Merkel aliyasema hayo siku moja baada ya kuanza muhula wake wa tatu kama kansela wa taifa kubwa kiuchumi barani Ulaya, kabla ya kuelekea Paris kwa mazungumzo na Rais Francois Hollande. Baadae atakwenda Brussels kuhudhuria mkutano wa kilele wa siku mbili wa Umoja wa Ulaya unaoanza kesho.
Bibi Merkel ameliambia bunge la Ujerumani kuwa Umoja wa Ulaya unahitaji kufanya kazi kwa kuzingatia uongozi wa pamoja wa kifedha na kiuchumi, ambapo wanachama wanaweza kushurutishwa kutimiza malengo kadhaa ya bajeti, hata kama kutahitajika mabadiliko katika mikataba muhimu ya Umoja huo.

Na DW.DE