MBUNGE AJAYE AFUNGUE OFISI


WAKAZI wa mkoa wa Njombe wamesema kuwa wanataka mbunge atakaye kuwa na ofisi Mkoani humo ili kupeleka matatizo yao wanapo kuwa na tatizo linalo mhusu mbunge.


Wito huo umetolewa na wakazi wa mkoa wa Njombe wakati Wabunge wakiendele na zoezi la kuchukua fomu nchini kote kwa lengo la kuwa na ofisi ya kufikisha mawazo yao, matatizo na kelo zao katika kila jimbo.

 Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa mkoa wa Njombe wamesema kuwa hawajawahi hubahatika kuwa na ofisi ya mbunge ambako wangefika kuto shida zao hatakama mbunge hayupo kutoa kwa katibu wa mbunge.

Mmoja wa kakazi wa mkoa wa Njombe, Enock Mwangongolwa alisema kuwa wanataka mbunge atakaye kuja aweke ofisi ya mbunge ambako  wananchi watawasilisha matatizo yao katika ofisi yao ya mbunge.

Mwangongolwa alisema kuwa wananchi wa mkoa wa Njombe wakekuwa wakishindwa kutoa matatizo yao kwa mbunge kwa kuwa hakukuwahi kuwa na ofisi ya mbunge.

Aidha Erick Sanga alisema kuwa amezunguka mikoa mingi hapa nchini ameona ofisi ya mbunge lakini katika mkoa wa Njombe hajaona ofisi ya mbunge hivyo anamba mbunge atakaye pita kwa chama chochote awe na ofisi ya mbunge ili wananchi wawe na ofisi yao ya kuwasilisha matatizo yao.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuchukua fomu ya ubunge wa jimbo la Njombe Kusini chama cha Mapinduzi CCM, Joseph Msemwa (Pichani mwenye kijani) alisema kuwa kitu cha kwanza akifanikiwa kuwa mbunge atahakikisha kuwa atakuwa na ofisi Mkoani Njombe ili kupokea matatizo ya wananchi.

Alisema kuwa atahakikisha kuwa atahakikisha kuwa yeye akiwa bungeni watu wanapata huduma katika ofisi ya mbunge na kuwa ofisi ya mbunge haiwi katika ofisi ya chama na kuwa ina wanyima uhuru Wananchi wa kupata huduma stahiki.

Alisema kuwa hatapendezewa na kutokuwapo kwa ofisi ya mbunge na atashawishi halmashauri kutoa kiwanja kwaajili ya ofisi ya mbunge.
Aliongeza kuwa atahakikisha kuwa anasimamia haki za wananchi hasa za kufanya pesa za jimbo kufanya kazi ya Maendeleo ya miundombinu ya barabara kwa lengo la kupandisha thamani ya madhao ya wananchi.

Akitoa taarifa kwa mwenyekiti wa CCM mkoa, Deo Sanga waliochukuo fomu kwa majimbo matatu ya wilaya ya Njombe mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo Sadakati Kimati alisema kuwa mpaka kufiukia julai 17 mwishoni mwa wiki iliyopita kulikuwa na watu 18 huku jimbo la Makambako la mwenyekiti wa, mkoa likiwa na wagombea wawili wkiwemo na mwenyekiti mwenyewe.

Alisema kuwa kwa wilaya yake kuna watu wengi walio hamasika kujitokeza kuchukua fomu za kuwania uongozi kwa kuwa wamejipina na kuona wanatosha kuwaongoza wananjombe tofauti na mika ya nyuma ambapo kulikuwa na watu wachache wakijitokeza.

Aidha Kimati alitoa onyo kwa wagombea kutoa anza kuchapisha mabango, Karenda na vipeperusi mpaka watakapo ruhusiwa kuanza kampeni na kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha kanuni za chama hicho.


Related Posts