Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa anaugua maradhi ya figo na madaktari wamesema wanahofia maisha yake.
Sharon aipatwa na ugonjwa wa kiharusi na kuvuja damu kwenye ubongo mnamo Januari 4 mwaka wa 2006, wakati akiendelea na kampeni za uchaguzi ambao alitarajiwa kushinda.
Alikuwa Waziri Mkuu wa Israel kuanzia mwaka wa 2001 hadi mwaka wa 2006.
Aliunga mkono ujenzi wa makaazi ya walowezi wa kiyahudi katika maeneo ya wapalestina yanayokaliwa na Israel.