CCM Njombe; Tutawakata watakao vunja kanuni


CHAMA cha mapindizi CCM mkoa wa Njombe kimesema kuwa kitakata majina ya wote watakao cheza lafu wakati wa uchukuaji wa fomu za nyadhifa tatu zilizoanza kutolewa julai 15 mwaka huu, nchi nzima kama walivyo fanyiwa viongozi wa ngazi ya kitaifa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani humo katibu wa chama hicho mkoa wa Njombe Hosea Mpagike alisema kuwa fomu hizo zinaaza kutolewa katika ofisi mbalimbali za CCM na kuonya watakao anza kupiga kampeni mapema na watakao vunga taratibu na kanuni.

Mpagike alisema kuwa fomu hizo zitaanza kutolewa Julai 15 mwaka huu na kufikia ukomo Julai 19 ambapo kampeni zitaanza rasim katika maeneo mbalimbali na kutafuta watu watakao waopigia kura huku kukiwa hakuna kipengele cha kutafuta wadhamini kama ilivyo kuwa katika nafasi ya urais.

“Fomu zinaanza kutolewa leo (jana) na kufika ukomo tarehe 19 na kampeni zitaanza rasm julai 20 mpaka julai 31 na uchaguzi ndani ya chama kufanyika Augosti mosi, na zitatolewa katika ofisi za kata kwa udiwani na ubunge katika ofisi za wilaya,” alisema Mpageke.

Alisema kuwa wanachama wanao chukua fomu wawe makini katika suala la kupiga kampeni mapema na kuvunja kanuni za chama majina yao yatakatwa hawato muonea huruma mtu kuwa huli.

“Kwa atakaye piga kampeni mapema na kuvunja kanuni jina lake litakatwa tu hatutakuwa na huruma na mtu kwa sababu katiba ya chama hairuhusu kitendo cha kupiga kampeni kabla ya kuruhusiwa,” alisema Mpagike.

Aidha mpagike alisema kuwa baada ya kupitishwa majina ya wagombea wa Ubunge yatapitishwa na kamati kuu ya CCM NEC ambapo majina yatakayo letwa na chama hicho  yataangaliwa kama watu hao wanakubalika kwao.

Akisoma ratiba ya utoaji wa form Mpagike amesema kuwa fomu za udiwani zitatolewa katika ofisi za makatibu kata wa CCM na kwa ofisi za ubunge zitatolewa katika ofisi za wilaya, na kwa wagombea udiwani nafasi ya viti maalumu zitatolewa katika ofisi ya CCM Wilaya na ubunge viti maalumu zitatolewa katika ofisi ya UWT mkoa.


Related Posts