UNYANYASAJI KWA WAALIMU WENYE ULEMAVU UKOME

WALIMU  wenye ulemavu na wanawake wanakabiliwa na changamoto mbali mbali wakiwa makazini kutokana na watu kutowaelewa vizuri na huku wengine wakifanya kwa makusudi vitendo  vya ukatili na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Akizungumza na walimu wanawake na walimu wenye ulemavu mbalimbali Mbunge na Mwenyekiti wa kamati ya mikopo kwa waalimu, Margret Mkanga alisema kuwa walimu hao wanakabiliwa na changamoto hizo katika ufanyaji kazi.
Alisema kuwa walimu wenye ulemavu wajitahidi kufanya kazi kwa makini na juhudi ya hali ya juu ili kuonyesha kuwa wanaweza kufanya kazi kuliko hata walimu wasio na ulemavu wa aina yoyote.
Mkanga alisema yeye alipo kuwa akifundisha alikuwa akifanya kazi kwa bidii na kuhakikisha mwanafuzi anaye mfundisha anafaulu vizuri kitu kilicho kuwa kikimpa furaha na faraja.
Alisema kuwa watu wengi wamekuwa wakiwazarau walimu wenzao wenye ulemavu na kuona wao hawaweza kufundisha vizuri.
 Alisema kuwa waalimu wakubaliane na changamoto hizo kwani zina mwisho wake ambapo zitakome na watakubalika na kila jamii.
Kwa upande wake Mbunge wa viti maalum (CCM) Singida Dayana Kilolo aliwataka walimu kutumia chombo chao cha CWT ili kuhakikisha wanapata maslahi yao.
Alisema alisema kuwa hakuna sababu kwa serikali kunyimwa haki stahili za walimu wakati wanadai.
Alisema kutokana na madai mengi wanayodai serikali,walimu wengi wamevunjika moyo wa kufundisha watoto mashuleni kutokana na muda mwingi kushughulikia madai yao.

Related Posts