JAJI ALIYEMUOMBA RAIS MAGUFULI KUJIUZULU AIAGA DUNIA

Aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Upendo Msuya amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam alipokuwa anapatiwa matibabu.
Jaji Msuya amefariki dunia ikiwa ni miezi miwili tu tangu alipojiuzulu wadhifa huo ambapo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 16 Mei, 2017 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi inaeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli ameridhia maombi ya kuacha kazi kwa kiongozi huyo kuanzia tarehe 15 Mei, 2017.
Taarifa iliyothibitishwa na mtoto wa marehemu, Kelvin Msuya imeeleza kuwa msiba wa mama yake utakuwa Tegeta, jijini Dar es Salaam.

from Blogger http://ift.tt/2tFJNTn
via IFTTT