MAMILIONI YAZUIWA KUIBIWA NA TAKUKURI NJOMBE





ZAIDI ya milioni 10.8 zimeokolewa na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) mkoani Njombe, kwa mwaka huu katika taasisi mbalimbali kwenye miradi ya maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa Takukuru mkoa wa Njombe Charles Nakembetwa alisema kuwa taasisi hiyo imefanikiwa kuziokoma pesa hizo zikiwa katika hatari ya kuchomolewa katika miradi ya kimaendeleo katika taasisi mbalimbali za serikali.

Nakembetwa alisema kuwa taasisi hiyo imeziokoa jumla ya shilingi 10,864,000 ambapo takukurui walipata taarifa kutoka kwa watu na kuzifanyia kazi na kuzuia kutolewa kama rushwa katika miradi ya kimaendeleo mkoani hapo.

Alisema kuwa Takukuru kwa sasa imekuwa ikitumia mfumo wa kuhakikisha wanazuia rushwa kabla ya kutokea na pesa kutumia vibaya kitu kinachookoa pesa, kuliko kusubili rushwa itolewa na kumkamata mtuhumiwa ambapo akikamatwa uwezekano wa kupatikana kwa pesa hizo unakuwa ni mgumu.

Alisema udhibiti huo wa mianya ya kutoa rushwa kuna saidia kuokoa pesa za serikali kutumika vibaya kutokana na kutoa ama kupokea Rushwa wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya serikali.

Nakembetwa alisema kuwa kwa mkoa wa Njombe kwa sasa kuna kesi 28 ambazi zipo mahakamani na kuwa kwa mwaka huu wamefungua kesi 5 na kuwa kuna kesi ambazo zinatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.

Related Posts