeza ari ya wanafunzi katika kujifunza, na kufanya kuwa rahisi kwao kuelewa masomo magumu.
Wanajeshi wa S.Kusini wakomboa Bentiu

Wanajeshi wa S.Kusini wakomboa Bentiu




Hli ya wakazi wa Sudan Kusini ni ya kusikitisha baada ya maelfu kukimbia vita
Taarifa kutoka Sudan Kusini zasema kuwa wanajeshi wa taifa hilo wamechukua udhibiti wa mji wa Bentiu kutoka kwa waasi watiifu kwa aliyekuwa makamu wa Rais wa nchi hiyo Riek Machar.
Msemaji wa kijeshi huko Juba ameiambia BBC kuwa majeshi ya serikali kwa sasa yamechukua usukani wa mji huo.

Hakuna taarifa iliyotolewa kuhusiana na majeruhi.Amesema kulikuwa na makabiliano madogo kwani waasi walikuwa wakitumia vifaru katika daraja moja nje kidogo ya mji huo.
Maelfu ya raia wamekimbia mji wa Bentiu ambao ni makao makuu ya jimbo lenye utajiri wa mafuta la Unity kabla ya serikali kuukomboa.
Mpatanishi mkuu katika mkutano wa mazungumzo ya kuleta amani huko Ethiopia anasema kuwa ana imani muafaka wa kukomesha vita utaafikiwa karibuni.
Na BBCSwahili
UN yamuasa Kiir kuwaachilia wafungwa

UN yamuasa Kiir kuwaachilia wafungwa



Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametishia kupeleka wanajeshi wake Sudan Kusini ikiwa Machar hatakubali kusitisha mapigano
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limemsihi Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir awaachilie huru wafungwa wa kisiasa ili aweze kumaliza mgogoro wa kisiasa unaotokota nchini humo.
Kiongozi wa waasi Riek Machar, anataka wafungwa 11 wa misiasa waachiliwe huru kabla ya kutia saini mkataba wowote wa Amani .

Serikali inasema inajiandaa kuukomboa mji wa Bor, ambao ni wa mwisho unaodhibitiwa na wanajeshi waasi wa Machar.Majeshi ya Machar ambaye pia alikuwa makamu wa zamani wa Rais nchini Sudan Kusini, yanaonekana kushindwa hasa baada ya serikali kukomboa mji wa Bentiu ambao walikuwa wameuteka.
Machar amesema kuwa atajitahidi kuendelea kuudhibiti mji wa Bor ambao ni mji mkuu wa jimbo la Jonglei lililo umbali wa kilomita 200 Kaskazini mwa Juba.
Machar aliambia shirika la habari la AFP kuwa wapiganaji wake walishindwa katika mji wa Bantiu kwa sababu ilikuwa nia yao kuzuia vita kwa lengo la kulinda maisha ya Raia.
Msemaji wa jeshi Philip Aguer anasema kuwa pande zote zimepata hasara kwani baadhi ya wapiganaji wao wameuawa katika vita hivi ambavyo vingali kupata suluhu.
Maelfu walilazimika kuutoroka mji wa Bentiu wakati jeshi la serikali lilipokuwa katika harakati za kuukomboa.
Na BBCSwahili
Mapigano mapya yahofiwa Sudan Kusini.

Mapigano mapya yahofiwa Sudan Kusini.



Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir akisalimiana na wananchi.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir akisalimiana na wananchi.

Maelfu ya watu wamekimbia mji mkuu wa Sudan Kusini wakihofia mapigano mapya baina ya wanajeshi waasi na serikali.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa zaidi ya watu elfu moja wameuwawa na wengine laki mbili wamekoseshwa makazi kutokana na mapigano hayo yaliyodumu kwa wiki tatu sasa. Rais wa shirika la kimataifa la msalaba Mwekundu , Peter Maurer amemaliza ziara ya siku tatu nchini humo akitembelea makambi ya wakimbizi.

Anasema kitu kilichomshangaza ni kwamba watu walioondoka katika makazi  yao wameacha kila kitu nyuma na kwenda katika makazi mapya bila mali zao wakati huo huo mazungumzo ya amani katika nchi jirani ya Ethiopia bado hayajafanikiwa huku serikali ikikataa madai ya waasi kuwaachilia wafungwa 11 wa kisiasa.

Na Voa swahili
Al Shabaab yaharamisha Internet

Al Shabaab yaharamisha Internet


Shabaa limetoa makataa ya siku kumi na tano kwa wanaotoa huduma za internet kuzifunga
Wanamgambo wa Al Shabaab wenye uhusiano na Al-Qaeda, wamesema kuwa wamepiga marufuku raia wanaoishi katika maeneo wanayodhibiti kutumia internet.
Wapiganaji hao wametoa onyo kwa kampuni zote zinazotoa huduma ya internet siku 15 kufunga biashara zao.
"kampuni yoyote au mtu yeyote atakayepatikana akipuuza onyo hilo atajulikana kama mtu anayewafanyia kazi maaduzi zetu, na ataadhibiwa kulingana na sheria za ziisilamu,'' ilisema taarifa ya kundi hilo ambayo ilitumwa kwenye mitandao yake.
Wanamgambo hao hutumia sheria kali za kiisilamu katika maeneo wanayotawala na kuwakamata watu mara kwa mara kwa tuhuma za kufanya ujasusi.
Internet hutumiwa sana nchini Somalia, taifa ambalo limekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa zaidi ya miongo miwili, huku kundi hilo likionekana kuwa kikwazo kikubwa kwa amani.
Kundi la Shebab zamani lilikuwa likitawala katika sehemu kubwa za Kusini mwa Somalia na Kati, lakini likaondoa wapiganaji wake baada ya kushindwa na wanajeshi wa Muungano wa Afrika wanaopambana nao.
Majeshi ya Afrika ikiwemo wanajeshi kutoka Uganda, Burundi na Kenya, tangu hapo wamedhibiti sehemu kadhaa kutoka kwa wapiganaji hao.
Lakini mashambulizi ya kuvizia yanayofanywa na kundi hilo dhidi ya maslahi ya majeshi ya serikali na yale ya kigeni, yameondoa matumaini ya kunusuru taifa hilo kutokana na vita vya miaka mingi.
Somalia: Adhabu ya mauaji ni kifo

Somalia: Adhabu ya mauaji ni kifo




Wanajeshi zaidi Somalia watapata hukumu sawa na hii kwa kutenda uhalifu bila kujali
Mwanajeshi mmoja nchini Somalia ameuawa kwa kupigwa risasi na kikundi cha wanjeshi na polisi mjini Mogadishu , baada ya mahakama ya kijeshi kuamuru kuuawa kwake.
Uamuzi wa mahakama ulitokana na madai kuwa mwanajeshi huyo alimuua mwanafunzi mwaka jana.
umati wa watu wakiwemo watoto walishuhudia kuuawa kwa mwanajeshi huyo, katika kituo cha mafunzo cha wanajeshi mjini Mogadishu kwa mujibu wa picha zilizowekwa kwenye mtandano wa kisomali wa redio Shabelle.
Hukumu ya mauaji nchini Somalia ni kifo.
Wanajeshi wa serikali mara kwa mara hutuhumiwa kwa kufanya vitendo vya uhalifu bila kujali ikiwemo mauaji na ubakaji.
Kituo cha Redio kiliripoti kuwa wanajeshi zaidi watakaopatikana na hatia ya mauaji huenda wakakabiliwa na adhabu sawa na hiyo katika siku zijazo.
Maslah Isse Jimaan alihukumiwa kifo baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mwanafunzi wa shule katika soko rasmi la Bakara, alipokuwa anashika doria mwaka jana.
Aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi pamoja na wanajeshi kumi walioonekana katika picha hiyo kabla ya Jimaan, kufumbwa macho na kufungwa kwenye mlingoti na kisha kupigwa risasi mbele ya umati wa watu.
'Jimaan alikuwa amekiuka kanuni za jeshi, na hii ndio ilikuwa adhabu yake,' alisema mwenyekiti wa mahakama ya kijeshi Libaan Ali Yarow.
Hata hivyo bwana Yarow alisema kuwa hakua na habari kuwa Jimmah aliuawa mbele ya watoto.
Na BBCSwahili

Kategori

Kategori