Showing posts with label Chadema. Show all posts
Showing posts with label Chadema. Show all posts
Mwalongo Mshinde kesi ya kupinga matokeo jimbo la Njombe kusini

Mwalongo Mshinde kesi ya kupinga matokeo jimbo la Njombe kusini


MAHAKAMA kuu kanda ya Iringa imemtangaza Edward Mwalongo Kuwa mbunge wa jimbo la Njombe kusini katika kesi iliyo kuwa ikimkabili ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyo funguliwa na aliye kuwa mgombea ubunge kupitia Chadema Emmanuel Masonga.

Akisoma hukumu hiyo ya kesi namba 5 ya uchakuzi mwaka 2015 jaji wa mahakama hiyo Jaji Jacob Mwambegele alisema kuwa baada ya kupitia ushahidi ulio tolewa mahakamani hapo unaonyesha kuwa mlalamikaji hakupeleka malalamiko yake katika kamati ya ya maadili ya uchaguzi ya jimbo.

Alisema kuwa mahakama yake haiwezi kutengua ushindi uliomtangaza mbunge wa jimbo la Njombe Kusini kwa kuwa mdai hakupeleka malalamiko yake katika kamati ya maadili kama sheria inavyo sema.

Jaji Mwambegele alisema kuwa licha ya mahakama yake kubaini kuwapo kwa kampeni zilizo kuwa zemekiuka misingi ya kimaadili na kuendeshwa kwa udhalilishaji lakini mlalamikaji hakufuata sheria ya uchaguzi.

Alisema kuwa kigezo cha kuto peleka malalamiko katika kamati ya maadili Masonga inamnyima haki ya kupinga matokeo hayo kwa kuwa kamati ya maadili ilikuwepo na kuunyima ushahidi wake nguvu ya kushinda.

Jaji Mwambegele alisema kuwa uchaguzi huo uliendeshwa kwa uhuru na haki na kuwa hawezi kumtegua mshinde aliye shinda katika uchaguzi huo.

Kesi hiyo ilisikilizwa mashahidhi zaidi ya 30 kutoka pande zote za walalamikaji na washitakiwa na kusikilizwa kwa zaidi ya miezi 3 huku baadhi ya wiki kuendeshwa mfurulizo bila kupumzika na kufanya kesi hiyo kuisha haraka.

Katika ukumbi wa mahakama wafuasi wa Chadema walionekana kuwa wengi kuliko wale wa Chama cha mapinduzi CCM ambao walifika kusikiliza hukumu hiyo.

Aidha mbunge Mwalongo alitoa shukrani zake kwa mahakama Kuu kwa kumtangaza mshinda katika kesi hiyo ya kupinga matokeo.


Octoba 25 mwaka huu kulifanyika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani ulimtangaza Edward Mwalongo kuwa mshindi wa kiti cha ubunge katika jimbo la Njombe Kusini ambako kulikuwa na wagombea wane ambao walisimamishw ana Vyamba vya CCM, Edward Mwalongo kura 27285, Chadema Emmanuel Masonga kura 23003, Act Wazalendo Emilian Msingwa kura 3888 na DP William Myegeta. kura 94 katika kata zake 13
CHADEMA KUELEKEA iKULU WAPIGWA MKWALA

CHADEMA KUELEKEA iKULU WAPIGWA MKWALA


Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limepiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanyika hapo kesho na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuelekea Ikulu jijini Dar es salaam kushinikiza kurejeshwa ka matangazo ya moja kwa moja ya Bunge.
Akizungumza leo jijini Dar es salaam, Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Naibu Kamishna wa Polisi Simon Siro amesema Chama hicho kinatakiwa kutumia mbinu nyigine ya kushinikiza kurejeshwa kwa matangazo hayo ya Televisheni ya Taifa na sio kupitia maandano.

Katika hatua nyingine jeshi hilo limesitisha kazi za vikundi vya ulinzi shirikishi katika kituo cha kati kutokana na kufanyika kwa vitendo vyenye harufu ya rushwa, kutofuata sheria za ukamataji pamoja na kutumia nguvu kupita kiasi huku Naibu Kamishna Siro akianisha kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kukamata wanaokiuka taratibu.

HII NDO KAULI YA ZITO KABWE MALA BAADA YA HALIMA MDEE KUTEULIWA KUWA Waziri Kivuli Fedha na Mipango



VIONE VITU LIVILYO MTIA WASIWASI MSAMBICHAKA MGOMBEA UBUNGE LUDEWA WA CHADEMA

MGOMBEA wa ubunge jimbo la Ludewa kupitia Chadema anawasiwasi wa matokeo yaliyotangazwa kutokana na sababu mbili alizo zitaja kuwa huenda lilipunguza kura na kufanya uchaguzi kuwa sio wa huru.

Mgombea huyo Batromayo Msambichaka alisema kuwa sababu ambazo zinamfanya kuwa na wasiwasi na matokeo ni pamoja na baadhi ya mawakala walio wateua kukataliwa na vuruguzilizo tokea usiku wa kuamukia uchaguzi.

Msambichaka ambaye kura zake hazikutosha katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Ludewa, kwa kupata kura 7,956 dhidi ya mbunge mteulia wa CCM Deo Ngalawa aliye pata kura 23861 na kutangazwa mshindi.

Alisema kuwa wakati wa kupelewa mawakala kwa msimamizi wa uchaguzi baadhi yao walikataliwa kushiriki kusimamia uchaguzi huo hiyo anasema kuwa ni moja ya sababu ambayo huenda imempunguzia kura katika uchaguzi huo.

Alisema kuwa “Tulipeleka mawakala kwa msimamizi wa uchaguzi ili awathibitishe kuwa mawakala wangu katika uchaguzi huo lakini walikataliwa kwa kigezo walikuwa wametoka mbali wakati hao ndio chama kiliwasimamisha,”

Alisemam kuwa mbali na kuwapo kwa pingamizi la mawakala wa chama  hicho katika uchaguzi pia chama hicho siku moja kabla ya uchaguzi wafuasi wake walipigwa na wafuasi wanao daiwa kuwa ni wa chama cha mapinduzi.

“Usiku wa kuamukia siku ya uchaguzi wanachama wangu walivamiwa na wanachama wa CCM na kupigwa vibaya na kulazwa katika Hospitali ya misheni ya Lugalawa hii nayo ni sababu inayo sema kuwa uchaguzi huu siku lidhika nao,” alisema Msambichaka.

Msambichaka alisema kuwa vijana watatu wauasi wa Chadema walivamiwa na Wauasi wa CCM na kusema kuwa wauasi saba wa CCM walishikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na tukio hilo.

Kushusi kukubari ama kukataa matokeo alisema kua anashauriana na wiongozi wa chama hicho na atatoa maamuzi ya kukubali ama kukataa matokeo.

Hata hivyo Kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe Wilbrod Mutafungwa alithibitisha kuwakamata watu saba wanao daiwa kuwa ni wafuasi wa CCM siku ya Jumapili kuhusisha na tukio usiku wa kuamkia siku ya kupiga kura.

Kuhusiana na kuzuiwa kwa mawakala wa chama hicho msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Ludewa, William Waziri alisema kuwa wakala wa anatakiwa kutoka katika eneo la jimbo la uchaguzi na sio nje ya jimbo hilo suala hilo lipo kisheria.
Msambichaga Bathromeo wa Chadema alikuwa mgombea wa Ubunge jimbo la Ludewa
CCM SABA MBARONI KWA KUGAWA DOZI CHADEMA

CCM SABA MBARONI KWA KUGAWA DOZI CHADEMA

WAFUASI watatu wa chama cha deomokrasia na Maendeleo Chadema Jimbo la Ludewa wameshambuliwa na watu wanao daiwa kuwa ni wafusai wa chama cha Mapinduzi CCM na jeshi la polisi lina washikiria wafuasi saba kuhusiana na tukio hilo lililotokea usiku wa kuamukia siku ya uchaguzi.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Wilbrod MUtafungwa kusibitisha tukio hilo alisema kuwa jeshi hilo jana liliwakamata na kuwashikili wafuasi saba wa CCM kwa tuhuma za kuhusika na tukio la kuwashambulia wafuasi wa Chadema wilayani Ludewa ambako kumefanyika uchaguzi kumpata mbunge wa jimbo hilo jana.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya jioni katika maeneo ya Lugalawa ambapo haikuwa muda wa kampeni ambapo vijana wanao daiwa ni wafuasi CCM wakiwa kwenye gari yao ambapo vijana wa Chadema walikuwa wanawahoji ni kwanini wapo maeneo hayo wakati muda wa kampeni umepita ndipo walianza kuwashambulia.

"Kwa uchunguzi ambao tumeufanya vijana saba tunao washikili wa CCM walikuwa kwenye gari yao maeneo ya Lugalawa majira ya jioni na muda wa kampeni ulikuwaumeisha walianza kuulizwa na vijana wa Chadema wameenda kufanya nini maeneo hayo ndipo wakaanza kupigwa vijana hao, vijana hao wapo kituo cha polisi wilayani Ludewa kwa kosa la kushambulia Mwili na kudhuru" alisema Mutafungwa.

Alisema kuwa vijana walio jeruhiwa ni vijana watatu wa Chadema huku wawili tayari wameruhusiwa na mmoja bado yopo katika hospitali ya Lugalawa ambaye amejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwa ni pamoja na kichwani na vitu vyenye ncha kali.

Hata hivyo makamu mwenyekiti wa Bavicha taifa, Patric Ole Sosopi anasema kuwa vijana hao walijeruhiwa vibaya na kuwa ni kweli ni wafuasi wa chama hicho.

Alisema kuwa watu walioumizwa ni watano na kuwa wawili wamelazwa hospitali ya Lugalawa na kuwa mmoja alipo pigwa na wafuasi wa CCM waliamua kumpeleka wao wenyewe katika kituo cha polisi ambapo kijana huyo alipigwa maeneo ya mlangani na kuwa baada ya matukio hayo pia vijana hao walipita katika maeneo la Mawengi, Mlangali na kupiga wafuasi  chama hicho.

Alisema kuwa vijana hao wa CCM walikuwa na gari yenyi namba ya usajili T 155 CKS  na kuwa waliikamata gari hiyo na kuipileka katika kituo cha polisi.

Hata hivyo CCM wamekili kukamatwa kwa vijana wao ambao mpaka kufiki majira ya saa 9:00 Mchana walikuwa mado wanashikiliwa na jeshi hilo.

Akizungumzia kukamatwa kwa vijana wao katibu wa CCM wilaya ya Ludewa, Lusiana Mbosa, kulitokea mapambano kati ya vijana wao na vijana wa Chadema wakati mgombea  ubunge akiingia katika eneo la Lugalawa ambapo vijana wa ulinzi wa CCM Greenguard walikuwa dolia maeneo ya Lugalawa.

Alisema kuwa walipo kutana vijana walio kuwa wakimlinda mgombea wa Chadema, Bathromeo Msambishaka, wakaanza mapambano ambapo ilibainika kuwa kuna hujuma ambazo zilitaka kufanyika katika maeneo hayo ya kijiji cha Lugalawa.

 Alisema kuwa vijana hao wakati wakipambana ni vijana wa Greenguad na Redbriguad ambapo vijana wa CCM walibaini kuwa mbunge anataka kufanya hujuma za uchaguzi ambao ulitakiw akufanyika jana.

Hata hivyo mgombea ubunge anaye tuhumiwa kutaka kufanya hujuma na Mwenyekiti wa CCM, amesema kuwa gali ya CCM aina ya Hadtop ilifika katika eneo la Lugalawa ambapo walikuwepo baada ya kumaliza kampeni zao walianza kuvamiw ana vijana wa CCM walio toka katika gari hiyo kabla ya kuwateka watu wawili wa Chadema.

Msambichaka ameongeza kuwa walipowakamata walianza kuwapiga na kuwa meneja kampeni wake naye alikamatwa na kuwa kuna watu walipigwa vichwani na vitu kama chuma  na kuwa mtu mmoja alipigwa mpaka alidondoka chini.

Hata hivyo Msambishaka alitaja majina ya walio jeruhiwa kuwa ni Focas Mtitu ambaye alipigwa kichwani na kujeruhiuwa vibaya na Seba, alitibiwa na kuruhusiwa, Geogina alipigwa na kukimbi huku siku ya jana jioni kurejea, na mmoja aitwae Lenard mpaka sasa hajulikani aliko na kuwa msichana mmoja alibakwa katika tukio hilo baada ya kupigwa.

SUGU 'MADIWANI FANYENI KAZI KWA KASI YA MAGUFULI'

Sugu Akiteta Jambo
Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu amewataka madiwani wa jimbo hilo waliochaguliwa kwa tiketi ya Chadema kuhakikisha wanafanya kazi kubwa kushindana na kazi ya rais John Magufuli.

Sugu alitoa kauli hiyo hivi karibuni katika kikao cha kumchagua diwani atakayewania nafasi ya Umeya kwa tiketi ya chama hicho.

Aliwataka madiwani hao kuchapa kazi na kuwafanya wananchi kujivunia kasi ya maendeleo inayoletwa na Mbunge na Meya wa jiji hilo ili wasitamani jimbo hilo lingeongozwa na wapinzani wao wa CCM.

“Hata CCM wenyewe wamebadilika, Magufuli anakwenda jalamba. Hakutakuwa na vitu kama ambavyo mnaviwaza, tunaenda kufanya kazi za wananchi ili wananchi wasitamani kwamba afadhali na hapa pangekuwa CCM. Waseme hata kama Magufuli anaenda spidi na sisi Mbeya yetu Meya na Mbunge wanakwenda spidi.”

Kategori

Kategori