Watu wengine 18 wamejeruhiwa kufuatia mripuko uliotokea katika Rawalpindi mita chache kutoka makao makuu ya jeshi.
Mashambulio hayo mawili yaliyotokea ndani ya kipindi cha saa 24 yamedhihirisha kuongezeka kwa ghasia zinazofanywa na kundi la Tehreel e Taliban TTP baada ya kipindi cha utulivu kidogo kufuatia kuuwawa kwa kiongozi wake Hakimullah Mehsud aliyeuwawa katika shambulio la ndege isiyokuwa na rubani lililofanywa na Marekani mwezi Novemba.
Kwa mujibu wa taarifa ya afisa wa ngazi ya juu wa polisi Haroon Joya waliouwawa kwenye mripuko wa leo ni pamoja na wanajeshi sita na raia saba.
Dw.deSwahili