TAASISI ZA UMA LIPENI ANKALA ILI MAMLAKA ZA MAJI ZIFANYEKAZI KWA UFANISI


TAASISI za umma nchini zimetakiwa kulipa ankala za maji ili kuziwezasha mamlaka za maji kutoa huduma nzuri za maji na kuhudumia watu wengi kwa pamoja.
Akizungumza katika kilele cha maji Mkoani Mbeya Afisa wa maji Bonde la Mto Rufiji, Idrisa Msuya ambaye alikuwa mgeni rasimi katika hafla fupi ya kilele hicho alisema kuwa taasisi za uma zimekuwa zikisita kulipa Ankara za maji na kujilimbikizia madeni.
Msuya alisema kuwa mamlaka za maji nchini zimekuwa zikishindwa kutekeleza majukumuyake kwa weledi kutokana na taasisi hizo kuto lipa Ankara za maji kwa wakati na kusababisha changamito kuto kwamuliwa katika mamlaka ya maji.
Alisema hiyo ni changamoto inayo zikabili mamlaka nyingi za maji hapa nchini na kuwa huenda serikali haiweki bajeti ya maji kwa taasisi hizo ama kumekuwa na matumizi mabaya ya fedha zinazotengwa kwaajili ya maji.
Msuya pia aliwataka wananchi kutunza vyanzo vya maji ili maji kuendelea kuwapo wakati wote hapa nchini bila kupungua hata kipindio cha mvua zitakapo katika.
Nae Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya Maji Mkoani Mbeya Mhandisi Simon Shauri alisema kuwa kutokana taasisi za Uma kuto lipa Ankara zao na kuwa na madeni makubwa wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali za kuboresha huduma za maji.
“Taasisi za umma zimekuwa na madeni makubwa ambayo mpaka sasa mamlaka ya maji inazidai na hazija lipa kitu kinacho tupa sisi kama mamlaka katika ufanyaji wa kazi,” Alisema Shauri.
Alisema mbali na changamoto hiyo mamlaka imekuwa ikifanya juhudi za kuhakikisha wananchi wa jijini Mbeya wanapata maji kwa masaa kati ya 15 na 24 kwa maeneo yote ja jiji la Mbeya.
Alisema mamlaka ya maji imekuwa ikifanya ulinzi shirikishi katika vyanzo vya maji kwa kushirikiana na jamii inayo zunguka katika vyanzo vya maji ili kuhakikisha vyanzo vinatunzwa na kupata maji kwa kipindi chote cha mwaka.

Related Posts