Showing posts with label Vituko Duniani. Show all posts
Showing posts with label Vituko Duniani. Show all posts

Video: Wema Sepetu, Jackline Wolper, Bosi wa GSM ndani ya China kunani?

Kwenye Instagram zao mastaa hao wamepost waki safiri toka dar siku moja na wote wamepost picha wakiwa dubai same day then wote wamepost wakiwa china same place Canton Kama Picha zinavyoonesha Location ila hawajapiga picha pamoja.. Ambapo mdogo wa GSM counselor Salaah amepost akiwa Canton fair na wema na wolper wakipost wakiwa canton railway station same area ila wamekuwa makini kutopiga picha pamoja au labda hawafahamiani. Au labda ma baby wao idriss na harmonize ndo wamegharamia safari yao ya china.. Au labda yule MCM aliyempost kawasponso

Tazana Video Hapa chini






Video: Mrembo Atinga Global Afichua Siri Za ‘Scorpion’


Mrembo aitwaye Talta Msofe (21) akiwa katika pozi baada ya kutinga katika ofisi za Global Publishers kufichua siri za mtuhumiwa huyo, Salum Njwete ‘Scorpion’, mkazi wa Yombo Machimbo jijini Dar es Salaam.

Tazama hapa video Akifunguka 





Nyoka 'watoroka' katika shamba China

Nyoka 'watoroka' katika shamba China



cobra

Maafisa mashariki mwa China wanawasaka zaidi ya nyoka 50 aina ya swila (cobra kwa Kiingereza) waliotoweka kutoka shamba la nyoka linaloendeshwa bila ya kibali .
Zaidi ya nyoka 200 walitoweka kutoka shamba hilo mnamo Agosti mwaka huu. Wafugaji nyoka katika shamba hilo wameambia polisi kwamba walikuwa wanajaribu kuwasaka nyoka hao waliotoroka pasi kuwaarifa maafisa wa eneo hilo.
Tatizo hilo lilidhirika kwa umma baada ya swila mmoja kuonekana na kuwashutusha wakaazi katika shamba jingine kwenye eneo la karibu.
Serikali ya eneo hilo inajaribu kuwahakikishia wakaazi kuwa wana dawa za kutosha za kukata sumu ya nyoka hao iwapo wakaazi wataumwa kabla ya nyoka wote kupatikana.

Nyoka atafuta 'joto' kwenye kiatu huko Australia

Image copyright

Nyoka mwenye sumu kali atafuta 'joto' kwenye kiastu Australia 
Mwanamke wa Australia amewaita maafisa wa wanyama pori kumtoa nyoka wa urefu wa mita 1 mwenye sumu kali kutoka kwenye kiatu chake.
Mnasa nyoka Rolly Burrell alimdhibiti nyoka huyo wa rangi ya chokoleti aliyekuwa anatafuta ''joto'' nyumbani mwa mwanamke huyo Adelaide, kusini mwa Australia.
Alikuwa ametoka nje ya nyumba yake iliopo mashambani kukusanya viatu vyake na hapo akaona mkia ukipotea ndani ya kiatu chake kimoja.
Nyoka huyo ni mmoja wa wanaoonekana kuwa wenye sumu kali duniani na hupatikana katika pwani na maeneo ya ndani ya ardhi kavu Australia.
"Alitoka nje kuchukua viatu vyake na akaona kitu kikitoweka kwa kasi," Burrell ameiambia BBC.
"Aligundua kuwa ni nyoka."
Nyoka huyo ambaye ni aina inayopenda kujificha, alichiliwa msituni kando na mbali na maenoe ya makaazi ya watu .
Bwana Burrell amesema kampuni yake iliitwa kwa mara nyengine kutoa nyoka kwenye kiatu takribana mwaka mmoja uliopita.
Viatu hivyo aina ya buti, vimetengenezwa kwa ngozi ya kondoo, na hutumika sana Australia, Huwana joto zuri wakati wa msimu wa baridi, pengine ndio sababu iliomvutia nyoka huyo.
"Ndio wanaanza kuamka kutoka usingizini," Bwana Burrell anasema.
"Msimu wao wa kujamiiana umeanza kwa hivyo wanatafuta joto na wana njaa."

THIS WOMEN SHE WILL NEVER FORGET WHEN SHE WEAR SHORT DRESS (Mwanamke huyu hata sahau)






KITUKO CHA MWAKA ONA VIDIO HAPA






 tripleclicks.com
tem Type Wristwatches Case Material Stainless Steel Dial Window Material Type Glass Dial Material Type Stainless Steel Water Resistance Depth 5 m Movement digital led watches Band With 20mm to 29mm Dial Diameter 4.1 cm Band Width 18mm Clasp Type normal Boxes & Cases Material OPP BAG, smae as My picture, well protect...


tem Type Wristwatches Case Material Stainless Steel Dial Window Material Type Glass Dial Material Type Stainless Steel Water Resistance Depth 5 m Movement digital led watches Band With 20mm to 29mm Dial Diameter 4.1 cm Band Width 18mm Clasp Type normal Boxes & Cases Material OPP BAG, smae as My picture, well protect Gender Men Style Fashion & Casual Condition New without tags Dial Display Digital Feature None Case Shape Animal Shape Band Material Type Silicone Band Length 24.5 cm
7.2 USD LimitedAvailability
IMPRISIONMENT FOR RETALITORY PIG HEAD TOSS INTO MOSQUE

IMPRISIONMENT FOR RETALITORY PIG HEAD TOSS INTO MOSQUE


The state of the world has truly become a confusing one. Being born white is considered racist, being conservative is considered intolerant, being a Christian is considered violent and being a Muslim is considered peaceful.
Meanwhile, the list of things that people find offensive has grown by thousands of pages since 2013, when four Englishmen tossed a severed pig’s head at a Mosque in retaliation for the brutal street butchering of Lee Rigby, a British soldier, who was run down by a car and then decapitated by two Muslims in the middle of the day.

Of course, the judge wouldn’t side with them one iota come the day of their sentencing. Instead he gave the four individuals responsible for the pig head toss four to fourteen months in jail. While this is certainly appalling, it isn’t exactly an unexpected move from a British authority figure.

HUYU NDIYE MWANAUME ALIETUMIA $ 150,000 KUJIBADILI SURA AFANANE NA KIM KARDASHIAN

Jordan James Parke mwenye umri wa miaka 23 huenda ndie shabiki mkubwa zaidi duniani wa mwanamitindo ambae ni drama queen Kim Kardashian mke wa rapa Kanye West
Jordan alipohojiwa kwenye gazeti la The Sun alidai kuwa amezama kimapenzi kwa msanii huyo baada ya kutazama kipindi cha Tv cha Kim kinachokwenda kwa jina la Keeping Up With The Kardashians alinukuliwa akisema ‘I love everything about Kim,’ ‘She’s the most gorgeous woman ever.
 Her skin is perfect, her hair, everything about her.’ In a bid to resemble his idol, Jordan has undergone more than 50 cosmetic procedures including Botox, lip and cheek fillers, eyebrow tattoos and laser hair removal.
Tizama Picha Zaidi 



WEKA MAONI YAKO HAPA
SI NIMEOTA NIMEKATWA

SI NIMEOTA NIMEKATWA


Kitime-191x300Dah ndoto jamani ndoto kitu cha ajabu sana. Ndoto hizihizi watu wengine ndio huwa wanatumia kama dira ya maisha, wakiota ndoto tu basi mapema kesho yake wanakuwa na kazi ya kutafuta maana ya ndoto. Dunia nzima kumejaa wataalam mabingwa wa kutafsiri ndoto. Ukiota unapaa, mtaalamu mmoja atakwambia hiyo ni dalili kuwa matatizo yako yote yamekwisha, mwingine atakwambia kama umeota unapaa ujue basi unalogwa, mwingine atakwambia hiyo maana yake maadui zako hawakupati tena, basi kasheshe tupu.
Kuna maelezo mengine kuwa ndoto ni matokeo ya kumbukumbu mbalimbali za mambo yaliyotutokea au kusikia au kuyaona au hata kuyahisi, kwa hiyo ndoto hazina tafsiri ni ubongo tu unafanya kazi ukiwa umelala. Lakini jamani hii ndoto niliyopata wiki hii lazima ina maana yake. Baada ya kutoka katika mihangaiko yangu nikaingia kitandani kulala, katikati ya usingizi si nikaanza kuota, nikajikuta nashuka kwenye gari la bei mbaya lenye full kiyoyozi. Moja kwa moja nikaingia katika ukumbi uliojaa watu ambao nikawa najua ni Halmashauri Kuu ya Kamati Kuu ya chama changu cha siasa. Na mkutano ule ulikuwa wa kumpitisha mtangaza nia ili awe mgombea urais, na mimi nilikuwa mmoja wa watangaza nia. Ile kuingia tu watu wote wakasimama na kuanza kunishangilia kwa nguvu na kunipigia makofi. Nikawapungia mikono tena hapo nikaanza kutembea slow moshen kama kwenye kwenye sinema, nikiwapungia mkono wajumbe wa mkutano huo. Baada ya kukaribishwa kwenye kiti changu na mabinti waliopendeza kwa yunifom za chama changu. Nikawekewa mbele yangu soda na mazagazaga mengine na kukaribishwa kuanza kula, ukumbi mzima walikuwa wakitaja jina langu na misifa kibao, mkombozi, shujaa, kiboko yao, Mzee Chekanakitime wa ukweli. Kiukweli ilikuwa wazi mimi ndie chaguo la watu, nakumbuka nikaanza kupanga watu wa kuwakaribisha siku ya kuapishwa, na pia nikaanza kupanga listi ya watu wa kuwashughulikia nikishaapishwa tu. Si unajua watu wengine vimeo. Niwe mkweli nilianza kupanga michepuko gani ntaanza nayo wiki ya kwanza ya utawala wangu.
Mwenyekiti wa chama changu akaniomba niongee na wajumbe ambao ni wazi walikuwa wamejawa na mapenzi makuu na imani juu ya uongozi wangu, niliwaahidi nitawakumbuka mara baada ya kuapishwa. Nilidhamiria nikipewa rungu tu, nabadili katiba ili wajumbe hawa wawe wa kudumu maana walionyesha uzalendo mkubwa kwangu na kwa chama chetu kitukufu. Kuna binti mmoja alikuwa na shepu nzuri sana na alikuwa anacheza na kuimba kwa furaha , huyu nilijiwekea nadhiri nitampa ukuu wa mkoa au Ubunge wa kuteuliwa, mpiga debe wangu msanii maarufu nitampa kawilaya. Kuna kagazeti fulani kanajifanya kananifuatilia sana maisha yangu, wiki ya kwanza tu nakafungia, na kale kachoraji kavikatuni kwenye gazeti lile ntakatia ndani kakajifunze kazi ya uashi kule gerezani.
Nilikatishwa mawazo kwa kushtuliwa na kuambia kuwa ni muda wa wajumbe kupitisha majina ya wagombea rasmi, hivyo mimi na watangaza nia wengine wengine tutoke nje na kusubiri matokeo. Wakati tunatoka nikawa nasikia wajumbe wakipiga makofi na kulitaja jina langu, niliwaonea huruma watangaza nia wenzangu maana nilijua wananisindikiza tu. Muda si mrefu tukaitwa ndani nikawa tayari kusherehekea kwa nguvu, Mwenyekiti wetu kaongea machache akaanza kutaja waliokatwa si akanitaja na mimi, nikashtuka mpaka usingizi ukapea, nikajikuta niko ghetto kwangu. Ndoto hii maana yake nini wataalamu?
MJUE JOHN KITIME

MJUE JOHN KITIME

Kitime-191x300 

NAME: John Kitime  
Aka: Anko
HOBBIES: Kung’oa meno simba walio hai bila ganzi wala nini kwa kutumia koleo. pia napenda mchezo wa kukwepa risasi, au kuzidaka kwa meno.  
GREAT ACHIEVEMENT: Nilikuwa mtu wa kwanza kutua kwenye jua, japo nifanya hayo usiku wakati kidogo joto limepungua. Pia naweza kuzungumza lugha mbalimbali10,956.  
JAMBO KUBWA LA KIJINGA NILILOWAHI KUFANYA: Kuogelea kwenye volkeno nilibabuka sana.
EMBARRASSING MOMENT: Nilishindwa kusukuma treni ili washtue iwake.
JAMBO LA KUJISIFU: Nyoka mwenye sumu kali aliniuma akafa yeye. SIFA ZANGU BINAFSI: SPENDI KUJISIFU
Kujua mambo yangu zaidi kila mara soma www.johnkitime.co.tz
Kila mmoja hutamani harusi yake iwe ya kitofautiโ€ฆlakini huyu alitamani yake iwe hivi!!

Kila mmoja hutamani harusi yake iwe ya kitofauti…lakini huyu alitamani yake iwe hivi!!


Maharusi wengi hutamani siku ya harusi kuwa siku ya kitofauti zaidi katika maisha yao wakiamini ndio siku pekee ambayo ni ya furaha zaidi huku wengine wakitumia kila aina ya njia kuhakikisha sherehe yao inapendeza.
bride
Utakuta wengine wanatumia usafiri wa farasi au magari ya kifahari kuhakikisha tu sherehe inakuwa ya kipekee zaidi kwao lakini kwa Jenny Buckleff ilikua tofauti kwani yeye alitumia jeneza kama usafiri wake.
aruc2
Jenny alitaka kuwashangaza wageni waliofika kwenye sherehe yake hata kwa mumewe pia kwani hakumwambia mtu yoyote kuhusu uamuzi wake huo.
nne
Siku ya sherehe aliingia ukumbini akiwa ndani ya jeneza lililokuwa likisikumwa kwa pikipiki huku kila mmoja akishikwa na butwaa kutokana na kitendo hicho ambacho si rahisi kutokea.
akitoka
By millwrdwyo.com
TUMBILI AZALIWA NA KUPEWA JINA LA MTOTO WA MFALME,

TUMBILI AZALIWA NA KUPEWA JINA LA MTOTO WA MFALME,


Tumbili mwenye jina sawa na binti mfalme
Hifadhi moja ya wanyama huko Japan imelazimika kuomba radhi baada ya wahudumu wake kumpa tumbili mtoto wa  kike, jina sawa na lile la mwanawe mwanamfalme wa Uingereza Charlotte.

Kituo hicho cha wanyama cha Takasakiyama kilicho kusini mwa taifa hilo kilikabiliwa na gadhabu kuu ya watu baada ya kumpa tumbili huyo wa kike jina hilo sawa na binti mfalme wa Uingereza.

Chombo cha habari cha Kyodo kiliripoti tukio hilo kikidai kuwa raia waliihusika katika kuchagua jina la tumbili huyo wa kike.

''ni kawaida kwa tumbili wa kwanza kila mwaka kupewa jina na umma'' Kyodo
Jina hilo la Charlotte ndilo lililotokea kupendwa na watu wengi huku watu 59 kati ya raia 853 wakiipigia kura.

Baadhi ya raia walipinga pendekezo hilo wakisema haifai kuipa tumbili huyo jina sawa na binti mfalme.

Wengine walisema kuwa haitakuwa vyema kwao wenyewe iwapo waingereza wataita tumbili wao majina sawa na ya wafalme wao.

Kituo hicho cha Wanyama kilichapisha taarifa kwenye mtandao wao wakiomba msamaha huku wakipanga mikakati ya kubadilisha jina la tumbili huyo
BI HARUSI ATOROKA SIKU MOJA BAADA YA NDOA, AANIKA MAZITO YALIYOMFANYA AMKIMBIE MUMEWE

BI HARUSI ATOROKA SIKU MOJA BAADA YA NDOA, AANIKA MAZITO YALIYOMFANYA AMKIMBIE MUMEWE

AIBU ya mwaka! Mwanadada aliyefahamika kwa jina la Tatu Ally (26), mkazi wa Kongowe, Mbagala, Dar amejikuta akiifedhehesha familia yake kufuatia kutoroka kwa mumewe siku moja tu baada ta kufunga ndoa, Amani lina picha kamili.

Mwanadada Tatu Ally anayedaiwa kutoroka baada ya kufunga ndoa.

Kwa mujibu wa chanzo, ndoa hiyo ilifungwa Aprili 4, mwaka huu Mbagala jijini Dar kisha bi harusi huyo kwenda kwa mumewe aliyetajwa kwa jina moja la Ramadhani kule Mbezi ya Kimara, Dar ambapo Aprili 5 aliingia mitini.
Chanzo kikadai kwamba, bibi harusi huyo aliamua kuchukua uamuzi huo kwa sababu alikuwa na mwanaume mwingine ambaye angefunga naye ndoa.

Chanzo cha kuaminika kinaeleza kwa kina kuwa mwanadada huyo alishaolewa na mwanaume mwingine akatoroka na amekuwa na tabia za ajabuajabu kiasi kwamba watu wanamchukulia kama anafanya biashara ya kujiuza.

KISIKIE CHANZO
“Kusema kweli alichofanya dada Tatu ni kibaya sana, siwezi kusema sana lakini tukio hilo limemuuma kila mtu hapa mtaani.“Baada ya tukio la kutoroka, sasa mumewe anataka arudishiwe mahari yake (haikutajwa ni kiasi gani) sambamba na gharama zote zilizotumika siku hiyo ikiwemo usafiri na chakula kitu ambacho hakiwezekani.

“Familia imekaa kikao na kujadili juu ya tukio hilo lakini Tatu mwenyewe yupo mitaa ya Toangoma njia ya kwenda Kigamboni (Dar), tunasikia anataka kuolewa tena Jumanne (juzi),” kilisema chanzo.

Bwana Ramadhani anayedaiwa kutorokwa na mkewe baada ya ndoa.

BABA MZAZI ATOA NENO ZITO 
Naye baba mzazi wa Tatu, mzee Ally alipotafutwa na Gazeti la Amani juzi ili azungumzie tukio hilo la binti yake kutoroka kwa mume siku moja baada ya ndoa, alikuja juu na kusema kuwa hataki kumuona (Tatu) wala kumsikia kwa lolote kutokana na aibu waliyoipata kama familia.

“Sitaki hata kumsikia masikioni mwangu na kwanza si mwanangu tena nimemtoa hata kwenye orodha ya watoto wangu. Yeye hakulazimishwa kuolewa alitaka mwenyewe na nikamuuliza kama anataka sherehe akakataa na kudai kuwa anataka dua tu na ndiyo tukafanya hivyo kama alivyotaka lakini yeye ametupa aibu kubwa sana hapa mtaani.

“Mtoto hatulii sijui amekuwaje jamani? Sasa nasema hivi kwa aibu aliyonipa sitaki kumuona tena na kama anaolewa basi ajiozeshe mwenyewe huko aliko mimi nimechoka kabisa siwezi na ulimi wangu hauwezi kuziba pua yangu.

“Hatujui aliko mpaka leo hii na hapatikani kabisa hata kwenye simu yake ya mkononi tunasikia ana namba za simu nyingi ila tumeshakwenda kutoa taarifa polisi kwa upande wetu sisi wanafamilia na kwa upande wa mume wake naye nilimshauri akatoe taarifa polisi huko kwao Mbezi,” alisema kwa jazba baba wa Tatu.

MUME HATAKI MASWALI
Akizungumza kwa njia ya simu na Amani huku sauti yake ikiwekwa kwenye kifaa cha kumbukumbu, mwanaume aliyemuoa Tatu ambaye anadaiwa kutaka arejeshewe mahari yake alisema:
“Sihitaji kuulizwa kitu chochote, naomba mniachie mwenyewe nifuatilie suala hili mpaka mwisho.”

Ramadhani na mkewe siku ya ndoa yao.


BI HARUSI MWENYEWE SASA
Tatu alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi naye akarekodiwa, alijitetea na kudai kuwa yupo mkoani Morogoro na aliamua kuondoka kwa mume wake kwa sababu ya matatizo aliyokutana nayo huko na kukanusha taarifa za kutaka kuolewa upya.

“Niko Morogoro sasa hivi, sijatoroka niliamua kuondoka kwa yule bwana aliyenioa kwa sababu kuna matatizo yalinikuta ndiyo nikaona niondoke na aliyewaambia kuwa nataka kuolewa tena ni muongo, mimi siwezi kujiozesha mwenyewe.

“Kwanza (wazazi) wamekwambia wamenipa shilingi ngapi? Wao wanataka watajirike kupitia mimi, yaani katika mahari yote eti mimi wanipe shilingi laki mbili tu na wao wachukue laki sita wapi na wapi!” alisema Tatu.
Kwa madai hayo ya Tatu, mahari ya kuolewa kwake ilikuwa shilingi laki nane (800,000).

Hata hivyo, Jumanne iliyopita gazeti hili lilifuatilia kwa karibu ili kujua kama Tatu atafunga ndoa tena au la! Mpaka gazeti linakwenda mitamboni, chanzo kilisema Tatu alionekana mitaa ya Kigamboni mchana wa siku hiyo akifanya ‘window shopping’

Kategori

Kategori