Jeshi la Sudan laendelea na juhudi za kuukomboa mji wa Bor
Jeshi la Sudan Kusini la SPLA, leo limesonga mbele katika mji wa Bor,
unaodhibitiwa na waasi, wakati pande hizo mbili zinazohasimiana zikikutana
nchini Ethiopia kwa mazungumzo ya amani yenye lengo la kumaliza
machafuko yaliyodumu wiki tatu na kutishia kuitumbukiza nchi hiyo katika vita
vya wenyewe kwa wenyewe. Pande zote mbili zimekubaliana kimsingi
kuweka chini silaha lakini hakuna upande uliosema wazi ni lini
yatasimamishwa mapigano hayo yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000
na kuwaacha wengine karibu 200,000 bila makaazi. Rais wa Salva Kiir
ametangaza hali ya hatari katika majimbo ya Unity na Jonglei ambayo mji
mkuu Bor ulitekwa mapema wiki hii na waasi wanaomuunga mkono makamu
wa rais aliyefutwa kazi Riek Machar. Nchi jirani zinazosimamia mazungumzo
ya upatanishi baina ya pande zinazozozana zimeonya kuwa kuendelea kwa
mapigano Sudan kusini, kunaweza kuvuruga mazungumzo hayo ya Addis
Ababa.