WAZEE WAHAKIKIWA MBEYA


SERIKALI kote nchini imeamua kufanya zoezi la kuwahakiki wastaafu wote walioitumikia serikali waki hii ili ili kupata takwimuhalisi ya watu waliopo baada ya wengine kufariki dunia.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa hazina ndogo mkoani Mbeya Stanford Siwale jana jijini Mbeya wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na kazi ya uhakiki wa wastaafu hao inayo endelea mkoani Mbeya.

Siwale alisema kuwa kutokana na ratiba iliyo tolewa na Wizara ya Fedha jijini Dar es salaam zoezi hilo lilianza Machi 3 na kumalkizaka Machi 14 mwaka huu.

 Alisema kuwa idadi ya siku za usahili kwa halmashauri itategemeana na wingi wastaafu waliopo katika halmashauri husika na kuwa katika halmashauri ya Mbarali uhakiki ulifanyika kwa siku moja ambayo ina wastaafu 11 pekee kuwa zoezi litafanyka kwa siku moja tu.
“Mfano katika halmashauri ya wilaya ya Chunya kuna wastaafu wanaoishi katika maeneo ya vijiji kama vile Kambikatoto, Namkukwe na Bitimanyanga, ambavyo vipo  yapata zaidi ya kilomita 200 kutoka makao makuu ya wilaya ya chunya,” alisema Siwale

Siwale aliongeza kuwa hatakama utaratibu huo ungepangwa mapema lakini bado zoezi hilo linge chelewa, kwa sababu wengi wa wastaafu sio waajiliwa hivyo kuwapata inakuwa vigumu.
Kwa upande wao wastaafu walisema kuwa nia ya serikali ya kufanya uhakiki kwa watu wanao ishi sio mbaya, kwa sababu inataka isiwe inatoa mafungu kwa watu ambao ni wafu.
Kauli hiyo ilitolewa na mzee Maclean Mwangomale ambaye ni mkazi wa Forest Jijini Mbeya, na kuongeza kuwa mpango wa kuwaita wazee kwenye uhakiki haukuandaliwa vizuri kwani umejaa usumbufu.
Mzee Alford Kasule Mkazi wa Nzovwe, alisema kuwa zoezi hilo sio baya ila utaratibu unaotumika si mzuri, kwa sababu ofisi inayo toa huduma ambayo ni ya jiji ni moja hali inayo sababisha washinde kwenye foleni kutwa nzima.
Naye Oswald Malofwa wa Nzovwe ameiomba serikali inapo andaa program ya namna hii iwe inawaandalia na alawansi ya posho, kutokana na matatizo wanayo yapata wakati Sajenti mstaafu Duncan Mponda naye amelalamikia kiwango wanachopewa  kuwa ni kidogo kutokana na ugumu wa maisha.
Mstaafu mwanamke Nabwike Mwasumbwe m kazi wa mkazi wa Mwanjelwa ameiomba serikali itafakali sana juu ya utendaji wake kwa wastaafu, ambao wamedai waliitumikia serikali yao kwa utiifu mkubwa lakini leo hii serikali haiwathamini.
Wastaafu wengine wamesema kuwa pesa wanayolipwa kwa sasa na serikali ya shilingi 150,000/= kama mafao yaani shilingi 50,000/= kwa mwezi, haitoshi kabi sa ukizingatia ugumu wa maisha. 

Related Posts