Showing posts with label June 09. Show all posts
Showing posts with label June 09. Show all posts
PICHA: KOREA KASKAZINI YAANZISHA MAFUNZO YA KIJESHI KWA WATOTO WADOGO

PICHA: KOREA KASKAZINI YAANZISHA MAFUNZO YA KIJESHI KWA WATOTO WADOGO

Korea Kaskazini yaanzisha mafunzo ya Kijeshi kwa watoto nchini humo kuwaandaa na mapambano dhidi ya “ukoloni wa Marekani” na kumlinda Rais wao mpendwa, Kim Jong-un.
Mwalimu katika shule hiyo ya Kijeshi amesema, “Watoto wetu wanajua kuwa Rais Kim Sung wa pili na jenerali Kim Jong wa pili ni baba zao na katika shule hii wanajifunza kwa bidii kama wanavyotaka. Hiki ni Chuo cha hali ya juu kabisa kinachoandaa Jeshi la Korea.”
“Tunasoma kwa bidii kwa sababu tunajua hivyo ndio tutakavyoweka kulipa kisasi dhidi ya ukoloni wa Marekani. Ninasoma kwa bidii nipate ufaulu wa juu kwenye masomo ya Kijeshi kama vile mbinu za kivita na kulenga shabaha,” ni kauli ya mmoja ya wanafunzi vijana katika chuo hicho.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rILwtD
via IFTTT


TUNDU LISSU: NITAKATAA NAFASI YOYOTE NITAKAYOTEULIWA NA RAIS MAGUFULI

TUNDU LISSU: NITAKATAA NAFASI YOYOTE NITAKAYOTEULIWA NA RAIS MAGUFULI

Swali: Tumeona kuwa sasa hivi Rais anachukua watu kutoka upinzani na kuwapa nafasi katika serikali yake, unalichukuliaje hili?
Lissu: Hao sio wapinzani na hawajawahi kuwa wapinzani, walianzishwa kwa ajili ya kuua upinzani – imeshindikana na sasa wanazawadiwa. ACT na Anna Mghwira walikuwa wakabiliane na Lowassa, sio wakabiliane na CCM, walipata kura elfu tisini na ngapi sijui hawakufika hata kura laki moja. Sasa, huu ukuu wa mkoa ni zawadi tu. Ukatibu mkuu wa Kitila Mkumbo ni kuwazawadia watu wao. Serikali ya Chama Cha Mapinduzi haijawahi kuwa na shida na ACT, haijawahi kuwa na shida na Anna Mghwira, haijawahi kuwa na shida na Kitila Mkumbo na haijawahi kuwa na shida na ‘hao wote wanaojiita wapinzani.’ Shida yao kubwa ni CHADEMA, shida yao kubwa ni CUF. Hao ndio wapinzani, wengine wote hawa ni wana CCM. Wengine wamevaa gwanda hili, wengine wamevaa gwanda lile. Wote ni wana CCM kwa sababu wanafanya kazi za CCM.
Swali: Labda itokee Mh. Rais amekuteua kwenye nafasi yoyote ile ambayo ana mamlaka nayo, itakuwaje?
Lissu: Kwanza haitatokea, nikutoe wasiwasi. Pili, hata ikitokea Rais akafanya hivyo, nitamwambia mheshimiwa mimi napinga mfumo uliokuweka madarakani. Tunataka Katiba mpya, tunataka tutengeneze nchi upya. Kwahiyo kwanza hawezi na pili akinijaribu nitamwambia wazi kwamba kama unataka niitumikie nchi hii tubadilishe Katiba na tuiweke nchi sawa kwenye misingi sawa. Lakini mimi siwezi kutumikia utawala wa kidikteta kwa nafasi yoyote ile. Mimi ni mpinzani, na ndio maana nipo Mahakamani kila siku. Wanaopewa hizo nafasi sio wapinzani, ni watu wanaotumiwa kuua upinzani na hawataweza.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rU95Oq
via IFTTT


RAIS KIKWETE AELEZA CHANGAMOTO ANAZOKUMBANA NAZO KWENYE KULIMA MANANASI

RAIS KIKWETE AELEZA CHANGAMOTO ANAZOKUMBANA NAZO KWENYE KULIMA MANANASI

. Rais mstaafu, Jakaya Kiwete amezungumzia shughuli za kilimo anazozifanya huku akianika changamoto mbalimbali zinazomkabili.
Akizungumza leo Ijumaa muda mfupi mara baada ya Mwenge wa Uhuru kufika kwenye shamba lake la mananasi lenye ukubwa wa eka zaidi ya 200 mkoani hapa, amesema ingawa kilimo alianza tangu mwaka 1989, lakini suala la palizi na ukosefu wa maji ni moja ya changamoto anazokabiliana nazo.
“Nilianza kilimo miaka mingi sana na mpaka nastaafu nilikuwa naendelea na kilimo, lakini changamoto kubwa katika kilimo ni suala la palizi hususan haya mananasi unaweza palilia zaidi ya mara tatu,” amesema.
Amesema kuwa ingawa mananasi yanazaa vizuri kama yatapata huduma zote kikamilifu, lakini mkulima anaweza kupambana na ukosefu wa masoko pindi unapofikia msimu wa mavuno.
“Hata kama viwanda vitajengwa kwa wingi lakini ili mkulima apate faida ya juu ya kilimo hasa cha mananasi ni lazima kuwe na bei nzuri, lakini kama wanunuzi watakuwa wananunua bei isiyo na masilahi hakutakuwa na maendeleo kwa wakulima,”amesema.
Amesema kuwa mikakati aliyonayo kwa kushirikiana na taasisi na wakulima mbalimbali ni kutafuta mbegu za mananasi kutoka nje ya nchi na mkakati wa kuanzisha kilimo cha mananasi kwa njia ya umwagiliaji hali aliyosema itawainua wakulima wengi na kujikwamua katika janga la umaskini.
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa, Amour Hamad Amour amempongeza Kikwete kwa kuonyesha mfano bora hususan kuendeleza kilimo cha mananasi huku amiwahimiza Watanzania kuiga mfano huo.
Mwananchi

from Blogger http://ift.tt/2rIEp4i
via IFTTT


Exclusive. Hatimaye Nabii Frank Afichua Kiini cha Mauaji ya Kibiti na Rufiji..!!!

Exclusive. Hatimaye Nabii Frank Afichua Kiini cha Mauaji ya Kibiti na Rufiji..!!!

Akizungumza mapema asubuhi ya leo na Kituo cha Luninga cha Channel Ten na Magic fm Radio Nabii anayekuja kwa Kasi nchini Nabii Frank leo amefunguka na kueleza mambo makuu mawili ambayo ndiyo chanzo cha mauaji yanayoendelea Kibiti na Rufiji na amezitaka Mamlaka husika kuyafanyia Kazi ili kumaliza mauaji.
Amesema kwamba mauaji hayo yanatokana na sababu za Harakati za Kidini ( yaani kuna dini moja inataka kuwa ndiyo inayoaminika na kukubalika katika huo Ukanda hivyo wanaua Watu hasa wa dini fulani ili kuwatisha na wakimbie au wahame hayo maeneo na wabaki wao tu ) na sababu ya pili kasema kwamba Mfumo wa Kiuchumi wa Watu wa hayo maeneo umeharibiwa hivyo Wauwaji wameamua sasa kuwauwa wale wote ambao wanahisi ndiyo chanzo cha Mfumo wao huu kuharibiwa. Na inasemekana kwamba Mfumo mkubwa wa Kiuchumi au uingizaji Kipato kwa asiimia kubwa ya Watu wa hayo maeneo ni Mkaa na kama tunavyojua Serikali imepiga marufuku huku ikiweka Sheria kali dhidi ya wale watakaokamatwa.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sKFMh8
via IFTTT


Hivi ndivyo majibizano kati ya Costa na Conte yalipoanzia.

Hivi ndivyo majibizano kati ya Costa na Conte yalipoanzia.

Baada ya msimu kumalizika kocha wa Chelsea Antonio Conte aliamua kuongea na wachezaji wake kupitia ujumbe mfupi wa message ambapo aliwapongeza kuhusu msimu uliopita na kuwaambia matarajio yake juu yao kuhusu msimu ujao wa ligi kuu ya Epl.
Chanzo kimoja cha habari kimedai Antonio Conte hakumtumia Costa message mbaya lakini alimuambia maoni yake kama kocha lakini Mhispania huyo hakupendezwa na maoni ya Conte hivyo akamjibu Conte vibaya na ndipo Muitaliano huyo alipokasirika na kumuambia Costa kuwa hamtaki katika kikosi chake.
Costa kuona amejibiwa vibaya na Conte naye akaanza kumjibu vibaya hali iliyopelekea wawili hao kutumiana message mbovu na baadae Diego Costa alikasirika sana akaamua kutuma message hizo kwa wachezaji wote wa Chelsea aliokuwa na namba zao.
Tayari mgogoro huo umechukua sura mpya kwani mmiliki wa klabu ya Chelsea tajiri Roman Abromovich amechagua upande wake katika pande hizo mbili zinazovutana na Roman anaona hakuna mchezaji mkubwa kuliko kocha hivyo na yeye yuko upande wa kocha wao.
Chelsea wanapambana kutafuta mshambuliaji namba 9 ambaye anaweza kuziba nafasi ya Diego Costa na ugomvi kati ya Costa na Conte umezidi kuisukuma Chelsea kutafuta saini ya mchezaji wao wa zamani Romelu Lukaku ambaye thamani yake inatajwa kuwa euro 100m.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2smd2OF
via IFTTT


Hii ndio klabu inayoongoza kwa idadi kubwa ya makombe Ulaya.

Hii ndio klabu inayoongoza kwa idadi kubwa ya makombe Ulaya.

5.Juventus. Msimu huu walionekana bora sana na walitabiriwa na wengi kwamba huenda wangeweza kuchukua ubingwa wa Champions League lakini wakafungwa na Real Madrid. Juventus ndio klabu inayoongoza kwa mafanikio nchini Italia kwani wameshashinda Serie A mara 33 wakashinda Italian Cup mara 12 na Italia Super Cup mara 7,Champions League mara 2,Europa League mara 3 na kombe la washindi mara moja,Uefa super cup mara mbili,klabu bingwa dunia mara mbili na kuwafanya jumla kuwa na makombe 62.
4.Manchester United. Hii ndio klabu inayoongoza kwa mafanikio nchini Uingereza ikiwa imeshashinda vikombe 20 vya ligi kuu nchini Uingereza huku wakiwa wamebeba Fa mara mara 12, vikombe vya ligi mara 5 na mara 21 wakibeba ngao ya hisani,kombe la washindi mara moja,super cup mara 1,intercontinental cup mara 1,klabu bingwa dunia 1 na makombe makubwa ya Ulaya wameshashinda mara 4 huku mwaka huu wakibeba kombe la Europa ambalo walikuwa hawajalibeba kwa siku nyingi na jumla pamoja na makombe ya vilabu vya dunia na mabara United wameshinda vikombe 66.
3.Bayern Munich.Wana vikombe vya Bundesliga mara 27 huku wakiwa na vikombe vya ligi ya Ujerumani mara mara 6,German Cup mara 18, German Super Cup mara 5, nje ya Ujerumani klabu hii imeshashinda makombe ya Ulaya mara 5,Intercontinental cup mara 2 huku wakiwa wameshinda kombe klabu bingwa dunia mara moja, kiujumla klabu hiyo ya Ujerumani imechukua jumla ya makombe 67 hadi sasa.
2.Real Madrid. Wamefanikiwa kutetea kombe la Champions League na hiyo ikawapa kombe hilo kwa mara ya 12 ya makombe ya ya Uefa, Uefa super cup mara 3,klabu bingwa dunia mara 2, La Liga mara 33, Copa Del Rey mara 19, 9 Spanish super cup,intercontinental cup mara 3,Spanish League Cup 1 na Europa 2 hii ikiwapa jumla ya makombe 84.
1.Kama mpira ni makombe baasi Barcelona ndio klabu bora barani Ulaya kwa sasa kwani ndio klabu inayoongoza kuchukua makombe mengi ulimwenguni kuliko klabu nyingine yoyote, wameshashinda ubingwa wa La Liga mara 24,Spanish Cup 29,Spanish Super Cup mara 12,Spanish League Cup mara 2,klabu bingwa dunia mara 3, na mwaka 2009 walishinda makombe 6,makombe 5 ya Ulaya,kombe la washindi mara 4,Uefa super cup mara 5 lakini jumla Barcelona wana makombe 87.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sbf04x
via IFTTT


Baada ya kuhusishwa na Manchester City, Sanchez atoa neno.

Baada ya kuhusishwa na Manchester City, Sanchez atoa neno.

Kati ya wachezaji wanaotawala sana vichwa vya habari hivi sasa ni Alexis Sanchez, kuna habari zinasema kwamba mwisho wake kuichezea Arsenal umekaribia lakini kuna habari zinazosema anabaki Arsenal.
Kwa sasa Sanchez yupo katika majukumu ya timu yake ya taifa na mambo mengi ambayo yanazungumzwa kuhusu yeye sio ya kuaminika kwa kuwa mwenyewe Sanchez hajasema lolote amekaa tu kimya.
Lakini baada ya ukimya wa muda mrefu Sanchez ameibuka na kusema kitu kuhusiana na suala lake la usajili, Alexis Sanchez hajaongea kile ambacho mashabiki wanataka kusikia kwani ameongea kwa lugha ya mafumbo.
“Naangalia ambacho wakala wangu atakifanya, ila kwa sasa kitu pekee katika kichwa changu ni kuisaidia Chile katika michezo iliyoko mbele yetu, wawawkilishi wangu wanafanya vitu kwa ajili yangu na watakaa na klabu kujua nini ni bora kwa ajili yangu” alisema Sanchez.
Tayari tetesi zilisema Alexis Sanchez anakaribia kumwaga wino katika klabu ya Manchester City lakini kumejitokeza wapinzani wapya wa Man City ambao ni klabu ya Bayern Munich wanaotajwa kumtaka Sanchez kwa nguvu zote.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sKClaw
via IFTTT


Saudi Arabia wafanya tukio la aibu wakati wa mchezo dhidi ya Australia.

Saudi Arabia wafanya tukio la aibu wakati wa mchezo dhidi ya Australia.

“Fair play” ndio kitu ambacho kimekuwa kikisisitizwa na Fifa kila siku, mpira unatakiwa utumike kama sehemu ya kuleta amani kati yetu,upendo kati yetu na pia kuwafariji wale waliopoteza faraja za maisha.
Lakini Saudi Arabia kwao ilikuwa tofauti wakati wa mchezo kati ya Saudi Arabia dhidi ya Australia, katika mchezo huo wachezaji walipaswa kujipanga mstari kabla ya mchezo huo kama kumbukumbu na pole kwa wahanga wa tukio la kigaidi lililotokea mjini London.
Australia walishikana mabega na wakajipanga mstari lakini wachezaji wa kikosi cha kwanza wa Saudi Arabia hawakufanya hivyo kwani kila mmoja alikaa kivyake akifanya yake na huku baadhi ya watu wa benchi lao la ufundi walionekana wakiwa wamekaa wakati wa tukio hilo.
Japokuwa kiongozi mmoja wa chama cha soka nchini Saudi Arabia amedai kwamba kwao utaratibu wa kupanga mstari huwa haupo lakini kumbukumbu zinaonesha kwamba mwaka 2005 timu hiyo ya taifa ya Saudi Arabia ilishawahi kupanga msatari kwa ajili ya “moment of silence”.
Chama cha soka cha Saudi Arabia kimeomba radhi kwa wahanga wa tukio hilo na kimesisitiza kwamba kinapinga kwa nguvu zote masuala ya kigaidi na tukio walilofanya halikuwa na nia ya kuwaudhi wahanga wa tukio lililotokea London.
Katika tukio hilo la kigaidi lililotokea London kulikwa na Waaustralia wawili waliofariki Sara Zelenak na Kirsty Boden walifariki katika mlipuko huo na Sara alikuwa ni nesi alifariki wakati akikimbia kwenda kujaribu kumuokoa mgonjwa.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2t26JfV
via IFTTT


NJIA 3 RAHISI ZA KUONDOA GARI LA MANUAL TRANSMISSION KWENYE MWINUKO

NJIA 3 RAHISI ZA KUONDOA GARI LA MANUAL TRANSMISSION KWENYE MWINUKO

Watu wengi sana hasa wanawake hupata wakati mgumu kuendesha gari lenye mfumo wa ‘manual transmission’ kwani magari haya humtaka dereva kufanya kila kitu mwenyewe tofauti na ‘automatic transmission’ ambalo baadhi ya mambo hufanya lenyewe na hivyo kumuachia dereva majukumu machache tu.
Changamoto inayowakumba wengi hata ambao wamekuwa wakiendesha gari la manual transmission kwa muda mrefu ni namna ya kuondoka kwenye eneo lenye mwinuko pasi na gari kurudi nyuma ambao linaweza kusababisha madhara kama kuna gari jingine limeegeshwa nyuma.
Kwa ufupi tutaangalia njia tatu za kukusaidia kuweza kuondoa gari lako katika sehemu yenye mwinuko bila kusababisha madhara au gari lako kurudi nyuma.
Njia ya kwanza ni kutumia breki ya dharura. 
Breki hii watu wengi huifahamu kama breki mkono (hand break) kwa sababu kwenye magari mengi huwekwa kwa kutumia mkono, lakini ni vyema kuelewa kuwa kuna magari mengine breki hii huwekwa kwa kutumia mguu.
Namna ya kutumia breki hii kuondoa gari lako kwenye kilima kwanza hakikisha breaki yako ya dharura umeiweka halafu unaweza kuliwasha gari lako, kanyaga pedo ya ‘clutch’ baada ya hapo, ingiza gia namba moja, halafu kanyaga mafuta kiasi huku ukiiachia pedo ya clutch taratibu. Baada ya sekunde utaona gari kama linaanza kutikisika na ukishuka au kuitoa breki yako ya dharura, gari litaondoka bila kurudi nyuma.
Mambo ya msingi ya kuzingatia hapa ni kuwa, ukubwa au mwinuko wa kilima ndio utaamua ni mafuta kiasi gani uweke. Kadiri kilima kinavyoinuka zaidi, ndiyo mafuta yakavyohitajika kwa gari lako kuondoka bila matatizo. Lakini pia hakikisha unapoachia clutch yako, unaiachia taratibu na si kwa ghafla kwani gari litazima.
Njia ya pili ni kutumia breki na kichapuzi (accelerator) kwa wakati mmoja.
Njia hii ni rahisi pia lakini inakutaka kuwa makini na mguu wako kuwa mwepesi kiasi unapoitumia kuondoa gari lako kwenye kilima bila kuleta madhara.
Unachotakiwa kufanya hapa ni, kuwasha gari lako, kisha kanyaga clutch na kuweka gia namba moja, ikifuatiwa na breki kisha ondoa breki yako ya dhararu (hand break) ambapo sasa gari litakuwa likiitegemea breki yako uliyokanyaga kwenye mguu. Hivyo unatakiwa kuwa makini kwani miguu yako ikiwa mizito kidogo unaweza kusababisha madhara.
Baada ya kutoa breki ya mkono, mguu wako wa kulia ambao umekanyaga breki uweke kwa upande (kama pichani hapo juu) uwe juu ya pedo ya breki na accelerator kwa wakati mmoja lakini wakati huo sehemu ya kisigino cha mguu wako kinatakiwa kiwe bado kimeshikilia breki, wakati sehemu ya vidole ikiwa juu ya pedo ya mafuta. Utakachotakiwa kufanya ni kuachia pedo ya clutch taratibu huku ukiinua kisigino chako na wakati huo huo sehemu ya mbele ya mguu wako ukiminya pedo ya mfuta, na gari litaanza kuondoka.
Muhimu, hakikisha miguu yako inafanyakazi kwa ushirikiano sawa kwani, mfano, ukiinua kisigino bila kubonyeza pedo ya mafuta gari litarudi nyuma kwa kukosa nguvu ya kulipeleka mbele, au ukiminya pedo ya mafuta na breki kwa wakati mmoja, gari litaishia kupiga kelele bila kwenda popote, hivyo hakikisha miguu yako inawasiliana.
Njia ya tatu ni kutumia uwiano wa pedo ya clutch na mafuta.
Njia hii hutumiwa mra nyingi na watu ambao ni wazoefu sana katika kuendesha magari ya manual transmission ambayo inamtaka dereva kuweza kuweka uwiano sawa wa kukanyaga pedo ya clutch na mafuta kwa wakati mmoja.
Kinachofanyika katika njia hii ni kuwa, dereva akiwasha gari lake, ataingiiza gia wakati mguu wake upo kwenye breki ili aweze kuondoa breki ya mkono bila gari kurudi nyuma. Baada ya hapo dereva atahamisha mguu wake kutoka kwenye breki kwa haraka na kuuhamishia kwenye pedo ya mafuta wakati huo huo ataachia cluth kwa kiasi fulani ili aweze kukanyaga mafuta yatakayoruhusu gari kuondoka.
Ukiitumia njia hii, hakikisha kuwa hauruhusu mafuta mengi kuingia kwenye injini wakati unahamisha mguu wako kwa haraka, au kuachia clutch ghafla hadi mwisho kwani gari litashtuka na kuzima.
Njia hii inaaminika kuwa ni ngumu zaidi kuliko mbili zilizotangulia kwani inamhitaji dereva kufanya maamuzi kwa haraka zaidi na kuhakikisha kuwa yanakuwa ya ufasaha.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rdiQp9
via IFTTT


Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

Nimerudi kutoka kazini mida ya saa 12 jioni, nikapaki gari langu ndani ya fence, nikaamua niangalie TV na nakufanya shughuli zangu za ofisini.
Baada ya kula mida ya saa mbili, nikaenda kulala mapema tu.
Naamka hasubuhi, nakuta gari limesogweza karibia na geti na limeibiwa vipuli vya gari, (kuanzia taa za mbele na nyuma, site mirror, bumper la mbele na nyuma, na vitu vya ndani).
Wizi wa Vifaa vya gari
Nikaamua kwenda Police kuripoti, nikaambiwa awa watu wako sana na hizi kesi tunazipata kila siku ya mungu, na Police wawili wakakiri ata wao wameshaibiwaga.
Baada ya kuongea na rafiki zangu kuhusu tukio langu, nikaambiwa kitu hichohicho kwamba ata maeneo yeo wamepiga magari kama manne siku za karibuni, na wengine wakinisimulia matukio hayo ya uwizi yalivyowatoke kwao au kwa familia/rafiki zao miezi michache iliyopita.
Kitu kimoja walichokuwa wanaongea sawa na kukubaliana (Police and Raia) ni kwamba wote wanajuwa hivyo vitu vinapopelweka “GEREZANI MNADANI”. Na ata vya kwangu nikaambiwa viko na mpaka wanajuwa vimeibiwa wapi na lini.
Swali langu na natumaini watu wengi wanajiuliza!
Kwa hiyo hii taabia itaendelea mpaka lini? Tunazungumzia vifaa vyenye thamani mpaka zaidi ya million 7 saa nyinginee watu wanaibiwa na visivyopunguwa laki 6.
Hii ni biashara kubwa yenye mtandao mkubwa na inaaribu uchumi wa wananchi wema na kama sio wa Nchi.
Tunashindwa nini kwenda kupafunga Gerezani Mnadani na kuwakamata wausika watoe ushirikiano kuhusu watu wanaofanya uwizi huwo. Kwa ujumla ni eneo linalo ifadhi vitu vya ujambazi, Mpaka wanajigamba kwamba “Si Serikali ya Magufuli wala ya Mtu yeyote itakayoweza kuwafanya kitu”.
Hii ni kauli ya Dharau kwa vyombo vya Dola na Serikali ya Rais wetu Mchapa kazi Magufuli asiyependa watu kama hao wanaotaka kuishi kwa majasho ya watu wengine.
Ombi langu kwa wananchi wenzangu:
Mie nimeanza kupaza sauti , lakini sauti yangu ni ndogo sana, tukishirikiana mimi na wewe hii sauti itakuwa kubwa na itasikika, na Amin’ na waambia RAIS WETU MAGUFULI Hashindwi kuwashughulikia awa watu na hii tabia ikapungua ama kuisha kabisa.
Note: HAKUNA KINACHOSHINDIKANA KATIKA DUNIA.
By Ruukada
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rIMPZt
via IFTTT


Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

Nimerudi kutoka kazini mida ya saa 12 jioni, nikapaki gari langu ndani ya fence, nikaamua niangalie TV na nakufanya shughuli zangu za ofisini.
Baada ya kula mida ya saa mbili, nikaenda kulala mapema tu.
Naamka hasubuhi, nakuta gari limesogweza karibia na geti na limeibiwa vipuli vya gari, (kuanzia taa za mbele na nyuma, site mirror, bumper la mbele na nyuma, na vitu vya ndani).
Wizi wa Vifaa vya gari
Nikaamua kwenda Police kuripoti, nikaambiwa awa watu wako sana na hizi kesi tunazipata kila siku ya mungu, na Police wawili wakakiri ata wao wameshaibiwaga.
Baada ya kuongea na rafiki zangu kuhusu tukio langu, nikaambiwa kitu hichohicho kwamba ata maeneo yeo wamepiga magari kama manne siku za karibuni, na wengine wakinisimulia matukio hayo ya uwizi yalivyowatoke kwao au kwa familia/rafiki zao miezi michache iliyopita.
Kitu kimoja walichokuwa wanaongea sawa na kukubaliana (Police and Raia) ni kwamba wote wanajuwa hivyo vitu vinapopelweka “GEREZANI MNADANI”. Na ata vya kwangu nikaambiwa viko na mpaka wanajuwa vimeibiwa wapi na lini.
Swali langu na natumaini watu wengi wanajiuliza!
Kwa hiyo hii taabia itaendelea mpaka lini? Tunazungumzia vifaa vyenye thamani mpaka zaidi ya million 7 saa nyinginee watu wanaibiwa na visivyopunguwa laki 6.
Hii ni biashara kubwa yenye mtandao mkubwa na inaaribu uchumi wa wananchi wema na kama sio wa Nchi.
Tunashindwa nini kwenda kupafunga Gerezani Mnadani na kuwakamata wausika watoe ushirikiano kuhusu watu wanaofanya uwizi huwo. Kwa ujumla ni eneo linalo ifadhi vitu vya ujambazi, Mpaka wanajigamba kwamba “Si Serikali ya Magufuli wala ya Mtu yeyote itakayoweza kuwafanya kitu”.
Hii ni kauli ya Dharau kwa vyombo vya Dola na Serikali ya Rais wetu Mchapa kazi Magufuli asiyependa watu kama hao wanaotaka kuishi kwa majasho ya watu wengine.
Ombi langu kwa wananchi wenzangu:
Mie nimeanza kupaza sauti , lakini sauti yangu ni ndogo sana, tukishirikiana mimi na wewe hii sauti itakuwa kubwa na itasikika, na Amin’ na waambia RAIS WETU MAGUFULI Hashindwi kuwashughulikia awa watu na hii tabia ikapungua ama kuisha kabisa.
Note: HAKUNA KINACHOSHINDIKANA KATIKA DUNIA.
By Ruukada
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sKiSXn
via IFTTT


Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

Nimerudi kutoka kazini mida ya saa 12 jioni, nikapaki gari langu ndani ya fence, nikaamua niangalie TV na nakufanya shughuli zangu za ofisini.
Baada ya kula mida ya saa mbili, nikaenda kulala mapema tu.
Naamka hasubuhi, nakuta gari limesogweza karibia na geti na limeibiwa vipuli vya gari, (kuanzia taa za mbele na nyuma, site mirror, bumper la mbele na nyuma, na vitu vya ndani).
Wizi wa Vifaa vya gari
Nikaamua kwenda Police kuripoti, nikaambiwa awa watu wako sana na hizi kesi tunazipata kila siku ya mungu, na Police wawili wakakiri ata wao wameshaibiwaga.
Baada ya kuongea na rafiki zangu kuhusu tukio langu, nikaambiwa kitu hichohicho kwamba ata maeneo yeo wamepiga magari kama manne siku za karibuni, na wengine wakinisimulia matukio hayo ya uwizi yalivyowatoke kwao au kwa familia/rafiki zao miezi michache iliyopita.
Kitu kimoja walichokuwa wanaongea sawa na kukubaliana (Police and Raia) ni kwamba wote wanajuwa hivyo vitu vinapopelweka “GEREZANI MNADANI”. Na ata vya kwangu nikaambiwa viko na mpaka wanajuwa vimeibiwa wapi na lini.
Swali langu na natumaini watu wengi wanajiuliza!
Kwa hiyo hii taabia itaendelea mpaka lini? Tunazungumzia vifaa vyenye thamani mpaka zaidi ya million 7 saa nyinginee watu wanaibiwa na visivyopunguwa laki 6.
Hii ni biashara kubwa yenye mtandao mkubwa na inaaribu uchumi wa wananchi wema na kama sio wa Nchi.
Tunashindwa nini kwenda kupafunga Gerezani Mnadani na kuwakamata wausika watoe ushirikiano kuhusu watu wanaofanya uwizi huwo. Kwa ujumla ni eneo linalo ifadhi vitu vya ujambazi, Mpaka wanajigamba kwamba “Si Serikali ya Magufuli wala ya Mtu yeyote itakayoweza kuwafanya kitu”.
Hii ni kauli ya Dharau kwa vyombo vya Dola na Serikali ya Rais wetu Mchapa kazi Magufuli asiyependa watu kama hao wanaotaka kuishi kwa majasho ya watu wengine.
Ombi langu kwa wananchi wenzangu:
Mie nimeanza kupaza sauti , lakini sauti yangu ni ndogo sana, tukishirikiana mimi na wewe hii sauti itakuwa kubwa na itasikika, na Amin’ na waambia RAIS WETU MAGUFULI Hashindwi kuwashughulikia awa watu na hii tabia ikapungua ama kuisha kabisa.
Note: HAKUNA KINACHOSHINDIKANA KATIKA DUNIA.
By Ruukada
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2r2CkNP
via IFTTT


Zitto Kabwe na Profesa Kitila Mkumbo watofautiana kwa mara ya kwanza hadharani

Zitto Kabwe na Profesa Kitila Mkumbo watofautiana kwa mara ya kwanza hadharani

Kwa mara ya kwanza, Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ametofautiana hadharani kimtazamo na aliyekuwa mshauri wa chama hicho, Profesa Kitila Mkumbo ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
Profesa Mkumbo na Zitto walitofautiana jana kuhusu Bajeti ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2017/2018 iliyosomwa jana bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango.
Msomi huyo alikuwa wa kwanza kuandika kwenye akaunti yake ya Twitter akiimwagia sifa bajeti hiyo pamoja na namna ilivyowasilishwa na Dk. Mpango, akieleza kuwa ni bajeti safi na kwamba anajivunia kuwa sehemu ya timu iliyoiwasilisha.
Hata hivyo, Zitto aliibuka na mawazo kinzani akieleza kuwa bajeti hiyo haitekelezeki, huku akikumbusha kuwa katika bajeti iliyopita ni asilimia 30 pekee ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo zilitolewa na kwamba asilimia 20 ya fedha hizo zilipotea.
Jana, idadi kubwa ya wabunge walionesha kuipokea kwa furaha kuu bajeti iliyosomwa na Dk. Mpango ambayo pamoja na mambo mengine ilitaja kuondoa ada ya mwaka ya leseni ya magari, kupunguza kodi ya bidhaa za mazao huku ikipandisha kodi ya mafuta na bia.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rTSTg6
via IFTTT


Matokeo Yamweka njiapanda Waziri Mkuu Uingereza

Matokeo Yamweka njiapanda Waziri Mkuu Uingereza

Uingereza. Matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika jana Alhamisi, nchini Uingereza yanaonyesha wazi kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi mkubwa wa wabunge wa kukiwezesha kuunda serikali peke yake.
Hili ni pigo kwa Waziri Mkuu, Theresa May aliyeitisha uchaguzi wa mapema akiamini kuwa atapata uungwaji mkono na kuaminiwa, ili aweze kuongoza serikali peke na kuepuka serikali ya muungano.
Hakufanikiwa. May na chama chake cha Conservative anatarajiwa kupata ushindi wa viti 318, huku kile cha Labour kikitarajiwa kupata 262. Hadi asubuhi leo Ijumaa, Conservative ilikuwa na viti 314 na Labour 261 huku Bunge zima likiwa na wabunge 650.
Waziri Mkuu May amesema baada ya matokeo ya mwisho kutangazwa, kutakuwa na muda wa uthabiti huku kiongozi wa Chama cha Labour, Jeremy Corbyn akimtaka May ajiuzulu.
Conservative ilikuwa inahitaji viti 326 ili kuongoza serikali peke yake, lakini kwa namna mambo yalivyo, itabidi kupata uungwaji mkono kutoka chama kingine ili kuunda Serikali.
Haijafahamika iwapo May ataendelea kuongoza chama hicho kutokana na matokeo haya mabaya, kinyume na matarajio yake au atajiuzulu. Kazi kubwa iliyo mbele ya serikali mpya itakayoundwa ni kuendeleza na kufanikisha mchakato wa kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2r2ByjT
via IFTTT


Kategori

Kategori