Jinsi ya Kumtambua Anayekupigia Kwenye Simu yako Kwa Jina na Mahali Alipo

Leo nitakuonesha hatua ambazo zitakusaidia wewe kumfahamu nani anayekupigia kwenye simu yako na wapi anapotokea. Utaweza kufahamu kama simu hiyo inatoka kwenye kampuni au ni watu wanaosumbua. Nimeandalia njia mbili ambazo zitakusaidia kufuatilia namba ya simu kwa jina na mahala inapotokea.
Namba ngeni na binafsi ni moja kati ya vitu vinavyotisha katika maisha yetu ya kila siku unakutana na namba binafsi ambayo siyo ya kawaida tofauti kabisa na tulizozizoea.
Namba nyingi ambazo zinakuwa tofauti mara nyingi hutoka kwa makampuni ya kutafuta masoko kwa njia ya simu ili kutangaza bidhaa au huduma za wateja wao mbali mbali ambazo unaweza ukazipenda au usizipende. au namba ya mtu ambaye haipo katika simu.
Zifuatazo ni njia ambazo zinatumika kutambua namba ya simu ambayo imeingia kwenye simu yako ambapo utaweza kutambua jina na mahala alipo mtu anayekupigia.
Kutumia tovuti ya Truecaller
Hatua ya 1. Fungua tovuti ya Truecaller kwenye pc.
Tovuti ya Truecaller
Hatua ya 2. Chagua nchi ambayo unatokea kwenye orodha kama unatokea Tanzania chagua hapo kisha andika namba ya simu ya mtu ambaye unataka kumfahamu halafu bonyeza search.
tovuti ya Truecaller
Hatua ya 3. Kitatokea kiboksi ambacho kinakutaka ujiunge na true caller ili kuweza kupata taarifa za namba uliyo andika. Kama una account ya Gmail unaweza ukaitumia, au unaweza ukajiunganisha nao kwa kupitia account yako ya facebook kwa urahisi zaidi chagua kisha endelea.
Chagua njia za kujisajili ili kupata matokeo unayotafuta
Baada ya kumaliza usajili utapewa taarifa zote za namba uliyoandika ikiwa ni jina pamoja na mahali alipo. Taarifa hizo zinakuwa ni kweli kwa 90%.
Truecaller itakuletea taarifa za namba ya mhusika kama jina na mahala alipo
Hiyo ndiyo ilikuwa njia rahisi ya kufahamu namba ngeni kwa kutumia tovuti ya True caller. Nadhani kuanzia sasa hakuna namba ngeni mpya tena shikamoo Truecaller.
Kutumia App ya Truecaller kwenye simu yako
Unachotakiwa kufanya fungua playstore kisha pakua app ya Truecaller halafu install kwenye simu yako.
Hatua ya 1. Pakua app ya Truecaller moja kwa moja kwenye simu yako kwa kubonyeza hapa hiyo link inayofuata >> Truecaller pakua hapa
Hatua ya 2. Baada ya kupakua Truecaller kwenye playstore fanya installation ya app hiyo kwenye simu yako kisha ifungue.
Muonekano wa app ya Truecaller
Hatua ya 3. Utaona sehemu ya kutafuta jina au namba, tofauti na uzuri wa hii app haihitaji ujisajiri ili kuweza kupata taarifa za mtu unayetaka kumfahamu kama ilivyokuwa kwenye tovuti yake, kwa hiyo unaweza ukaandika namba yake hapo kisha utaona jina na mahali alipo.

from Blogger http://ift.tt/2rFjBLc
via IFTTT