Showing posts with label July 19. Show all posts
Showing posts with label July 19. Show all posts
WAZIRI WA MKAPA NA JK ATIWA MBARONI NA POLISI KWA AMRI YA MKUU WA WILAYA

WAZIRI WA MKAPA NA JK ATIWA MBARONI NA POLISI KWA AMRI YA MKUU WA WILAYA

Waziri wa zamani wa Serikali ya awamu ya tatu na nne, Dkt. Mary Nagu amekamatwa na Jeshi la Polisi Wilaya ya Hanang’ mkoani Manyara kwa amri ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Sara Msafiri. Mbali na Nagu, wengine waliokamatwa ni Katibu wa CCM Wilaya hiyo, Othman Dunga na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, George Bajuta.
Viongozi hao walikamatwa jana wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Siasa baada ya kudaiwa kuibuka vurugu kwenye kikao hicho kulikosababishwa na agenda ya uchaguzi iliyowasilishwa kwenye kikao hicho ambayo baadhi ya wajumbe hawakukubaliana nayo. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na DC Sara Msafiri ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo.
Baada ya kuibuka kwa vurugu hizo, Mkuu wa Wilaya aliamuru Dkt. Mary Nagu na viongozi hao wa CCM wakamatwe na kupelekwa Kituo cha Polisi Katesh kwa ajili ya kutoa maelezo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis Massawe alithibitisha kukamatwa kwa viongozi hao waliokuwa kwenye kikao cha ndani cha CCM Wilaya wakijadili masuala yao na kusababisha kuibuka vurugu zilizohatarisha usalama.
“Mkuu wa Wilaya alielekeza waende Kituo cha Polisi kutoa maelezo yao, sasa sisi tunawahoji kujua tatizo ni nini, walikuwa wanajadili nini na nani alisababisha vurugu? Kwa vile kikao hicho kilikuwa na Mwenyekiti wake, atatuambia nani walioanzisha vurugu ndani ya kikao,” alisema.
HT @ MTANZANIA

from Blogger http://ift.tt/2tpo0UX
via IFTTT


STARS KWENDA KIGALI MCHANA HUU KUZICHAPA NA RWANDA JUMAMOSI

STARS KWENDA KIGALI MCHANA HUU KUZICHAPA NA RWANDA JUMAMOSI

Kikosi cha timu ya Taifa ya mpira wa miguu Tanzania (Taifa Stars), kinakwea pipa leo mchana kwenda jijini Kigali, Rwanda kutafuta nafasi ya kushiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN)
Taifa Stars inaenda Kigali ikitokea jijini Mwanza ilipoweka kambi kabla ya kucheza mchezo wa kwanza dhidi ya Rwanda Jumamosi iliyopita, itapitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere kwenda Rwanda.
Stars itaondoka Mwanza saa nne asubuhi na kuwasili Dar es Salaam majira ya saa sita mchana kabla ya kuunganisha ndege ya Rwanda majira ya saa nane alasiri kwenda Kigali.
Inakwenda Kigali kwa ajili ya mchezo wa marudiano na Rwanda maarufu kama Amavubi kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika nchini Kenya mwakani.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Mshindi wa jumla katika michezo miwili atakuwa amesonga mbele hivyo kukutana na Uganda mwezi ujao.
Katika mchezo huo, Stars itacheza bila beki Shomari Kapombe aliyeumia mguu katika mchezo kwanza uliopigwa jijini Mwanza.

from Blogger http://ift.tt/2tp8uZ4
via IFTTT


HAJI MANARA NA WENZAKE WASAMEHEWA ADHABU NA TFF

HAJI MANARA NA WENZAKE WASAMEHEWA ADHABU NA TFF

Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imefuta adhabu dhidi ya wanafamilia wanne waliofungiwa kushiriki masuala la soka kwa mwaka mmoja.
Wanafamilia hao ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Rukwa, James Mwakwinya; Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Rukwa (RUREFA), Blassy Kiondo; Kaimu Katibu wake, Ayoub Nyaulingo pamoja na Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara.
Haji Manara alitiwa hatiani Aprili 23, mwaka huu kwa makosa ya lugha chafu na za chuki kwa viongozi wa TFF na kupotosha umma dhidi ya kadi njano ya mchezaji Mohammed Fakhi wa Kagera Sugar ambako alifungiwa kushiriki masuala ya mpira kwa mwaka mmoja na faini ya Sh milioni tisa.
Viongozi wa RUREFA walifungiwa kwa mwaka mmoja na faini ya Sh. milioni mbili kwa kila mmoja kwa makosa ya kukiuka maagizo ya viongozi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliyotaka wasitishe mchakato wa uchaguzi mkoa kwa kuwa kulikuwa na rufaa iliyokatwa TFF.
Akizungumza na Wanahabari leo Julai 17, 2017 Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, Tarimba Abbas, alisema viongozi hao wamesamehewa adhabu zao kwa kuwa waliomba kupitiwa upya kwa mashauri yao na kamati imeona ni bora kuwaachia huru ili kuendeleza masuala ya soka.
“Wapo wengi waliofungiwa wengine maisha na wengine adhabu fupi, msamaha huu ni kwa wale ambao wameomba tu kupitiwa upya kwa adhabu zao, pia milango ipo wazi kwa wengine ambao wanataka kupitiwa kwa mashauri yao, lakini si kwa wale waliopanga matokeo uwanjani,” alisema Tarimba.
Kadhalika, Tarimba aliwaomba viongozi wa TFF kuandaa semina ya Maofisa Habari na Viongozi wa Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ili kuepuka maneno machafu ambayo yanasababisha wao kufungiwa.
“Inaonekana viongozi na Maofisa Habari hawana maneno mazuri ya kuongea na wadau wa soka na ndio maana matatizo ya kufungiwa yanajitokeza mara kwa mara, naamini wakipata semina hiyo itawasaidia kujirekebisha na kupunguza kesi kama hizo,” alisema Tarimba.
Kwa niaba ya TFF, Ofisa Habari wa Shirikisho, Alfred Lucas, wameyapokea mapendekezo hayo kutoka kwa Tarimba na kwamba tutafanyia kazi ili kurekebisha makosa hayo kwa manufaa ya soka la Tanzania.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

from Blogger http://ift.tt/2vBuXyB
via IFTTT


YULE MUUGUZI ALIYEMCHOMA MSICHANA SINDANO YA USINGIZI NA KUMBAKA ALALA LUMANDE

YULE MUUGUZI ALIYEMCHOMA MSICHANA SINDANO YA USINGIZI NA KUMBAKA ALALA LUMANDE

Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora linamshikilia muuguzi wa kituo cha afya cha Kata ya Igulubi, Damian Mgaya (26) kwa tuhuma za kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 18 baada ya kumchoma sindano ya usingizi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa alisema muuguzi huyo ameshahojiwa na atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika. Alisema msichana huyo amepatiwa fomu ya PF3 baada ya tukio hilo na jana aliruhusiwa kutoka hospitali baada ya hali yake kuendelea vizuri.
“Hali ya huyu msichana imeimarika na ameruhusiwa, naye atahojiwa kwa upande wake ili tujue uhalisia wa tukio lilivyokuwa,” alisema Kamanda Mutafungwa.
Kamanda huyo alisema siku ya tukio msichana huyo alifika kwenye Zahanati hiyo kumuuguza mama yake mzazi ndipo muuguzi huyo alipotumia nafasi hiyo kumchoma sindano ya usingizi kisha kumbaka.
Ntemi James, ambaye ni Mtendaji wa Kata ya Igulubi amesema tukio hilo lilitokea Ijumaa iliyopita kuanzia saa 8 usiku hadi alfajiri wakati msichana huyo akimuuguza mama yake aliyelazwa katika Zahanati hiyo.

from Blogger http://ift.tt/2u9Gyas
via IFTTT


JAJI ALIYEMUOMBA RAIS MAGUFULI KUJIUZULU AIAGA DUNIA

JAJI ALIYEMUOMBA RAIS MAGUFULI KUJIUZULU AIAGA DUNIA

Aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Upendo Msuya amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam alipokuwa anapatiwa matibabu.
Jaji Msuya amefariki dunia ikiwa ni miezi miwili tu tangu alipojiuzulu wadhifa huo ambapo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 16 Mei, 2017 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi inaeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli ameridhia maombi ya kuacha kazi kwa kiongozi huyo kuanzia tarehe 15 Mei, 2017.
Taarifa iliyothibitishwa na mtoto wa marehemu, Kelvin Msuya imeeleza kuwa msiba wa mama yake utakuwa Tegeta, jijini Dar es Salaam.

from Blogger http://ift.tt/2tFJNTn
via IFTTT


Mghwira: Lowassa Kuhamia Chadema Ufisadi wa Kisiasa

Mghwira: Lowassa Kuhamia Chadema Ufisadi wa Kisiasa

Moto wa Uchaguzi Mkuu wa 2015 ulishazimika lakini kuna kila dalili kwamba majivu yake bado hayajapoa na moja ya dalili za kuwapo kwa hali ya uvuguvugu ni kauli ya hivi karibuni ya Anna Mghwira dhidi ya Edward Lowassa kwamba njia aliyotumia kugombea urais ilikuwa ni aina nyingine ya ufisadi.
Katika uchaguzi huo, Mghwira ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, alikuwa mwanamke pekee aliyegombea urais na kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alishika nafasi ya tatu nyuma ya Lowassa akipata kura 98,763 sawa na asilimia 0.65 ya kura zote.
Lowassa, aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika Serikali ya Awamu ya Nne, katika uchaguzi huo aliwania kiti hicho kupitia Chadema akiungwa mkono na vyama vilivyoungana chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa)na alipata kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote. Dk John Magufuli aliibuka mshindi kwa kupata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46.
Juni 3, Mghwira aliteuliwa na Rais Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro wakati huo akiwa mwenyekiti wa ACT –Wazalendo na muda mfupi baadaye chama hicho kikamuondoa katika nafasi hiyo kutokana na uteuzi huo.
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili wiki hii, Mghwira alisema njia aliyoitumia Lowassa kugombea urais ilikuwa ni aina nyingine ya ufisadi wa kisiasa kwa kuwa hakupitishwa na chombo chochote ndani ya chama chake.
Alidai kuwa hata katika kampeni, Ukawa haukuzungumzia ajenda ya ufisadi baada ya waziri mkuu huyo wa zamani kujiunga Chadema.
“Kwenye kampeni 2015 chama kikuu cha upinzani (Chadema) hakikuwa kinazungumzia tena ufisadi labda kwa hofu kwamba mshutumiwa mmojawapo wa ufisadi ndio alikuwa mgombea wao. Kwa bahati mbaya ni wao walioibua tuhuma hizo za ufisadi. Lakini kuondoka Dk Slaa (Wilbroad aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema) nako kulileta tatizo ambalo watu hawakutaka kulifuatilia.
“Ni tatizo watu walitakiwa kuuliza alikuwa (Dk Slaa) na sababu ya msingi ya kuondoka? Ameondoka kwa nini? Anaenda wapi na anaenda kufanya nini. Ilikuwa ni ajabu kwamba kiongozi ambaye unataka uje kuwa mfano wa demokrasia, unaingia kugombea nafasi kubwa kama hiyo ya urais bila kuchaguliwa na chombo chochote cha chama,” alisema.
Mghwira aliendelea kujiuliza maswali kuhusu hatua hiyo ya Lowassa, “Umeingiaje? Inatokeaje?” Kisha alihitimisha, “Hiyo ni aina nyingine tena ya ufisadi wa kisiasa. Lowassa kama anataka kujisafisha vizuri kisiasa aangalie sana angeweza kufika mbali kama angetumia njia sahihi.”
Mghwira ambaye ni kiongozi wa kwanza wa upinzani kushika wadhifa wa ukuu wa mkoa tangu kurejea kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992, alisema, “Njia iliyotumiwa na Chadema si tu kwamba inarudisha nyuma siasa zetu lakini haikutoa picha nzuri ya uwepo wa demokrasia ndani ya upinzani. Hili lilikuwa doa kubwa kwa Mzee Lowassa.”
Uteuzi wa Lowassa kugombea urais kupitia Ukawa ulishuhudia Dk Slaa aliyetajwa sana wakati huo kuwa mgombea wa nafasi hiyo , akijiuzulu siasa na kwenda kuishi nje ya nchi.
Mbali na Dk Slaa, aliyekuwa mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba naye aliamua kuikimbia CUF aliyokuwa mwenyekiti wake kabla ya kurejea baadaye na kutambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa jambo lililozua mgogoro mkubwa ndani ya chama hicho hadi sasa.
Alikerwa kuvuliwa uenyekiti
Katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Shanty Town mjini Moshi, Mghwira alikumbuka karaha aliyoipata baada ya furaha ya kuaminiwa na Rais na kupewa wadhifa huo.
Alisema kama si ubabaishaji wa kisiasa Tanzania, asingeondolewa kwenye uenyekiti wa ACT-Wazalendo.
“Changamoto niliyokutana nayo ACT-Wazalendo kama mwenyekiti ni kukosa wigo sahihi wa kisiasa kwa sababu kama tungekuwa tunafanya siasa sahihi, nisingeondolewa uenyekiti,” alisema.
Mghwira alisema, “Naapishwa tu kuwa RC (mkuu wa mkoa) kesho yake naondolewa tena tukiwa tumepanga kukutana kwenye kikao na mpaka leo hatujawahi kukutana.
“Nimesoma kwenye magazeti kuwa mrithi wa Mghwira kutembelea mikoa saba, yaani na mrithi ameshapatikana. Hizo si siasa, huo ni ubabaishaji. Ubabaishaji wa kisiasa Tanzania ni tatizo,” alisema.
Aliongeza, “Sisi kina mama tukisimama imara tunaweza kuondoa dhana hii ya siasa za ubabaishaji. Ni siasa za kipuuzi kabisa. Mmekubaliana mkutane muongee, hamuongei wenzako wanakaa pembeni. Umechaguliwa na mkutano mkuu unaondolewa na kamati ndogo. Watu 370 karibu 400 hivi walikuchagua, siku ya kuondolewa unaondolewa na watu watatu au wawili au mmoja. Hiyo si siasa ni dalili tosha kuwa hakuna siasa.”
Alisema mbaya zaidi ni kuwa watu wanaokuondoa hawakutumwa na mkutano mkuu, wala hawakukaimishwa na kamati kuu.
Hakuna upinzani nchini
Baada ya kujumuisha yote hayo na hasa alivyotimuliwa kwenye uongozi, mkuu huyo wa mkoa akawa na jibu moja kuhusu siasa za upinzani, “Hakuna siasa za upinzani, bali zilizopo ni za kurudishana nyuma maendeleo.
“Siasa ni kitu kizuri kwa maana ya ile mijadala, kubadilishana mawazo na kuzungumzia masuala ya itikadi, mipango ya kijamii… hakuna hiki kitu Tanzania.”
Badala yake alisema, “Tumeweka siasa kama ni uhasama kati ya chama tawala kilichoshinda kihalali na vyama hivi vingine. Kila siku watu wanatafuta makosa ya wenzao (Serikali) hata kama inafanya vizuri. Hiyo sio siasa.
“Vyama vya upinzani hapa hatuendeshi siasa. Awali, chama chochote kitakachoibuka na siasa inayoeleweka kinaweza kutawala nchi hii kwa miaka 100 ilimradi tu kitoke na siasa inayoeleweka.”
Mghwira alisema, “Vikitokea vyama vitatu vinaendesha siasa inayoeleweka tunakuwa mahali pazuri zaidi. Kwa maana kwamba wale wakiongea jambo lao, hata kama hawatawali, mtawala asikie na kuthamini.
“Sisi hapa Tanzania kuna aina ya siasa za kudidimizana. Kwa sisi wanawake wanaharakati tunaziita PhD (pool her down). Unavutwa tu chini hutakiwi kukua. Nchi haiwezi kwenda kwa staili hii.”
Alisisitiza, “Kuna watu wanafikiri kwamba ili kitu kiwe sahihi ni lazima wao wakifanye (upinzani) lakini kikifanywa na watu wengine hakiko sahihi. Hiyo ni kutokuwa mwanasiasa. Kuwa mwanasiasa si kugombana ni kuwa na uwezo wa kujenga hoja, kuitetea na kuisimamia. Mwenzako akija na hoja kubwa zaidi kubali.”
Changamoto za ugombea urais
Mghwira alisema wakati akigombea urais alikumbana na changamoto mbili, moja ikiwa ni ya nchi na nyingine ni ya yeye kutojiandaa kugombea.
“Changamoto zangu binafsi sizijali sana kwa sababu sikuwa nimejiandaa kugombea urais. Ingawa sikushinda urais, lakini nilishinda hatua ya kushiriki kwenye kampeni. Nilishinda ndiyo maana hata Rais Magufuli ameona na akaniteua kuwa RC. Kushinda kwenye kampeni ni kushiriki na kutoka ukiwa umewaachia watu kitu.
“Nafikiri nimeacha hicho kitu. Kila mtu ana ushindi wa viwango vyake. Yeye (Rais Magufuli) alishinda ushindi halisi wa kura na nafasi lakini hajanyima nafasi, amegawa,” alisema na kuongeza kuwa kinachobaki ni kushirikiana ili kuijenga nchi.
“Kuna watu wanasema nilishindwa, sikushindwa kwa sababu sikuenda kushinda, bali nilienda kushiriki. Uchaguzi unashiriki kwanza, ukishashiriki wananchi ndio wanaamua nani ni mshindi.
“Kura zikishahesabiwa na akapatikana mshindi, mnarudi kuijenga nchi. Kuna wapinzani wa Magufuli ndani ya chama chake, nao wamo kwenye Serikali na tuko nao pamoja. Hao ni wabaya zaidi kuliko mimi kwa sababu mimi namkubali kwa asilimia 100 wao wanamkubali sehemu kwa sababu wanatoka chama kimoja. Wanajua mambo yao ndani ya chama yalikuwaje,” alisema.
Alisema wanaotoka upinzani wanaweza kuwa na ufanisi mzuri na uhusiano mzuri zaidi wa kikazi na Rais kwa sababu hawana masilahi ya kisiasa.
“Sina masilahi ya kisiasa CCM ila ACT-Wazalendo. Kama nina masilahi ya kisiasa kwenye chama changu hicho hakimdhuru yeye wala hakiharibu kazi yangu huku kwa sababu mimi na yeye tunahusiana kikazi tu,” alisisitiza.
ACT-Wazalendo ni CCM B?
Alipoulizwa kuhusu dhana iliyoanza kujengeka kuwa huenda ACT-Wazalendo ni tawi la CCM na ndiyo maana Rais ameteua wanachama wake wawili kushika nyadhifa kubwa serikalini alisema hilo si kweli.
Alisema katika kuunda Serikali ya mseto, ukitaka kwenda vizuri huchukui sana wale watu mnaopingana mno kwa kuwa mtapingana tu kila siku.
“Lazima uchukue watu ambao mnaendana katika utendaji kazi. Hata ACT-Wazalendo sidhani ana maanisha atachukua kila mtu…”
Mbali na Mghwira, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa mshauri wa chama hicho, Profesa Kitilla Mkumbo kuwa katibu mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Uteuzi ambao uliibua mijadala katika mitandao ya kijamii baadhi wakipongeza na wengine wakishutumu, huku baadhi ya wana-CCM wakinuna.

from Blogger http://ift.tt/2teOwfm
via IFTTT


Kategori

Kategori