Showing posts with label 2017 at 01:53PM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 01:53PM. Show all posts
Idris Sultan Apata Shavu la Kucheza Movie Hollywood Marekani

Idris Sultan Apata Shavu la Kucheza Movie Hollywood Marekani

Baada ya wiki ya mchakato wa usahili, Mshindi wa Big Brother Africa-Hotshots wa 2014, Idris Sultan ataonekana katika filamu ya ‘Ballin …On the Other Side of the World,’ itayoandaliwa nchini Marekani chini ya muongozaji Harvey White.
Muongozaji wa filamu hiyo aliwahi kufanya kazi na wasanii wenye majina makubwa akiwemo Chris Brown, Mariah Carey, Lady Gaga na Tamia.
Akiwa kama mhariri wa filamu, amehariri baadhi ya filamu kama vile ‘Think Like A Man 2,’ ‘The Wedding Ringer,’ na ‘King of the Dance Hall’ akishirikiana na Whoopi Goldberg.
Hadithi ya filamu hiyo imetungwa na Torino Von Jones, ambapo hadithi hiyo inamhusu kijana mdogo wa Kenya (Kunjani), ambaye wazazi wake ni waathirika wa uhalifu uliojaa vurugu.
Siku moja katika maeneo ya ya shule, kijana huyo aliye na umri wa miaka kumi na tatu aligunduliwa na padri wa Kimarekani ambaye alimwona akicheza mpira wa kikapu na akaamini ana uwezo mkubwa na anaweza kushirikia ligi ya NBA.
Wote wawili waliendelea na urafiki wao na padri huyo alianza kumpatia ushauri. (King) itaigizwa na Sultan, ana haiba kubwa,lakini ni mhalifu mkubwa na hatari sana ambaye ana wazo jingine na anataka Kunjani kujiunga na kundi lake la wahalifu na atafanya kila liwezekanalo ili mpango huo ufanikiwe.
Mara ya mwisho Sultan alionekana katika filamu ya Tanzania ‘Kiumeni,’ ambayo itaoneshwa katika tamasha lijalo la wiki ya filamu la Zanzibar (ZIFF) ambapo ‘Kiumeni’ itaoneshwa wakati wa Siku ya tamasha ya filamu za Kiswahili ya ZIFF Julai 14, na mtayarishaji na nyota wa filamu Ernest Napoleon.
Mapema mwaka huu, Napoleon aliweka historia wakati alipochaguliwa kuwa rais wa kampuni ya uzalishaji na usambazaji wa filamu ya Marekani ya D Street Media Group yenye makao yake jijini New York, pamoja na ofisi katika miji ya Berlin, Buenos Aires na Cape Town.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa D Street na mtayarishaji mtendaji Dexter Davis walimtambua Idris kutokana na kuiangalia filamu ya “Kiumeni’.
“Idris Sultan has what it takes to become an international star and our upcoming film ‘Ballin… On the Other Side of the World’ is a perfect fit. We’re considering Mr. Sultan for other movies as well, alisema Davis.
Kampuni hiyo ya filamu inaazimia kupiga picha sehemu za Marekani na Kenya na haitachelea kutafuta vipaji vingine kwa waigizaji wa Kenya na nchi nyingine za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania pale inapolazimu.
Filamu hiyo imeandaliwa kwa bajeti ya Dola za Marekani milioni tano.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2ukTQ1P
via IFTTT


Chagua Kufanya Mambo Haya, Ili Yakupe Mafanikio Makubwa

Chagua Kufanya Mambo Haya, Ili Yakupe Mafanikio Makubwa

Siku zote maisha ya binadamu yanaongozwa na uchaguzi tunaoufanya kila siku. Uchaguzi huo ndio unatufanya tuwe na maisha haya au yale. Kama uchaguzi unaoufanya ni mbovu kila siku, basi ni wazi na maisha yatakuwa mabovu vilevile. Na kama uchaguzi wako ni mzuri, halikadharika na maisha yako yatakuwa mazuri vivyo hivyo.
Kitu cha kuwa makini nacho hapa, angalia uchaguzi unaoufanya kila siku na kila wakati. Uchaguzi huo ndio unaoamua maisha yako ya kesho yaweje. Kama ni hivyo, ni lazima kwetu kufanya uchaguzi utakaotupa maisha bora. Jaribu kujiuliza, ni uchaguzi wa mambo gani unaotakiwa kuufanya ili kukupa mafanikio makubwa?
1. Chagua kutumia fursa vizuri.
Kwa fursa yoyote inayojitokeza mbele yako, jifunze kuitumia vizuri. Kama ni fursa ya kibiashara au elimu itumie vizuri mpaka uone mafanikio yake. Acha kucheza na fursa yoyote ya kimafanikio inayojitokeza mbele yako. Ikiwa utafanya hivyo elewa ni lazima ipo siku utakuja kujuta kwa uamuzi ulioufanya leo.
Kuna watu ambao wameshindwa kufanikiwa kwa sababu ya kutokuwa makini na fursa zilizojitokeza kwao. Bila shaka umeshawahi kuwaona watu hawa ambao wana majuto na majonzi makubwa kila wakikumbuka ujinga walioufanya. Hili ni tatizo linalosababisha ndoto za wengi kukwama. Ili ufanikiwe, jifunze kutumia kila fursa vizuri.
2. Chagua kuishi na watu chanya.
Siku zote ukiwa mtu wa kuishi na watu hasi basi ni wazi utapata matokeo wanayopata watu hao. Kama ni kulalamika, kulaumu ama kukosa mafanikio, utapata matokeo kama hayohayo. Hakuna kikubwa utakachoweza kukibadilisha. Mara nyingi maisha yetu yanathiriwa sana na wale watu wanaotuzunguka.
Siri kubwa ya mafanikio ipo kwenye watu wanaokuzunguka pia. Sio rahisi kuishi na watu hasi, halafu ukategemea mafanikio, sahau hilo. Ni lazima watakurudisha nyuma. Watu wenye mafanikio makubwa wanalijua hili. Hata wewe ukitaka kufanikiwa chagua kuishi na watu chanya. Utajifunza mengi huko na utafika mbali kimafanikio.
3. Chagua kufanya kazi kwa bidii.
Kitu kitakachokutoa hapo ulipo na kukufanikisha ni kufanya kazi kwa bidii. Kazi yoyote unayoifanya jitoe kuifanya kwa nguvu zote mpaka uifanikishe. Acha kufanya kazi kwa mkono mlegevu utajikwamisha kwenye kwa mambo mengi kuliko unavyofikiri. Ile hali ya uvivu uliyonayo jitahidi uitoe na kisha endelea kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii.
Watu wenye mafnikio makubwa siku zote wanafanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kuona mipango na malengo yao yanatimia. Kumbuka hakuna kitu utakachokipoteza ikiwa utajitoa kwa moyo kufanya kazi zako kwa bidii. Zaidi utajiongezea ujuzi, maarifa na uzoefu mkubwa utakaoutumia leo na kesho kwa maisha yako.
4. Chagua kukabiliana na matatizo na kuyashinda.
Tatizo lolote unalokabiliana nalo unao uwezo wa kulishinda. Hakuna tatizo lilokubwa kwako ambalo linaweza likakushinda. Kwa kulijua hilo chukua jukumu la kuchagua kukabiliana na tatizo lako na acha kuruhusu hata kidogo hilo tatizo likakushinda.
Tumia uwezo wako mkubwa wa akili uliopewa, tafakari kisha tafuta njia sahihi za kuweza kukabilana na tatizo lako. Kwa kufanya hivyo utakuwa mshindi na hakuna ambacho kitashindikana kwao. Wanamafanikio wote siku zote huwa ni watu wakukabiliana na matatizo yao na siyo kuyakimbia.
5. Chagua kujifunza.
Ipo haja ya kutafuta mafanikio huku ukiwa unajifunza. Unapojifunza inakusaidia kujua mambo mengi sana ambayo utayatumia katika safari yako ya mafanikio. Huu ni uchaguzi muhimu sana kuufanya ili kujihakikishia nafasi kubwa ya mafanikio katika maisha yako. Jifunze kupitia vitabu, semina au warsha mbalimbali itakusaidia sana.
Hivi ndivyo ambavyo unaweza ukachagua mambo haya na yakawa nguzo na msaada mkubwa wa mafanikio siku zote.
Nikutakie ushindi katika safari yako ya mafanikio na kumbuka tupo pamoja.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2u5YQap
via IFTTT


RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI ZA SIKUKUU YA EID EL-FITR

RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI ZA SIKUKUU YA EID EL-FITR

Rais John Magufuli ametoa zawadi za Eidd El Fitri zenye thamani ya Sh10.9 milioni kwa vituo tisa vya wenye mahitaji maalumu vya Mkoa wa Dar es Salaam.
Pia, ametoa zawadi hizo katika vituo viwili vya Zanzibar na vituo 13 kutoka mikoa ya Tanzania Bara.
Zawadi hizo zimekabidhiwa leo (Jumamosi) katika mahabusu ya Watoto iliyoko Upanga jijini Dar es Salaam na Kamishina Msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto, Simon Panga kwa niaba ya Rais.
Panga amezitaja zawadi zilizotolewa kuwa ni mchele, mbuzi na mafuta ya kupikia ambazo zitawezesha makundi hayo kufurahi na kusherehekea sikukuu kama ilivyo kwa watu wengi.
“Mheshimwia Rais kwa upendo wake wa dhati kabisa ameona umuhimu wa kushiriki pamoja na watu walio katika makundi maalum wakiwamo watoto walio katika mazingira hatarishi na wazee wenye ulemavu wasiojiweza, wanaohudumiwa katika makazi, ili washerehekee sikukuu hii vizuri ,” amesema Panga.
Pia, amevitaja vituo vilivyonufaika na zawadi za Rais kuwa ni kwa upande wa Jiji la Dar es Salaam kuwa ni Makao ya Taifa ya Watoto Yatima Kurasini – Temeke, Makao ya Watoto IBN Kathry­ Ilala, Makao ya Watoto Yatima Msimbazi, Makao ya Watoto Yatima Chakuwama, Makao ya Watoto Yatima Group Trust Fund – Temeke na Makao ya Watoto Yatima Dar Al Arqum (International Islamic Relief Organization).
Vingine ni Mahabusu ya Watoto Dar es Salaam – Upanga, Makazi ya Wazee na Wasojiweza Nunge – Kigamboni na Shule ya Ufundi ya Watoto Wenye Ulemavu Yombo.
Vile vile, amevitaja vituo vilivyonufaika kwa upande wa mikoa ya Tanzania Bara kuwa ni Makao ya Watoto Tosamaganga – Iringa, Makao ya Watoto Yatima Malaika Kids Home, Mkuranga – Pwani, Makao ya Watoto Yatima Karibu Nyumbani, Kibaha – Pwani, Makao ya Watoto Yatima Miyuji Cheshire – Dodoma na Shule ya Maadilisho Irambo – Mbeya na Mahabusu ya Watoto – Mbeya.
Vituo vingine ni Mahabusu ya Watoto – Arusha, Makao ya Wazee na Wasiojiweza Kolandoto – Sinyanga, Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Ngehe – Ruvuma, Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Kiilima – Bukoba, Kagera, Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Magugu – Manyara, Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Ipuli – Tabora, Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Bukumbi – Mwanza.
Kwa upande wa Zanzibar, vituo vilivyonufaika ni Kituo cha Watoto Yatima Mabaoni – Chakechake – Pemba na Makazi ya Wazee na Wasiojiweza Sebleni – Unguja.
Utoaji wa zawadi hizo ni utaratibu unaofanywa na marasi wa awamu zote zilizopita zilizopita
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2s51yQ0
via IFTTT


Mpambe wa Diamond Platnumz Afukuzwa WCBโ€ฆZari Ahusika

Mpambe wa Diamond Platnumz Afukuzwa WCB…Zari Ahusika

Aliyekuwa mwanamitindo wa Diamond Platnumz na timu ya WCB, Q Boy Msafi amethibitishwa kutokuwapo ndani ya lebo hiyo baada ya kufutwa kazi kutokana na kosa alilofanya.
Q Boy amesema kuwa alifanya kosa ambalo linahusu gari la Zari (mpenzi wa Diamond Platnumz) na licha ya kuwa kosa lile ni la kibinadamu kwamba yeyote angeweza kulifanya, lakini uongozi wa WCB uliamua kumfuta kazi.
Q Boy alitoa kauli hiyo akifanya mahojiano na kituo kimoja jijini Dar es Salaam ambapo alisema kwa sasa anajikita zaidi katika kazi zake za muziki, na pia anawashukuru mashabiki kwa kumpokea vizuri.
Akizungumzia uhusiano wake na WCB, Q Boy amesema wale ni kama ndugu zake, hana ugomvi nao na kuwa wamekuwa msaada kwake hata baada ya yeye kutoka.
Amefafanua kwamba, hata alipotoa wimbo wake, timu ya WCB haikusita kumsaidia katika mambo mbalimbali. Lakini pia aliweka bayana kwamba yeye ndio anaanza muziki, na anategemea msaada wao sana ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wasanii wa WCB kama Rayvanny, Rich Mavoko, Harmonize hivyo hawezi kuwa na ugomvi nao.
Aidha, Q Boy amesema kuwa uongozi wa WCB umemtaka aendelee na kazi zake za muziki, na endapo patakuwa na uhitaji wowote wa masuala ya mitindo basi watamtafuta.

from Blogger http://ift.tt/2qmOZu0
via IFTTT


Breaking News: Rais Magufuli Amtaka Profesa Muhongo Aachie Ngaza Kutokana na Ripoti ya Makontena ya Mchanga

Breaking News: Rais Magufuli Amtaka Profesa Muhongo Aachie Ngaza Kutokana na Ripoti ya Makontena ya Mchanga

Kutokana na Madudu ya yaliyowekwa wazi na Taarifa ya Makontena ya Mchanga aliyokabithiwa Rais Leo hii, Rais Magufuli amemtaka Waziri Professor Dr. Sospeter Muhongo ajitasmini upya na amemtaki aachie ngazi
JPM Amenukuliwa akisema haya:
“…… .. Ni rafiki yangu lakini katika hili, 
Ajitathmini, Ningetaka ajiudhulu”-
JPM.

from Blogger http://ift.tt/2rgsxHP
via IFTTT


Maajabu.. Waungua kwa Kuchomwa Moto Bila Nyumba Kuungua.. Inasadikika Walifumaniwa..!!!

Maajabu.. Waungua kwa Kuchomwa Moto Bila Nyumba Kuungua.. Inasadikika Walifumaniwa..!!!

Watu 2 wa jinsia ya kike na Kiume ambao bado majina yao hayajatambulika wamekutwa wamepoteza maisha katika Kitongoji cha Elkiurei Kata ya Kiranyi wilayani Arumeru kwa kile kinachosemekana kuwa ni ajali ya moto.
Akithibitisha tukio hilo mwenyekiti wa kitongoji hicho Bwana Enesphori Chami amesema kuwa tukio hilo ni la kushangaza kwasababu wamekuta marehemu hao katika mazingira ya ya kujiuliza maswali mengi kwa kuwa mwanaume alikuwa amefungwa kamba mikononi jambo lonaloleta utata kuelewa nini kilikuwa kinaendelea.
Bwana Chamia amesema marehemu hao walikuwa mwanaume na mwanamke wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka kata ya 30 na 35 lakini kinachoshangaza wameungua wao pamoja na Godoro jambo ambalo linatia wasiwasi majirani waliokuwa eneo hilo.
Naye shuhuda aliyejionea tukio hilo amesema kuwa walilazimika kuvunja mlango kwa kuwa ulikuwa umefungwa kwa ndani lakini dirisha lilikuwa limefunguliwa jambo ambalo hawajaelewa kwasababu marehemu hao mwanaume alikuwa amefungwa kamba.
Shuhuda huyo amesema kuwa Mwanamke huyo anajulikana kwasababu wako naye siku zote lakini mwanaume anaonekana kuwa ni mgeni kwasababu hawajawahi kumuona na mwanamke alikuwa anaishi peke yake.
Naye Diwani wa kata ya Kiranyi Bwan John Seneu amesema kuwa tukio hilo ni la kushangaza kwasababu kama ni nyumba kuungua ingeteketea yote lakini kilichoungua ni godoro peke yake kitu kinachoendelea kuwafanya wananchi kuwa na maswali mengi.
Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa makini Na matukio kama haya na kutambua wageni wanaowatembeleakatika maeneo yao 
Pamoja na hayo jeshi la polisi linaendelea na upelelezi ili kubaini chanzi cha tukio hilo la kusikitisha.

from Blogger http://ift.tt/2qfIjhO
via IFTTT


Donald Trump Aanza Unyama..Aamuru Syria Ipigwe Makombora

Donald Trump Aanza Unyama..Aamuru Syria Ipigwe Makombora

Marekani imefanya shambulizi la makombora takriban 50 ,yalipigwa katika kambi ya jeshi la anga mjini Homs nchini Syria.
Awali maafisa wa Marekani walisema wana mpango wa kuchukua hatua za kijeshi baada ya Syria kushutumiwa kutumia silaha za kemikali katika mji unaodhibitiwa na waasi, ambapo watu kadhaa wamepoteza maisha.
Mashambulizi hayo yametekelezwa kutoka kwenye meli za kijeshi za Marekani katika bahari ya Mediterranea.
Rais wa Marekani Donald Trump amesema ameamuru kutekelezwa kwa mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Syria huku akitoa wito kwa mataifa yote yaliyostaarabika kukomesha vitendo vya mauaji na umwagaji damu nchini humo
Naye mshirika wa Syria Urusi ametahadharisha madhara yatokanayo na hatua zozote za kijeshi zinazochukuliwa na Marekani dhidi ya Syria.
Hata hivyo Rais Donald Trump amsema kuwa ,kutumia gesi hatari kuua raia wakiwemo watoto wengi, utawala wa Syria ulikuwa umevuka mipaka.
Mike Pregent ni mchambuzi wa masuala ya mashariki ya kati ameiambia BBC kuwa mashambulizi hayo yametoa ujumbe mzito kwa Assad.
Shambulio hilo linawapa Watu wa Syria matumain, na ninachomaanisha ni kuwa haya hakika haya ni Mashambulizi dhidi ya vikosi vya anga vya Assad, silaha za kemikali, pengine dhidi ya hifadhi za mafuta halikadhalika.hivyo haikuwa dhidi ya raia, haikuwaweka marubani wa kimarekani hatarini. Ulikuwa ujumbe maalum kwa Assad kuwa usitumie jeshi lako la anga kuwaadhibu raia, hivyo nafikiri ni ujumbe wenye nguvu

from Blogger http://ift.tt/2oIgX76
via IFTTT


Kimenukaa Cuf..Maalim Seif Ampasua Prof Lipumba..Atoa Kauli Hii Nzito kwa Hasira ..!!!

Kimenukaa Cuf..Maalim Seif Ampasua Prof Lipumba..Atoa Kauli Hii Nzito kwa Hasira ..!!!

VITA vya maneno vimezidi kushika kasi ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) na sasa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, ameibuka na kumtaka aliyekuwa mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba, amwache kwa kuwa hana uwezo wa kumfukuza kazi.
Kadhalika, amesema kama kweli Profesa Lipumba anadhani yeye ni mwenyekiti halali, afike makao makuu ya CUF kisiwani Unguja ili kufanya kazi badala ya kukubali aendelee kutumika.
Hivi karibuni Profesa Lipumba alitangaza kumfukuza kazi, Maalim Seif na kumteua Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Tanzania bara, Magdalena Sakaya, kuwa kaimu Katibu Mkuu.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa chama hicho katika kisiwa kidogo cha Tumbatu Mvuvini, Maalim Seif alisema anamshangaa Profesa Lipumba kwa madai kwamba yeye ameshindwa kazi kwa kuwa haendi kazini katika ofisi za chama zilikozo Buguruni, Dar es Salaam.
“Eti nimeshindwa kazi akidai kuwa siendi ofisi kuu ya CUF Buguruni. Mbona yeye haji makao makuu ya CUF Mtendeni. Lipumba hana mamlaka ya kuniondoa nafasi yangu ya ukatibu mkuu,” alisema.
Alisema tangu Agosti, 2015, Lipumba hajawahi kukanyaga makao makuu ya CUF Mtendeni na kwamba hata kama angekuwa Mwenyekiti halali wa chama, alipaswa kumwita na kumhoji kwa nini haendi ofisi kuu za chama Buguruni kuliko kuchukua madaraka ya kutangaza kuwa amemtimua.
Maalim Seif pia alikemea siasa za chuki na uhasama zilizotawala kisiwani humo kati ya CCM na CUF na kusema zimesababisha mapigano na hujuma ikiwamo kuchomeana nyumba kutokana na itikadi za vyama.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui, alisema Profesa Lipumba ametumika na amefanya kazi kubwa ya kukihujumu chama huku akiungwa mkono na baadhi ya wanachama.
Mazrui pia alimwomba Rais John Magufuli kumtimua Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, kwa madai kuwa ni miongoni mwa watendaji wabovu wa serikali.
Alisema utendaji mbovu wa Jaji Mutungi umesababisha mtafaruku mkubwa na mgogoro unaoendelea ndani ya CUF.
“Rais Magufuli anatumbua watendaji ambao si waadilifu, lakini Msajili amemwacha kwani anapaswa kutumbuliwa kwa sababu ameivuruga nchi,” alisema.
Alisema Msajili huyo amempa uhalali Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wa CUF, wakati alijiuzulu kabla ya uchaguzi mkuu na sasa amekuwa akikihujumu chama.

from Blogger http://ift.tt/2n0Zhms
via IFTTT


Kategori

Kategori