Showing posts with label June 25. Show all posts
Showing posts with label June 25. Show all posts
Wahamiaji haramu 10 mbaroni,magunia 120 ya mkaa yakamatwa Sengerema

Wahamiaji haramu 10 mbaroni,magunia 120 ya mkaa yakamatwa Sengerema

Operesheni ya kuwasaka watu wanaoharibu Hifadhi ya misitu ya Taifa,ikiwemo kujihusisha na kilimo cha zao
haramu la bangi ndani ya misitu hiyo inayomilikiwa na wakala wa huduma za misitu tanzania ( TSF ) katika
kisiwa cha Meisome wilayani Sengerema mkoani Mwanza,imewezesha kukamata wahamiaji haramu
10,magunia 120 ya mkaa pamoja na kuharibu matanuru matano ya mkaa. 

Operesheni hiyo iliyoendeshwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Sengerema kwa kushirikiana na
ofisi ya wakala wa huduma za misitu wilayani humo,inalenga kunusuru uharibifu wa msitu wa hifadhi wa
Maisome,kubaini na kuteketeza mashamba ya bangi,kilimo,uvunaji haramu wa mazao ya misitu,uvuvi haramu
pamoja na kuwakamata wahamiaji haramu.

Mkuu wa wilaya ya Sengerema Emmanuel Kipole,akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisaba katika
mkutano wa hadhara muda mfupi baada ya mkazi wa kijiji hicho Isack Paschal kukamatwa na magunia 90 ya
mkaa nyumbani kwake, 
huku kikosi kazi hicho kikifanikiwa pia kuteketeza robo heka ya shamba la bangi
lililokuwa linamilikiwa na raia mmoja kutoka nchi jirani ya Burundi,amewataka wananchi kulinda msitu huo na
kupiga vita uvuvi haramu ndani ya Ziwa Victoria.
Operesheni hiyo ambayo ni endelevu halikadhalika imewanasa wavunaji haramu wa mazao ya misitu wapatao
sita, 
msumeno mmoja,nyavu haramu 50 aina ya timba,kokoro moja,tani moja ya samaki wachanga aina ya
sangara ambapo taratibu za kisheria za kuwafikisha mahakamni zimeanza kufanyika. 
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sa8giX
via IFTTT


Kondakta Afariki Dunia Na Wengine 21 Akiwemo Dereva Kujeruhiwa Katika Ajali Ya Basi Songea

Kondakta Afariki Dunia Na Wengine 21 Akiwemo Dereva Kujeruhiwa Katika Ajali Ya Basi Songea

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa kwa ajali ya basi katika maeneo ya Hangangadinda Songea baada ya dereva wa basi la
kampuni ya Superfeo Bw.Ally Ramadhan ally kuendesha gari mkono mmoja na mwingine kuutumia kufanya mawasiliano ya simu huku ajali hiyo
ikiwa imetokea siku moja baada ya gari la kampuni hiyo kupata ajali na kuua mtu mmoja kilomita 5 toka ilipotokea ajali ya kwanza.

 Aliyepoteza maisha katika ajali ya basi hilo aina ya Hiang lililokuwa likitokea mkoani Mbeya kuja Songea ni kondakta wa gari hilo Hassani
Ngonyani aliyechomoka kwenye mlango wa gari hilo baada ya kumshinda dereva na kuingia porini na kudondosha kifaa kimoja kimoja likigonga
miti porini huku majeruhi mmoja akilazwa wodi ya wagonjwa mahututi .
Meneja huduma wa kampuni ya Super Feo bw.Francis Sengo anasema wamesikitishwa na ajali hiyo kwa kuwa imetokea siku moja baada ya
kutokea ajali ya kwanza iliyoua dereva wao Ismail Nyami ambapo watoto wadogo wamenusurika kwenye ajali hiyo kwa miujiza ya mungu.

Mkuu wa wilaya ya Songea Bw.Pololeti Kamando Mgema aliyetembelea Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kuwaona majeruhi ameagiza
madereva kuanza kupimwa kilevi na kupendekeza madereva wanaosababisha ajali kunyang’anywa leseni ambapo dereva aliyesababisha ajali hiyo
Bw.Ally Ramadhani anatibiwa chini ya ulinzi wa polisi ili akimaliza matibabu aweze kufikishwa mahakamani.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sPM9jK
via IFTTT


TAARIFA KUHUSU RUFAA ZA WATUMISHI WALIOKUTWA NA VYETI FEKI

TAARIFA KUHUSU RUFAA ZA WATUMISHI WALIOKUTWA NA VYETI FEKI

Serikali imesema kuwa watumishi wa serikali ambao wamekutwa na vyeti feki na kukata rufaa wakielezea kuwa vyeti vyao ni halali, itajulikana mwezi huu mwishoni ambapo uamuzi kuhusu rufaa zao utatolewa.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk Laurian Ndumbaro alipokuwa akiongea na watumishi wa halmashauri sita za Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani humo.
Kiongozi huyo alisema mchakato wa kuvihakiki unakaribia kumalizika na karibuni uamuzi kuhusu wao utatolewa.
“Tunatarajia hadi kufika Juni 30 mwaka huu, wale wote ambao walikata rufaa baada ya kubainika kuwa na vyeti vya kughushi tutatoa majibu ya rufaa zao, ambazo tulikuwa tukiendelea kuzipitia kwa makini.”
Watumishi hao 9,932 waliokuwa katika orodha aliyokabidhiwa Rais Magufuli walitakiwa kuondoka katika utumishi wa umma baada ya kubainika kuwa na vyeti vya kughushi.
Wale ambao waliona kuwa wameonewa walipewa nafasi ya kukata rufaa ambapo ndio maamuzi ya rufaa zao yatatolewa mwishoni mwa mwezi huu.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2t8Nepn
via IFTTT


TETESI: MTAA WA โ€œVICTOR WANYAMAโ€ DAR WAFUTWA

TETESI: MTAA WA “VICTOR WANYAMA” DAR WAFUTWA

Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam, imeufuta mtaa uliopewa jina la mchezaji wa Kimataifa wa Kenya katika Kata ya Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kamati ya Kata ya Ubungo jana ilimpa mtaa Victor Wanyama ambaye ni nahodha wa timu ya Taifa ya Kenya na kiungo wa Tottenham Hostpurs ya nchini Uingereza ambaye yupo nchini kwa mapumziko.
Taarifa za kufutwa kwa mtaa huo zimeanza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii huku ikiwa imenukuu Kitengo Cha Habari na Uhusiano cha Manispaa ya Ubungo.
Taarifa hiyo inasomeka, “Majina ya mitaa hupendekezwa na kamati za mitaa husika kisha hupelekwa kwenye vikao vya WDC vya Kata halafu maamuzi ya WDC hupelekwa kwa Mkurugenzi kwa ajili ya kuingizwa kwenye kikao Cha kamati ya Fedha na uongozi, Baraza la Madiwani, halafu DCC, RCC na Kisha Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na baadaye kwa Mchapaji mkuu wa serikali na mwisho hutokea kwenye Tangazo la serikali GN.”
Aidha taarifa hiyo ilieleza zaidi kuwa, taratibu za kubadilisha jina la mtaa ndizo hizo hizo.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuthibitisha au kukanusha madai hayo ambayo yamewasikitisha wengi hasa mashabiki wa mpira.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2u39Ww5
via IFTTT


Kategori

Kategori