Showing posts with label 2017 at 01:54PM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 01:54PM. Show all posts
MANENO YA SPIKA NDUGAI BAADA YA WABUNGE KUSUSIA FUTARI ALIYOANDAA

MANENO YA SPIKA NDUGAI BAADA YA WABUNGE KUSUSIA FUTARI ALIYOANDAA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Job Ndugai amewakumbusha wabunge wa vyama vya upinzani hasa vinavyounda UKAWA umuhimu wa jamii kukaa pamoja, kujadiliana na kumaliza tofauti zao.
Ndugai ambaye ni mmoja wa wabunge wa Bunge la 11 aliyasema hayo baada ya baadhi ya wabunge hasa wa upinzani kususia futari aliyoiandaa siku ya Jumanne kwa ajili ya wabunge wote. Kiongozi huyo wa juu wa mhimili huo alisema kuwa licha ya jukumu zito la kujadili na kupitish bajeti ya serikali ya 2017/2018, ushirikiano kwa jamii ni muhimu.
Jambo hilo lilmfanya asiwe na raha na kuamua kuzungumzia ndani ya bunge kwa upole kabisa ambapo alisema kuwa, baada ya kuhudhuria futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu Jumatatu, na baada ya kuwepo tetesi za kususia ya kwake alisema, amejifunza kuwa baadhi wamekatazana kuhudhuria shughuli kama hizo.
“Lakini nikajifunza kitu kimoja ambacho sikupenda kukisema, ila nikiseme hapa kidogo. Kuna wenzetu wamekatazana rasmi kuhudhuria shughuli kama hizi.”
Ndugai aliyasema hayo Jumanne wakati akihitimisha kipindi cha maswali na majibu kabla ya kupisha mapumziko na kisha kupigiwa kura kwa bajeti ya serikali.
Bunge linaendeshwa kwa mawasiliano ya namna mbalimbali baina ya wabunge na uongozi. Endapo kuna jambo linakwaza na kusababisha watu wasipate futari pamoja, ni vizuri wakae pamoja na kuondoa jambo hilo, alizungumza Ndugai.
Licha ya kutoa tahadhari hiyo, Ndugai alisema kuwa wabunge hao wana uhuru wa kufanya hivyo (kutohudhuria) kama wanaona ni sawasawa.
“Siyo mwezi wa chuki na kubaguana. Niwakaribishe tena kwenye futari kwa watakaoweza kufika. Watakaoshindwa In Sha Allah, kila la heri. Tutaendelea kuwa pamoja mjengo huu huu,” alisema Spika Ndugai akihitimisha nasaha zake.
Chanzo: Mwananchi
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rPXgYU
via IFTTT


Amber Lulu: Bila Pombe Kali Siimbi, Siuzi Nyago!!

Amber Lulu: Bila Pombe Kali Siimbi, Siuzi Nyago!!

VIDEO Queen ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva amefungukia kazi zake kuwa bila kutumia kinywaji cha pombe kali kabla ya kuimba ama kuuza nyago kwenye video hawezi kufanya vizuri kwani atashindwa kuchetuka.
Akibonga na Ijumaa juzikati, Amber anayetikisa na Wimbo wa Watakoma alisema, mara nyingi atumiapo pombe kali humpa stimu ya kufanya kazi vizuri na pia ipo kwenye ‘damu.’

“Sijajua kwa nini yaani lakini nikitumia pombe kali huwa zinanipa stimu kinoma ya kufanya kazi zangu na bila hizo siimbi wala kushiriki freshi kwenye uandaaji wa video,” alisema Amber.

from Blogger http://ift.tt/2nKQWyP
via IFTTT


DR Slaa Aibuka…Afikiria Kurudi Tanzania…Adai Watanzania Wamvumilie Rais Magufuli

BAADA ya kuishi nchini Canada kwa zaidi miaka miwili sasa, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa amesema anakuna kichwa ili kupima mazingira yaliyomfanya aondoke nchini na familia yake kama yapo au laa.
Septemba,2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu Dk. Slaa alijiweka kando na siasa, kwa kile alichokieleza kutofautiana na chama chake juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),Edward Lowassa.
Hata hivyo Dk. Slaa ambaye amekuwa mbunge wa Karatu kwa vipindi vitatu mfululizo, hakuweza kuainisha mazingira yaliyomfanya aondokea nchini na kwenda kuishi ughaibuni.
“Sina tabia ya kuyumbishwa…sina chuki na mtu yeyote, sipendi siasa za udanganyifu na propaganda. Nimeachana na siasa tangu Julai 28,2015, baada ya kuona misingi ya chama nilichoshiriki kukijenga imepotoshwa,”alisema Dk. Slaa siku alipotangaza kuachana na siasa.
Pamoja na mambo mengine, alisema sharti la kwanza ambalo alitaka Chadema izingatie ni kiongozi huyo wa zamani ndani ya serikali ya CCM, kujisafisha dhidi ya tuhuma ya kashfa ya sakata la Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond aliyohusishwa nayo akiwa Waziri Mkuu.
Kurudi nchini
Akizungumza na MTANZANIA akiwa nchini Canada jana, Dk. Slaa alisema amemaliza masomo yake na baada ya kufanya tafakari atarejea nchini wakati wowote.
“Ni kweli nimemaliza masomo yangu. Bado napima mazingira yaliyonifanya niondoke na familia yangu. Baada ya hapo tutaangalia uwezekano wa kurejea,”alisema.
Alisema kuhusu matarajio yake ya kisiasa, watu wameshindwa kumwelewa siku ambayo alitangaza kustaafu siasa za vyama.
Alisema alichomaanisha ni kwamba, pamoja na kuachana na siasa za vyama,atakuwa tayari kupiga kelele pale anapoona masilahi ya Taifa yanaumia.
“Hadi sasa sijapiga kelele kwa kuwa sijaona masilahi ya Taifa yakiangamizwa, hatua mbalimbali zinazochukuliwa ni kweli zinawaumiza wasiohusika.
“Ndio maana nilitumia katika makala mojawapo mtego wa panya huwakamata wanaohusika na wasiohusika. Hivyo, makosa madogo mimi hayanisumbui kwa kuwa hakuna binadamu kamilifu ,”alisema.
Rais Magufuli
Akizungumzia utendaji wa Rais Dk. John Magufuli, alisema watu waelewe hakuna nchi hata moja ambapo kiongozi atakubalika na watu wote kwa asilimia 100.
Alisema wako watu ambao masilahi yao yataguswa kwa namna moja au nyingine hivyo lazima watapiga kelele.
Kutokana hilo, alisema Rais Dk. Magufuli katika kundi ambalo halihitaji fedha ameyatekeleza yote kwa asilimia 99.9, ikiwa ni pamoja na uwajibikaji serikalini, kuchukua hatua kali dhidi ya rushwa, uwizi wa mali za umma, uwindaji haramu na kudhibiti dawa za kulevya.
“Hatua zote zimechukuliwa,zinapaswa kuwa endelevu. Kwa bahati mbaya mchwa wengine waliopenya mpaka ndani ya Ikulu na Serikali na huwezi kufagia Serikali nzima kwa siku mmoja.
“Kwa jinsi Rais ambavyo hayumbi na wala hayumbishwi, nina hakika atafikia malengo na kurudisha Taifa kwenye misingi ya tunu za Taifa ya uwazi, ukweli, uadilifu, kuheshimiana na kuthaminiana na hasa kujali utu.
“Hii ndiyo hali ambayo JPM kila siku anaiita ‘Transition’ (kipindi cha mpito). Tutafika tu, tunatakiwa kuwa wavumilivu na wenye uzalendo wa kweli ana nia njema ya kufikisha Taifa mahali pazuri. Hii inahitaji kuweka pembeni maslahi yetu binafsi kama mtu mmoja mmoja, viongozi wa Serikali au hata wa kisiasa,”alisema Dk. Slaa.
Upinzani
Kuhusu mwenendo huo endapo utasaidia upinzani kuingia Ikulu 2020, Dk. Slaa alisema wakija na ajenda mbadala na makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja itawasaidia.
Dk. Slaa ambaye pia alipata kugombea urais kupitia Chadema mwaka 2010, alisema endapo wataendelea kurukia kauli za Rais, basi upinzani utafutika kabla ya 2020. 
“Kama nilivyorejea mara kadhaa, upinzani makini utaingia Ikulu kwa ajenda mbadala. Ajenda makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja katika kuwatoa kwenye kero zao mbalimbali.
“Hadi sasa ninachoona ni ‘kurukia’ kauli za JPM, lakini kauli si ajenda na hatupeani maksi kwa kuzungumzia usahihi wa lugha. Wako wanaotazama usahihi wa lugha na mahali pa kutazama usahihi huo. Kimsingi hayo ni masuala ya darasani au kwenye uandishi wa vitabu.
“Aidha kumtuhumu JPM kukiuka Katiba na sheria nayo haina tija. Wote wanaomtuhumu wanajua kuwa wakiambiwa waonyeshe kifungu mahususi alichokiuka yeye mwenyewe katika utendaji wake hawana majibu ya kuridhisha.
“Hivyo mimi sijaona mwenendo wa JPM unaosaidia kuingiza upinzani Ikulu. Isitoshe kama hawatakuja na ajenda makini na mkakati ulioandaliwa unaowatoa wananchi hapa walipo kwenda kwenye raha, upinzani unaweza kufutika kabla ya 2020,”alisema Dk. Slaa.
Tazama video Mtoto amvua kofia
 Papa Francis

from Blogger http://ift.tt/2nGR7OU
via IFTTT


Kalianzisha Tena..Lema Achochea Vyama vya Upinzani Kufanya Haya Dhidi ya Utawala wa Rais Magufuli…!!!

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amekuja na staili mpya katika ulingo wa kisiasa mara hii akihimiza ushirikiano wa wapinzani kudai utawala bora.
Lema amesema hayo wakati akizungumza kwenye mkutano wa kumbizi ya miaka 50 ya Azimio la Arusha mjini hapa, akisema huu ni wakati wa vyama vya upinzani kushirikiana.
Lema alisema amehudhuria mkutano huo kutokana na kampeni ya ushirikiano wa vyama vyote vya upinzani waliokubaliana kupinga mwenendo wa Serikali.
“Mkiwa na mkutano semeni niwaalike na wanachama wa Chadema waje wawape ushirikiano, lengo letu ni kuhakikisha haki inatendeka bila matabaka ya walionacho na wasionacho wala makabila,” amesema.
Katika mkutano huo, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amezungumzia ukwepaji kodi unaofanywa na wafanyabiashara wakubwa na kusema kuna idadi kubwa ya kampuni za uwekezaji ambazo zinafanya hivyo.
TAZAMA HARMORAPA ALIVYO TIMUA MBIO BAADA YA KUIONA BASTOLA

from Blogger http://ift.tt/2njILv1
via IFTTT


Kategori

Kategori