Chadema Njombe yaungana na Ukawa, yapinga kutolewa wabunge wa Ukawa bungeni

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo mkoa wa Njombe kimesema hakikubaliani na hatua iliyo yanywa na bunge ya kuwafukuza bungeni Wabunge wa kambi ya Upinzani na wanao unda ukawa kwa kupinga hati ya dharula katika sera ya gesi na mafuta.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kutangaza nia ya kuwania jimbo la Njombe kusini linaloshikiliwa na Spika wa bunge la Tanzania, mbunge Anna Makinda,  Emmanuel Filangali, mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Njombe Faki Lulandala amesema kuwa Chadema haikubaliani na kitendo hicho kwa kuwa sera hiyo ina maslahi makubwa kwa wananchi hivyo haipaswi kupelekwa haraka.


Lulandala ambaye pia anatangaza nia ya kuwania jimbo la Njombe kusini amesema kuwa anashangaa kuona suala hilo mihumu kwa uchumi wa Watanzania kupelekwa bungeni kwa hati ya dharula wakati suala hilo likitengenezwa kwa utulivu kwa kuzipitia vipengele vilivyomo katika sera linaweza kubadilisha kilimo, na kuboresha mishahara ya watumishi Chadema mkoa wa Njombe hawakubaliani.


Aidha mtiania kuwani ubunge wa chama hicho jimbo la Njombe kusini Emmanuel Filangali amesema kuwa akipitishwa na chama chake na kuwa mbunge atahakikisha uchumi wa mkoa wanjombe unakuwa kwa kusimania pesa zinazoletwa kwaajili ya mfuko wa jimbo.

Amesema kuwa atasimamia Maendeleo vijijini na kuhakikisha vijana wa vijijini hawakimbilii mjini na kuhakikisha makusanyiko wa watu vijijini unakuwa kama zamani kwa kuhakikisha mazingira yanawawezesha vijana kujiajili huko.

Amesema kuwa anatamani Chadema kuchukua jimbo hilo lakini nafsi yake inatamani yeye kuwa mwakilishi wa wakazi wa jimbo hilo bungeni.


Related Posts