Exclusive. Hatimaye Nabii Frank Afichua Kiini cha Mauaji ya Kibiti na Rufiji..!!!

Akizungumza mapema asubuhi ya leo na Kituo cha Luninga cha Channel Ten na Magic fm Radio Nabii anayekuja kwa Kasi nchini Nabii Frank leo amefunguka na kueleza mambo makuu mawili ambayo ndiyo chanzo cha mauaji yanayoendelea Kibiti na Rufiji na amezitaka Mamlaka husika kuyafanyia Kazi ili kumaliza mauaji.
Amesema kwamba mauaji hayo yanatokana na sababu za Harakati za Kidini ( yaani kuna dini moja inataka kuwa ndiyo inayoaminika na kukubalika katika huo Ukanda hivyo wanaua Watu hasa wa dini fulani ili kuwatisha na wakimbie au wahame hayo maeneo na wabaki wao tu ) na sababu ya pili kasema kwamba Mfumo wa Kiuchumi wa Watu wa hayo maeneo umeharibiwa hivyo Wauwaji wameamua sasa kuwauwa wale wote ambao wanahisi ndiyo chanzo cha Mfumo wao huu kuharibiwa. Na inasemekana kwamba Mfumo mkubwa wa Kiuchumi au uingizaji Kipato kwa asiimia kubwa ya Watu wa hayo maeneo ni Mkaa na kama tunavyojua Serikali imepiga marufuku huku ikiweka Sheria kali dhidi ya wale watakaokamatwa.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sKFMh8
via IFTTT