AJUZA AUWAWA KWA PANGA MBEYA



MTU anayedaiwa kuwa na upungufu wa akili amemjeruhi kwa panga Bibi kizee (80) sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani na kusababisha kifo chake wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Makandana wilayani Rungwe.
Marehemu Daina Kihaba (80) Mkazi wa kijiji cha Syuku Wilayani Rungwe, alivamiwa na mtuhuyo juzi majira ya saa 3:00 Usiku huko katika kijiji cha Syukula kata ya Kyimo wilayani Rungwe na kumjeruhi na panga katika sehemu mbalimbali za mwili.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi alisema kuwa marehemu alivamiwa na Hosea Mwaiswelo anayedaiwa kuwa na upungufu wa akili mkazi wa maeno hayo.
Alisema kuwa Marehemu alijerukiwa kwa kukatwa na panga kichwani na katima mkononi kabla ya kupelekwa hospitalini.
Akisimulia tukio hilo Msangi alisema kuwa marehemu akiwa nanakula ndani kwakwe na mjukuu wake Esta Kitwika (9) mwanafuzi wa darasa la nne walivamiwa ndani na mtuhumiwa huyo.
Alisema mwanafunzi huyo wa shule ya msingi Syukula nae alijeruhiwa na mtuhumiwa huyo na alipatiw amatibabu kisha kuruhusiwa.
Alisema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jehi la polisi na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Msangi aliongeza kuwa chanzo cha tukio hilo kinachunguza na kuitaja jamii ya wakazi wa Mbeya kuwa makini wanapokuw ana watu wenye ugonjwa wa akili na kuwapeleka hospitalini ili kuepukana na madhara kama hayo.

Related Posts