Showing posts with label Rais Morsi wa Misri. Show all posts
Showing posts with label Rais Morsi wa Misri. Show all posts
Misri yaanda uchaguzi wa bunge

Misri yaanda uchaguzi wa bunge


Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Ayman Abbas, anasema uchaguzi utaanza October 18 na kumalizika baada ya awamu mbili ya siku mbili, hapo November 23.
Rais wa Misri Abdel Fattah el Sissi
Rais wa Misri Abdel Fattah el SissiMisri inapanga kufanya uchaguzi wa bunge ambao umecheleweshwa kwa muda  hapo mwezi October na November mwaka huu. Hiyo ni  zaidi ya miaka mitatu ya bila kuwepo na bunge. Wachambuzi wanasema bunge jipya huwenda likarudisha baadhi ya uaminifu wa kimataifa, lakini hio huwenda lisiweze kusaidia maisha ya watu wa huko Misri.
Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Ayman Abbas, anasema uchaguzi utaanza October 18 na kumalizika baada ya  awamu mbili  ya siku mbili, hapo November 23.
Abbass anaonya wagombea ubunge, dhidi ya kuchochea ghasia, au kujaribu kufanya wizi wa kura.
Bunge hilo jipya litafanya serikali kuonekana kuwa halali zaidi kwa wawekezaji wa kimataifa, anasema Said Sadek mwanasoshologia wa kisiasa. Anasema kukiwa na zaidi ya vyama mia moja vya kisiasa, na kanuni  nyingi mpya, huwenda ikachukuwa muda mrefu kabla kupatikana mafanikio makubwa.
Sadek anasema bunge ni kubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Misri. Lina wabunge 596. Anasema Misri hiajawahi kuwa na bunge kubwa kama hilo.
Kwa sasa, sheria Misri zinapitishwa na rais Abdel Fattah el Sissi, ikiwa ni pamoja na sheria mpya dhidi ya ugaidi iliyopitishwa wiki mbili zilizopita, na ambayo imevutia ukosowaji kutoka kwa makundi ya kutetea haki za binadam, ambayo yanasema, sheria hiyo itatumiwa kuwanyamazisha wapinzani, na vyombo vya habari.
Misri imekuwa bila ya bunge tangu June mwaka 2012, pale bunge lililotawaliwa na kundi la Muslim Brotherhood lilipovunjwa. Uchaguzi unaokuja ulicheleweshwa kutoka March kwa sababu za kiufundi na kisheria.
Hata hivyo baadhi ya wachambuzi wanasema sababu ya kweli kwa uchelewesho huo ni kuwa serikali inaweza kulishinda kundi lililopigwa marufuku la Muslim Brotherhood, na kuhakikisha wafuasi wao hawashindi viti katika bunge jipya.

Kesi ya Mursi kusikilizwa tena Februari 22

Kesi dhidi ya rais wa zamani wa Misri, Mohammed Mursi, na viongozi 21 wa Udugu wa Kiislamu kuhusiana na mashtaka ya kutoroka jela wakati wa mapinduzi ya 2011, imeahirishwa. Mursi na washtakiwa wengine walifikishwa mahakamani leo mjini Cairo, huku rais huyo wa zamani akiwa katika kizuizi kilichojengwa kwa chuma.
Akiwa amevaa mavazi meupe ya mfungwa wa jela Mursi alimkaripia jaji kwa hasira, akimuuuliza niambie wewe ni nani. Jumla ya washtakiwa 129 wanahusika na kesi hiyo. Mbali na wanachama wa Udugu wa kiislamu, wengine ni wapiganaji wa kundi la Wapalestina la Hamas na Hezbollah nchini Lebanon, ambao walikimbia jela wakati wa vuguvugu la siku 18 dhidi ya rais Hosni Mubarak lilipopamba moto 2011
Maadhimisho yapita kwa kishindo Misri

Maadhimisho yapita kwa kishindo Misri

Wafuasi wa jeshi wakiandamana medani ya Tahrir

Waandamanaji kadha wameuwawa katika mapambano yaliyotokea mjini Cairo na miji mengine ya Misri, wakati maandamano ya pande zinazopingana yamefanywa kuadhimisha mwaka wa tatu wa maandamano yaliyompindua Hosni Mubarak.
Mjini Cairo polisi walitumia moshi wa kutoza machozi na kufyatua risasi hewani kuwatawanya wanaharakati walioandamana na waandamanaji Waislamu wanaomuunga mkono rais wa zamani Mohamed Morsi ambaye alitolewa madarakani na jeshi.
Inaarifiwa kuwa bomu lilotegwa kwenye gari liliripuka karibu na kambi ya polisi katika mji wa Suez.
Wafuasi wa serikali piya walikusanyika katika medani ya Tahrir kuadhimisha siku hiyo, wakipiga kelele huku wamebeba picha za mkuu wa jeshi, Jenerali Abdul Fattah al-Sisi.
 Serikali yatoa masharti kwa Chama cha Muslim Brotherhood

Serikali yatoa masharti kwa Chama cha Muslim Brotherhood


Hazem Beblawi
Waziri Mkuu wa Mpito wa Misri ameambia BBC kuwa wafuasi wa chama cha Muslim Brotherhood wanaweza kushiriki Uchaguzi Mkuu ikiwa watalaani ghasia na machafuko.
Hazem Beblawi alisema kuwa kura ya maoni ya mwezi uliopita kuhusu Katiba mpya ilikuwa hatua ya kwanza kurejesha demokrasia na kuwa itafuatwa na Uchaguzi wa urais na ubunge katika kipindi cha miezi sita ijayo.
Lakini vugu vugu la Muslim Brotherhood, ambalo liliorodheshwa kuwa kundi la kigaidi hivi karibuni, limekanusha madai ya kuhusika na ghasia zinazokumba Misri.
Chama hicho cha Muslim Brotherhood, kiliongoza serikali ya kwanza kuwahi kuchaguziliwa kwa njia ya demokrasia nchini Misri, ambayo iliondolewa madarakani miezi sita iliyopita na jeshi.
Kiongozi wake Mohammed Morsi anakabiliwa na mashtaka kadhaa ya kihalifu.

Kategori

Kategori