MTOTO Atunukiwa Zawadi ya Kusafiri Kwa Ndege Maisha yake yote

Shirika la ndege la binafsi nchini India limemtunuku safari za bure mtoto aliyezaliwa ndani ya ndege moja ya shirika hilo iliyokuwa safarini kutoka Saudi Arabia kuelekea India.
Mhudumu mmoja wa ndege, ambaye alikuwa amepata mafunzo ya uuguzi alimsaidia mama kujifungua mtoto wakati ndege hiyo ikiwa umbali wa futi 35,000 angani.
Kutokana na tukio hilo, shirika hilo lilimpa zawadi ya kudumu maishani, ambayo itakuwa ni kusafiri bure kwa ndege ya shirika hilo katika maisha yake yote.
Mama na mtoto wake walipelekwa hospitalini baada ya ndege hiyo aina ya Boeng 737 kutua katika mji wa magharibi ya Mumbai.
Shirika hilo liliiambia BBC kuwa mama na mtoto wake walikuwa katika afya nzuri.
Kampuni iliwashukuru wahudumu kwa kumsadia mama kujifungua salama.
Shirika hilo lilisema kuwa hiyo ni mara ya kwanza mtoto kuzaliwa kwenye ndege zake.
Tukio kama hilo lilitokea nchini Uturuki ambapo mtoto wa kike alizaliwa katika ndege ya Shirika la Turkey Airline, Aprili mwaka huu.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2t91HSR
via IFTTT