KISIMA cha maji chenye
uwezo wa kutoa lita 5000 kwa saa kimekabidhiwa rasm katika Hospitali yenye
uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi kati ya 50 na 60 elfu wan chi mbili za
Tanzania na Zambia.
Kisima hicho
kimekabidhiwa katika Hospitali ya Tunduma wilayani Momba Mkoani Mbeya
Jana na kampuni ya Bia Tanzania TBL baada ya kukamilika.
Akikabidhi kisima
hicho Afisa uhusiano wa kampuni hiyo Doris Malulu (PICHANI) alisema kuwa kampuni yale imekuwa ikifanya shughuli ya
kurudisha faida kwa wananchi kwa kufanya vitu ambavyo vita wasaidia wananchi
kwa ujumla.
Alisema mradi huo ni
moja kati ya miradi miwili ya visima inayo tekelezwa na kampuni hiyo
Mkoani Mbeya huku mwingine ukitekelezwa wilayani Ileje Mkoani hapa.
Malulu alisema kuwa mradi huo mpaka kukamilika kwake
umeghalimu jumla ya shilingi milion24 na kuwa utaweza kutoa lita 5,000 za maji
kwa saa na kumaliza tatizo la maji katika Hospitali ya Tunduma wilayani Momba
Mkoani Mbeya.
Kwa upande wake Afisa
mipango miji wa mamlaka ya Mji mdogo wa Tunduma, Augustino Ngetwa alisema kuwa
mradi huo utamaliza tatizo la maji katika kituo hicho kinacho hudumia watu
wengi kwa mwaka na watu wanje ya nchi.
Alisema kuwa mbali ya
kukamilika kwa mradi huo wa maji Hospitali hiyo inakabiliwa na uchakavu wa
mabomba ya kusambaza maji katika vimba mbalimbali vya Hospitali kutokana na
kuto tumika kwa muda mrefu sasa.
Naye Mgeni rasm aliye
muwakilisha mkuu wa wilaya katika shuguli hiyo ya upokeaji wa kisima hicho
Mkurugenzi wa mamlaka ya mji Mdogo wa Tunduma, Aidan Mwashinga, alisema kuwa
mamlaka hiyo itatunza maji hayo na kuwa maji yatakayo baki yatasambazwa kwa
wananchi.
Alisema kuwa mradi huo
utatoa huduma mzuri katika nchi zote mbili na kuwa wananchi waishio mpakani
kutoka mchini Zambia watakimbilia katika Hospitali hiyo na kuwa wataisifu kuwa
hospitali ya Tundima Tanzania inatoa huduma nzuri na kukuza uchumi wa wananchi
jirani kwa kufanya biashara kwa wananchi wa maeneo karibu na hospitali.
Alisema kuwa kutokana
na maji kuwa adimu katika halmashauri hiyo wata lina mradi huo na kuhakikisha
wananufaika na maji hayo yaliyo letwa na kampuni ya TBL.
Naye diwani wa Kata ya
Tunduma, Frank Mwakajoka, aliwataka wahudumu katika Hospitali hiyo kuilina
miundombinu ya maji ili idumu na kutumika kwa kizazi hadi kizazi katika mji huo
na kuwa haitakuwa vizuri kama mradi huo utaharibiwa mapema.