Showing posts with label 2017 at 02:10PM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 02:10PM. Show all posts
DALILI TANO KWAMBA UNAFANYA KAZI NA BOSI MZURI

DALILI TANO KWAMBA UNAFANYA KAZI NA BOSI MZURI

Majukumu ya uongozi makazini yamekuwa yakibadilika hasa katika miaka michache iliyopita. Ni watu wachache wameweza kugundua hili mpaka sasa, lakini majukumu ya uongozi mwanzoni ilikuwa ni kulinda utawala na kusimamia sheria na taratibu. Mameneja walikuwa na jukumu la kuhakikisha wafanyakazi wanatimiza malengo ya kampuni na mara nyingi bila kujali kuhusu kuwawezesha, kuwahusisha au kufanya lolote kuhusu maendeleo ya wafanyakazi wake. Sasa mambo yamebadilika na yanaendelea kubadilika kwa kasi. Majukumu ya uongozi sasa yamebadilika, na zifuatazo ni dalili tano kwamba unafanya kazi chini ya bosi mzuri:
Anakuwa kama kocha
Makocha na walimu ni huhamasisha maendeleo ya watu wengine. Hutusaidia wakati wote maishani mwetu, iwe kwenye michezo au matibabu. Hii ndio sababu ya kuhitaji kuwa na kocha mahala pa kazi na mtu bora zaidi kuichukua nafasi hii ni meneja wako. Mameneja wazuri zaidi huhamasisha wafanyakazi wake kutimiza malengo yao kama ambavyo mwalimu wa michezo anafanya. Mameneja wa aina hii wana upeo wa kuona thamani yako mbali na kazi aliyokupa na kutaka mafanikio ya wafanyakazi wake. Viongozi wa namna hii wanaamini katika kuwainua wafanyakazi wake, kuwasaidia kutatua matatizo yao na kuwawezesha wapate mafanikio zaidi.
Anayaelewa mapungufu yako lakini anajali zaidi unayoyamudu
Ni rahisi sana kuona mapungufu ya mtu. Kama jambo halikwenda kama lilivyopangwa, ni rahisi kulaumu wengine. Ni ngumu kuangalia nje ya mapungufu ya watu na kuzingatia ubora na vipaji vyao halisi. Hii haimaanishi udharau mapungufu waliyonayo wafanyakazi – kinachomaanishwa ni kwamba kuelewa kwamba mapungufu yapo lakini anaamua kuwekea mkazo kwenye mambo unayoyaweza. Mameneja wazuri wanaelewa uwezo wa wafanyakazi wao na wanawahamasisha watumie vipaji vyao. Hili linaonekana sana kwenye michezo yote ambapo kocha humuweka mchezaji kwenye nafasi ambayo itampa mafanikio zaidi. Hili linahitajika zaidi makazini na mameneja ndio walitekeleze.
Anataka kujua historia yako
Kila mtu ana historia ya maisha toka utotoni mwake mpaka alipofikia sasa, mambo anayothamini na jinsi anavyotaka maisha yake yawe. Hadithi ya maisha yako ndiyo inakuelezea zaidi na mameneja bora wanapenda kuisikia toka kwako kwakuwa wanahitaji kumjua mtu zaidi ya kuwa unafanya kazi kwenye kampuni yake. Wanaweza kufanya hivi kwa kukuuliza tu “unaendeleaje?” au kuwachukua wafanyakazi wake na kwenda sehemu kuzungumzia mambo tofauti yasiyohusu kazi. Kwa mameneja, kujenga uhusiano wa namna hii na wafanyakazi wake ni muhimu sana, kwahiyo kama meneja wako yupo hivi, jihesabu mwenye bahati.
Wanatambua mapungufu yao
Mameneja wazuri wanakubali mapungufu yao na hawapendi kuigiza kujua kila kitu maishani. Wanahitaji kujua hadithi za wafanyakazi wao na pia hawaogopi kuhadithia historia za maisha yao ili wafanyakazi waweze kumjua vizuri zaidi. Mara nyingi tumesikia habari mameneja wakishuhudiwa kufanya jambo moja wakiwa mtaani na kubadilika kuwa mtu tofauti kabisa akiwa ofisini, anageuka kuwa roboti asiyetaka ushauri wa mtu – na watu hawapendi kufanya kazi na roboti, wanataka kufanya kazi na mtu anayetambua kwamba yeye si mtimilifu.
Huukosoa utaratibu uliozoeleka wa kufanya kazi
Maya nyingi makazini mwetu, taratibu na mbinu za kufanya kazi zimekuwa ni zile zile kwa miongo migi sana wakati dunia imebadilika sana katika miaka michache iliyopita lakini taratibu za utendaji kazi hazibadiliki kuendana na mabadiliko ya wakati. Ni sawa na kuishi mwaka 2017 lakini tunafanya kazi kwa taratibu zilizokuwa ni sahihi miaka ya 1970. Mameneja wazuri wanaelewa kuwa mara nyingine kuleta mabadiliko ni jambo zuri kuliko kuyazuia yanapotokea. Mameneja wa aina hii hawaulizi tu swali, “kwa nini tunafanya namna hii?” bali wanahamasisha wafanyakazi wawe wabunifu na kuja na mbinu mpya zitakazoboresha utendaji. Mabadiliko haya yaweza kuwa ni kuanzisha utaratibu mpya, matumizi ya teknolojia mpya au kubadilisha mpamgilio wa vitu ndani ya ofisi, mameneja wazuri huwa ni lazima watabadili taratibu zilizozoeleka!

from Blogger http://ift.tt/2twLi6c
via IFTTT


KIJANA Ajinyonga Kwa Kamba Juu ya Mti Kisa Ugumu wa Maisha….

KIJANA Ajinyonga Kwa Kamba Juu ya Mti Kisa Ugumu wa Maisha….

Kijana Paulo Ezekiel, amejinyonga kutokana na kile kinachodaiwa ugumu wa maisha.
Paulo (17) alikuwa anaishi na wazazi wake Mtaa wa Mazinge Kata ya Ndembezi mjini Shinyanga, alifariki dunia juzi usiku kutokana na kudaiwa kujinyonga kwa kamba juu ya mti jirani na nyumbani kwao.
Picha ya Tukio jingine
Tukio hilo lilitokea majira ya saa kumi alfajiri baada ya marehemu kutoka nje ya geti la nyumba yao na kuelekea kwenye mti huo kisha kijipiga kitanzi kunakodaiwa kusababisha kifo chake.
Akizungumza tukio hilo jana, baba mzazi wa marehemu, Ezekiel alisema awali kijana wake alikuwa na ugomvi na marafiki zake ambao ni madereva bodaboda, lakini huo ulisuluhishwa na akaendelea na majukumu yake.
Alisema chanzo cha kifo chake hakijafahamika vizuri, lakini mara kwa mara alikuwa akilalamika kuwa maisha ni magumu.

“Ilipofika majira ya saa 10 usiku nilisikia mlango wa chumba cha kijana wangu ukifunguliwa, nikajua ametoka kwenda kujisaidia lakini muda mrefu ulipopita bila kusikia amerudi, ndipo nikatoka nje na kukuta geti la uani likiwa wazi, nikaanza kumtafuta bila mafanikio”, alisema. 

Aliongeza:

“Niliporudi ndani nikamwamsha mama yake mzazi na wadogo zake wa kike, tukaanza kumsaka ndipo tukamuona akiwa juu ya mti jirani na nyumba yetu, akiwa ameshafariki kwa kujinyonga na kamba”. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Jumanne Murilo, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na jeshi la hilo kuhusiana na tukio hilo.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga na unatarajiwa kuzikwa leo kwenye Makaburi ya Mtaa wa Dodoma mjini hapa.
Chanzo: Nipashe
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2srAbg5
via IFTTT


Blackberry yaishtaki Nokia kwa wizi wa teknolojia

Blackberry yaishtaki Nokia kwa wizi wa teknolojia

Kampuni ya simu ya Blackberry inaishtaki Nokia kuhusu madai kwamba kampuni hiyo ya Finland imetumia uvumbuzi wake bila ruhusa.
Madai hayo ya ukiukaji yanahusisha teknolojia inayotumika katika 4G pamoja na mitandao mingine ya simu.
Kampuni hiyo ya Canada inadai kwamba transmita za Nokia pamoja na programu nyengime zinatumia teknolojia yake.
”Tunajua kwamba kuna malalamishi ,tutayajadili madai yaliotolewa na kuchukua hatua zinazohitajika kutetea haki zetu”,alisema msemaji
Kesi hiyo inasikizwa nchini Marekani.
Blackberry inataka kulipwa fedha badala ya kuizuia Nokia kutumia teknolojia yake kulingana na nakala za mahakamani zilizochapishwa na tovuti ya habari ya Ars Technica.
Madai hayo ni pamoja na yale yanayosema kwamba Nokia ilikuwa inajua uwepo wa uvumbuzi huo baada ya kujaribu kuununua hapo awali kabla ya Blackberry kuamua kutumia.
Kampuni hizo mbili zilizozana 2012 wakati Nokia ilipojaribu kuhakikisha kuwa mauzo ya simu za Blackberry yanapigwa marufuku nchini Marekani na Uingereza katika mzozo mwengine.
Kampuni zote mbili zimesitisha utengenezaji wa simu zao na badala yake wametoa leseni za haki ya umiliki wa simu zao kwa kwa watengenezaji wengine wa simu.

from Blogger http://ift.tt/2s3C0lo
via IFTTT


Imefichukaaa..Baada ya Nape Kufukuzwa Uwaziri.. Sasa Mawaziri Njiapanda..!!!

Imefichukaaa..Baada ya Nape Kufukuzwa Uwaziri.. Sasa Mawaziri Njiapanda..!!!

Ingawa wengi walishangaa Rais John Magufuli alipotengua uteuzi wa Charles Kitwanga, mshangao haukuwa mkubwa.
Sifa ya Kitwanga kwa Magufuli ilikuwa ukaribu wake na kiongozi huyo wa nchi, kama Rais alivyowaeleza wananchi katika moja ya mikutano yake.
Ndani ya chama na Serikali, Kitwanga hakuwa na nguvu ya kuweza kushtua watu kutokana na kuvuliwa uwaziri.
Lakini kwa kijana aliyekulia ndani ya CCM, aliyejitoa kukipagania chama hicho, aliyediriki kuwa mstari wa mbele kushambulia walioonekana maadui wa chama na hata kuwasema hadharani mawaziri walioonekana kuwa mizigo, uamuzi wa kumuengua umeshtua wengi.
Na si kushtua pekee, bali unaonekana kutuma ujumbe kwa mawaziri wengine kuwa lolote laweza kutokea.
Nape Nnauye aliachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyofanywa na Rais Magufuli takribani wiki mbili zilizopita. Alivuliwa wadhifa wake wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliyoishikilia kwa takriban mwaka mmoja.
Nafasi hiyo imechukuliwa na Dk Harrison Mwakyembe aliyekuwa Waziri wa Sheria na Katiba, nafasi iliyochukuliwa na mwanasheria nguli nchini, Profesa Palamagamba Kabudi.
Hakuna sababu zilizotolewa za kuachwa kwa Nape, lakini aliondolewa asubuhi ya siku ambayo angewasilisha kwa wakuu wake, akiwemo Rais, ripoti ya uvamizi wa kituo cha televisheni cha Clouds Media uliofanywa na kiongozi wa Serikali aliyeambatana na askari waliokuwa na silaha za moto.
Mbali na kuenguliwa, Nape alistahimili kukabiliana na askari kanzu waliotaka kumzuia asizungumze na waandishi wa habari kuhusu kuenguliwa kwake kwa kumtishia bastola, tukio lililomfanya aeleze kwa hisia kali jinsi alivyoisumbukia CCM, na hasa miezi 28 aliyoielezea kuwa ilimlaza “porini” kuikoa CCM iliyokuwa inazama.
Alielezea hayo yote akiwa juu ya gari baada ya Hoteli ya Prot
Akiwa kada aliyejipambanua kama mpambanaji wa ufisadi, miaka kumi iliyopita, Nape alimshambulia kwa maneno makali aliyekuwa mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la UVCCM, Edward Lowassa kwa madai ya kujihusisha na rushwa katika ujenzi wa jengo la kisasa la umoja huo.
Hata hivyo, Nape alishindwa kuthibitisha madai hayo na hivyo kusimamishwa uanachama wa umoja huo mwaka 2008. Baadaye Rais Jakaya Kikwete alitengua uamuzi huo.
Katika kuendelea kuandamwa na majanga ya kisiasa, mwaka 2010 Nape alipogombea ubunge Jimbo la Ubungo, aliishia katika kura za maoni, badala yake akapitishwa Hawa Ng’umbi ambaye hakummudu John Mnyika wa Chadema.
Kwa mara nyingine, Kikwete alijitokeza kuweka mambo sawa alipomteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi mwaka 2010 na katika Mkutano wa Halmashauri Kuu wa mwaka 2011 akateuliwa kuwa katibu wa itikadi na uenezi.
Akishikilia nafasi hiyo, Nape alifanya kazi na makatibu wakuu wawili ambao ni Wilson Mukama na Abdulrahman Kinana, ambaye walizunguka naye karibu nchi nzima wakishutumu watendaji wa Serikali kuwa hawafuati ilani ya CCM ambayo iligubikwa na kashfa za ufisadi.
Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kumalizika, Nape aliteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Sifa hizo zilimfanya Nape awe mmoja wa mawaziri wachache waliokulia ndani ya CCM, lakini waziri pekee aliyepigana kuisafisha CCM katika kipindi ambacho ilikuwa inaonekana kuanza kupotez umaarufu.
Pamoja na kuingia ndani ya Serikali kwa mara ya kwanza, historia ya Nape ndani ya CCM ilimfanya aonekane kuwa na nguvu zaidi ya mawaziri wengine wazoefu katika baraza la sasa kama William Lukuvi (Ardhi na Makazi), Profesa Jumanne Maghembe (Maliasili na Utalii) na Dk Mwakyembe (Sheria na Katiba na sasa Habari).
Lakini kuachwa kwake sasa kunaweka maswali kama kuna waziri mwingine anaweza kujisikia salama.
Wasomi watoa mtazamo
Wakizungumzia suala hilo, baadhi ya wasomi walisema kuachwa kwa Nape ni tahadhari kwa mawaziri wengine kuwa makini na Rais iwapo wanataka kuendelea kudumu madarakani.
“Hakuna mtu aliye juu ya chama wala hakuna aliye juu ya Serikali. Hata kama umefanya kazi kiasi gani, ukienda kinyume usishangae litakalokupata,” alisema Salim Hamad ambaye ni mhadhiri wa sayansi ya siasa wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).
“Serikalini kuna kitu kinachoitwa collective responsibility (uwajibikaji wa pamoja), hicho naona kilimpitia pembeni Nape.”.
Hata hivyo, alisema Serikali ya Magufuli haina mwelekeo unaoeleweka kiasi kwamba mawaziri nao wanashindwa cha kufuata.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Profesa George Shumbusho alisema Nape ni kiongozi wa Serikali haiwezekani aipinge hadharani akabaki.
“Haiwezekani kiongozi wa Serikali halafu uipinge hadharani, hiyo ni rahisi tu,” alisema Profesa Shumbusho.
Hata hivyo, Nape hakupinga uamuzi wa Serikali, bali alipingana na uvamizi wa kiongozi wa Serikali kwenye studio za kampuni ya Clouds Media.

from Blogger http://ift.tt/2nNO9YT
via IFTTT


Sababu 4 Zinazochangia Kuhisi Maumivu Wakati wa Tendo la Ndoa..!!!

Kuna baadhi ya wanawake wamekuwa wakipatwa na maumivu makali kila wanaposhiriki tendo la ndoa (kujamiana).
Kutokana na tatizo hilo kuna baadhi ya wanawake wamejikuta wakilichukia tendo hilo na baadhi yao hata kuhatarisha ndoa zao.
Leo nimeona niweze kukueleza msomaji wangu hasa wewe mwanamama mwenye tatizo hili kuwa miongoni mwa sababu zinazochangia hali hiyo ya maumivu ni pamoja na hizi zifuatazo hapa chini:-
1. Ukosefu wa ute ute sehemu za siri ambao husaidia kupunguza msuguano wakati wa tendo hilo. Mara nyingi uteute huo hutokana na maandalizi ya kutosha ambayo huweza kufanyiwa mwanamke na mwenzi wake.
2. Maambukizi, mfano fangasi, U.T.I pamoja na magonjwa mengine ya zinaa huweza kupelekea hali hiyo pia ya kuhisi maumivu wakati wa tendo. Hivyo unapoona hali hiyo ni vyema kufika hospitali iliyokaribu nawe ili uweze kufanyiwa uchunguzi zaidi.
3. Pia kuhisi maumivu hayo huweza kuashiria uwepo wa vijiuvimbe vidogovidogo kwenye njia ya uzazi ‘fibroid’ hivyo ni vyema kuwaona wataalam wa afya kwa uchunguzi zaidi unapohisi hali hiyo.
4. Kwa wale ambao huenda hutumia kinga (kondom) nao huweza kupatwa na tatizo hili la maumivu wakati wa tendo, hivyo unapohisi hali hiyo unaweza kubadilisha aina ya kondomu kwani baadhi ya kondomu zinaweza kutowafaha aina fulani ya watu kwa sababu mbalimbali zikiwemo za mzio ‘allergy’.
TAZAMA HARMORAPA ALIVYO TIMUA MBIO BAADA YA KUIONA BASTOLA

from Blogger http://ift.tt/2npb3pm
via IFTTT


Kategori

Kategori