Showing posts with label April 15. Show all posts
Showing posts with label April 15. Show all posts
CCM Wamteua DR Gertrude Rwakatare Kuchukua Nafasi ya Sophia Simba Aliyefukuzwa

CCM Wamteua DR Gertrude Rwakatare Kuchukua Nafasi ya Sophia Simba Aliyefukuzwa

Mchungaji Dkt. Getrude Rwakatare ameteuliwa kuwa Mbunge Viti Maalumu(CCM) kuchukua nafasi ya Sophia Simba aliyefukuzwa uanachama.
Ikumbukwe kuwa kwa mara ya kwanza Mchungaji Rwakatare alipata nafasi kama hii katika Bunge lililopita.
Uteuzi huu umekuja baada ya Spika wa Bunge kuiandikia barua ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na kuiarifu juu ya uwepo wa nafasi ya Ubunge Maalum kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) baada ya Sophia Simba kupoteza sifa za kuwa Mbunge baada ya kuvuliwa uanachama.

from Blogger http://ift.tt/2plPzc9
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2ohp3P2
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oKt56G
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2pm95oO
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2pmBuek
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oC0mjN
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oyj6iA
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oKQ4hK
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2pjKl3b
via IFTTT


TRA Waja na Mbinu Mpya ya Kuwabana Wakwepa Kodi Kupitia Mashine ya EFDโ€ฆ!!!

TRA Waja na Mbinu Mpya ya Kuwabana Wakwepa Kodi Kupitia Mashine ya EFD…!!!

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imeendelea kuwabana wala rushwa na wanaoghushi risiti za ukusanyaji maduhuli kwa kuboresha mfumo wa kieletroniki wa utumiaji wa mashine za (EFD) utakaowezesha miamala na risiti kuwa na saini za kieletroniki.
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Neema Mrema, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kwa ajili ya taasisi na mashirika ya umma.
Mrema alisema hivi karibuni mawakala wa mashine za kieletroniki za kutumia risiti watawafungia mfumo huo taasisi na mashirika hayo ili wakusanye maduhuli kupitia mashine hizo.
Aidha, alisema TRA imefanya mabadiliko katika mfumo wa usimamizi wa matumizi ya mashine za kieletroniki za utoaji risiti (EFDMS) pamoja na mashine za EFD ili kupunguza gharama kwa serikali.
Alisema mfumo huo wa kielektroniki utaipunguzia serikali gharama za kununua mashine halisi kwa kuwa umeunganishwa na mfumo wa kuhifadhi taarifa wa TRA.
“Una usalama wa hali ya juu kwani miamala na risiti zote itakuwa na saini ya kieletroniki … hivyo kunapunguza uwezekano wa kughushi risiti kutoka kwenye mashine ambazo hazijasajiliwa na mfumo wa TRA,” alisema.
Pia alisema mfumo huo ni wa kiintelejensia kutokana na kuwa na uwezo wa kutambua hati ya mauzo kwa mkopo, marejesho ya mauzo, risiti halali na za kudurufu.
Kadhalika, alisema mfumo huo ni rafiki na unaweza kuunganishwa na mifumo mingine kama ya ankara, mauzo na stakabadhi kwa kufanya mabadiliko machache na una ruhusu matumizi ya fedha mbalimbali.
Aliongeza kuwa mfumo huo ni wa uwazi kwa sababu ukomo wa kila risiti unahakikiwa na una uwezo wa kutambua huduma kama imetolewa au la.
Kuhusu kodi ya zuio iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2013, kamishna huyo alisema imekuwa na changamoto kwa idara na taasisi za serikali kutokana na wahusika kukosa uelewa wa kutosha wa utozaji wa kodi husika.
“Kumekuwa na mkanganyiko kati ya utozaji wa kodi ya zuio ya asilimia mbili katika usambazaji wa bidhaa kwa Idara na taasisi za serikali zinazotegemea bajeti ya serikali kuu kwa asilimia 100 na ile ya asilimia tano kwa huduma,” alisema.
Alisema kupitia mafunzo hayo washiriki wataelimishwa kuhusu mabadiliko ya sheria fedha ya mwaka 2016, sheria ya kodi ya ongezeko la thamani ya mwaka 2014, kodi ya zuio katika bidhaa na huduma na mfumo huo wa ukusanyaji maduhuli.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi TRA, Richard Kayombo, alisema utumiaji wa risiti za kawaida umekuwa ukitoa mianya ya upoteaji wa mapato hivyo kupitia mafunzo hayo wanaamini washiriki watatambua wajibu wao katika kuhakikisha makusanyo yanaongezeka.
Mhasibu Mwandamizi kutoka Bodi ya Sukari Tanzania, Devotha Sanga, alitaja changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni kushindwa kutambua viwango vinavyotakiwa kutozwa kwa mtu binafsi au kampuni kupitia kodi ya zuio ni asilimia ngapi.
Pia alisema katika kodi ya ongezeko la thamani kumekuwa na changamoto ya risiti za kughushi ambazo wanashindwa kuzitambua.

from Blogger http://ift.tt/2pi9YSb
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2ohmYmv
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2odZQ9h
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2pmcqnR
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oKmfhq
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oBWNKv
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nP2INz
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2ohGXl0
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oyF6tU
via IFTTT


Polisi Kenya Watoa Angalizo kwa Wananchi, ni Kufuatia Taarifa za Ujasusiโ€ฆ!!!

Polisi Kenya Watoa Angalizo kwa Wananchi, ni Kufuatia Taarifa za Ujasusi…!!!

Vikosi vya Usalama nchini Kenya viko katika hali ya ulinzi mkali na tahadhari baada ya kupokea taarifa za ujasusi kwamba wanamgambo wamekuwa wakipanga mashambulizi ya kigaidi wakati au baada ya sikukuu ya Pasaka.
Hayo yamethibitishwa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kenya, George Kinoti ambapo ameeleza kuwa wamepokea taarifa za ujasusi zikieleza kuwa wanamgambo tisa wanapanga mashambulizi, hivyo tayari vikosi vya usalama vimejiimarisha na kuhakikisha kunakuwa na tahadhari ya juu kudhibiti mashambulizi yasitokee.
Jeshi hilo limetoa wito kwa wananchi wote kuwa waangalifu kwa hali ya juu kabla ya sikukuu ya Pasaka na kuripoti shughuli zote watakazozitiliwa shaka.

from Blogger http://ift.tt/2ohhLLp
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2ohmgWg
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oKehoH
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2pm9Qyh
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2pmwtlZ
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oBLKks
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oy7yfp
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oKPMb0
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2pjJsYC
via IFTTT


Ndoa ya Lulu na Boss wa EFM Majay yanukia

Ndoa ya Lulu na Boss wa EFM Majay yanukia

Elizabeth Michael (Lulu) amedai ndoa yake na mpenzi wake Dj Majay inakaribia.
Muigizaji huyo ambaye ameonekana kutulia sana tangu alipokuwa na mahusiano na bosi huyo wa EFM na TVE amesema hivi karibuni wale waliokuwa wakitaka waachane watabaki midomo wazi. “Siku zinakaribia na karibu tarehe ya ndoa yangu itatangazwa kwa uwezo wa Mungu. Hapo ndipo waliotamani tuachane wataziba midomo, maana natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni,” ameliambia gazeti la Mtanzania.
Lulu ameongeza kuwa anatamani kuwa mke bora kwenye ndoa yake kama alivyokuwa sasa kwenye mahusiano yake.

from Blogger http://ift.tt/2nOoYHn
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2ohrIIx
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2odSWRr
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2pm3G0K
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oKAMcZ
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oC334V
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nPiBn8
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oi1Dt3
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2pjHojh
via IFTTT


Baada ya Kutekwa Roma Aamua Kuimba Nyimbo za Kumsifu Mungu

Baada ya Kutekwa Roma Aamua Kuimba Nyimbo za Kumsifu Mungu

Msanii wa muziki wa hip hop Roma Mkatoliki Ijumaa hii katika mitandaoni ya kijamii amekuwa gumzo baada ya kuonekana akiimba wimbo wa kumsifu Mungu ikiwa na wiki moja toka atekwe na kuachiwa.
Katika video hiyo rapa huyo amelalamika jinsi watu wanavyomsema vibaya kutokana na matatizo hayo ambayo yalimkuta akiwa na wenzake watatu.
Roma alisisika akisema “Ninalalaa macho wazi mimi, kama ndege mkiwa juu ya paaa, Nimekuwa kama muhuni mimi, fanya ima, fanya ima bwana uniokoee. Nimekuwa kama kichekesho kwa watu mimii bwanaa, kila nipitapo kunisema nakunicheka, munguu wangu mbona umeniachaa,”
Rapa huyo na wezake walitekwa na watu wasiojulikana wakiwa Tongwe Record na baadaye kutelekezwa katika beach za Uninio Jijini Dar es salaam

from Blogger http://ift.tt/2p53ZjI
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2ohwlCv
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oe4t2W
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2pm7OxQ
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2pmwqXl
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oBOv5C
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nP2eXS
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oKNdFS
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2oyBQP7
via IFTTT


Kategori

Kategori