BVR yafelisha wanafunzi Njombe


 ZOEZI la uandikishaji Daftari la kudumu la mpiga kura kwa mfumo wa kibaiolojia (BVR) umedaia kufelisha wanafunzi katika mihani wa moka halmashauli ya wilaya ya Njombe baada ya walimu wao kutumiwa katika zoezi hilo.

Hayo yamebainishwa katika baraza la Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Njombe na Madiwani baada ya walimu wa shule za kata zao kutumika katika zoezi la uandikishaji huku shule hizo zikiwa na walimu wachache.

Akichangia taarifa ya elimu ya kukamilisha mwaka uliopita wa fedha hasa katika mtihani wa kujipima uwezo wa darasa la saba (Mock) Diwani wa viti maalum kata ya Mfiliga, Salome Lugala amesema kuwa wanafunzi katika kata yake wamefeli kutokana na walimu wa shule ya msingi Iditima walimu wote kwenda kwenye zoezi la uandikishaji na kuacha shule zao kuwa bila walimu kwa kipindi chote cha uandikishaji.


Amesema kuwa serikali imekuwa ikisema kuwa walimu wanapewa motisha kwa kufanya kazi hilo lakini haiangalii madhara yanayo weza kujitokeza baadae.

Diwani wa kata ya Igogolo Ayubu Mkane amesema kuwa serikali inapashwa kuto tazama motishwa kwa wafanyakazi wa chini pekee itazame na madhara kama hayo na kuwatumia wasomi walioko mitaani kwa kuwapatia fura hizo ili nao kupata pesa kwa kuwachanganya na wafanyakazi wa serikali.


Awali akiwasiliasha taarifa ya elimu afisa elimu shule za msingi halmashauri hiyo Frida Kayava amesema kuwa taarifa ya elimu hiyo ipo katika sehemu tatu na imeeleza sababu za kufeli na mikakati ya huhakikisha elimu inapanda juu.


Aidha Ahmed Maguho kaimu Mkurugenzi amesema kuwa serikali kwa kuona matokeo hayo imeamua kuanza mikutano ya kuwakutanisha wakuu wa shule kwa kuwapa mikakati ya kupandisha elimu katika halmashauri hiyo na kuwa mikutano hiyo imeisha anza katika kata mbalimbali za halmashauri hizo.



Naye kaimu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Shaibu Masasi amesema kuwa halmashauri hiyo isijidai kuwa imejitahidi wakati haina alama ya kujani hata mija katika ufauru kwa kuwa hakuna shule hata moja zote zina langi ya njano kwa ufauru.