Wananchi wawafukuza Wawekezaji


WANANCHI wa vijiji vitatu katika kata ya Ramadhani mkoani Njombe wamepinga ujio wa kampeni ya Uchimbaji wa madini katika vijiji vyao ambayo iliitisha mkutano na wananchi hao kwa mara ya kwanza na wanakijiji hao kwa lengo la kuwaomba kutoa maamuzi ya kuwapatia eneo hilo kwaajili ya kufunguliwa mgodi wa Dhahabu.


Hatua hiyo ilikuja  juzi baada ya kampuni ya Noravia Gold iliyoitisha mkutano na wananchi kwa lengo la kuwataarifu juu ya upatikanaji wa madini ya Dhahabu katika vijiji vya Mgodechi, Igagala na Wikichi, ambapo lengo la mkutano huo ikiwa ni kupata maamuzi ya wananchi juu ya kuanza kuchimba madini katika vijiji hivyo.

Katika mkutano huo uliohudhuliwa na wataalamu wa maliasili, ardhi na afisa Maendeleo kutoka halmashauri ya mji Njombe, huku mkutano ukiwa ni wa kuwataka wananchi waseme wanataka wafanyiwe nini na mgodi huo ili wauruhusu kuanza kufanya kazi, wakifishwa madhara baada ya kuanza kuchimbwa madini katika eneo hilo.

Wananchi wa vijiji hivyo walivuruga mkutano huo kwa malengo ya kutaka mkutano wao kwanza kufanyika kabla ya kukutana na wawekezaji hao ambao watatakiwa kuja kukaa na wananchi baada ya mkutano wao kufanyika na kujadiliana wakiwa peke yao.

Walisema kuwa hawajapendezwa na kidendo cha serikali yao kuto pewa taarifa mapema juu ya ujio wa wageni hao wa mgodi huku wakitupiwa lawama ofisi ya Mkurugenzi kuwaruhusu watafiti kufanya utafiti bila wenyeji wa vijiji hivyo kupewa taarifa.

Mmoja wa wakati hao na aliyekuwa Diwani wa kata ya Ramadhani, Alfred Luvanda alisikika akitoa sauti ya kulalamika kwa kupinga kuwapo kwa mkutano huo na kuanza kuwaandikia majina wananchi kabla ya wananchi hawajajua nini malengo ya mkutano.

Alisema kuwa haiwezekani wananchi wakaanza kuandikisha majina katika fomu ambazo hawajapewa maelekezo ya kutosha na bado hawajakubali kutoa eeo hilo na kuwa mgodi wa madini.

Aidha Abubakar Msigwa mjumbe wa serikali ya kijiji cha Mgodechi alisema kuwa haiwezekani wawekezaji hawa wakawa wanaeleza tu juu ya kutoa ajira kwa wakazi wa vijiji hivyo na lakini hawaelezi madhala yatakayo jitokeza baada ya kuanza kuchimba madini.

Alisema kuwa wananchi wa vijiji hivyo wanategemea maeneo hayo kwa kilimo, na maisha yao yote haitawezekana kuwahalibia maeneo wanayo tegemeo kwa kilimo kwa kulipwa fidia inatakiwa wawekezaji waje na sela itakayo wawezesha wanakijiji kuwa na maisha bora kwa maisha yao yote rasivyo haiwezekani.

“Wananchi wa vijiji hivi vitatu wataenda wapi wakati shughuli za migodi zinaendelea kwa kuwa tumeshuhudia maeneo mbalimbali kukutoea migogolo kama Mtwala ni kutokana na kuto kuw na kauli nzuri zinazo wawezesha wakazi kunufaika licha ya serikali kunufaiki,” alisema Msigwa na kuongeza

“Napenda nchi yangu kupiga hauta ya Maendeleo lakini haiwezekani kujengwa barabara na wananchi kufa basi nani atakaye furahia Maendeleo hayo kwa kuwa kunanchi kunatokea vita kutokana na mali zinazochimbwa arhini na wananchi kuto nufaika,” aliongeza

Mkutano huo baina ya Noravia na wanavijiji hao ulivinjika huku watendaji kutoka halmashauri ya mji Njombe wakisema kuwa wanakubaliana na kauli za wananchi ya kusuburi wananchi waitishe mikutano yao ili wamewe kukubaliana wao wenyewe ndipo wawaite wawekezaji.

Ernest Ngaponda afisa kilimo halmashauri ya mji alisema kuwa yeye anawaongoza wananchi katika kilimo hawezi kukubali kirahisi wananchi kuhalibiuwa mazingira yao ya kilimi eti kwasababu ya Uchimbaji wa madini na kuwataka wananchi kukaakatika mikutano yao kujadili madhara na faida endelevu kwa wakazi wa eneo hilo.

Awali wakijitambulika wawekezaji hao kutoka kampuni ya Noravia walisema kuwa wamekuja kwaajili ya kutaka kupata maoni ya wananchi juu ya nini wawafanyie watakapo anza kuchimba madini na kuwaeleza kuwa wamefanya utafiti wa madini katika vijiji hivyo na kubaini mkuwa kuna madini.

Mwanaseria wa serikali aliyekuja chini ya kampuni hiyo ya madini George Stevin alisema kuwa mkutsno ho ulikuwa kwaajili ya kutoa maamuzi juu ya mgodi wa madini na kusema kuwa kampuni hiyo ipo katika vijiji hivyo tangu mwaka 2013 mwaka huu huku ikifanya utafiti na kugundua kuna madini mengi chini ya ardhi na madini yenye thamani ni dhahabu.
Alisema kuwa Noravia iliomba fulsa ya kupata maoni na ruhusa ya kupata nafasi ya kuchima madini ambapo kupitia mkutano huo wananchi wangeipa nafasi kampuni hiyo kupata kibali cha Uchimbaji wa madini na mpaka mwisho wa mkutano wananchi wataka kupewa muda wa kufanyamaamuzi.

Related Posts