Baada ya Kumwagana na Ali Kiba,,Jokate Aaamua Kuweka Wazi Vigezo kwa Kidume Mwingine Anayemtaka..!!!

Mrembo Jokate Mwegelo ameamua kuweka wazi juu ya mwanaume anayependa kuolewa naye na kuanzisha familia baada ya miaka mitano.
Akizungumza na gazeti la Mwanachi Jokate ambaye ametajwa kuwa katika orodha la jarida la Forbes Africa la kuwa miongoni mwa vijana walio na umri chini ya miaka 30 wenye mafanikio mbalimbali kwa mwaka 2017.
“Kusema kweli kitu ninachotamani awe nacho mume wangu ni hofu ya Mungu, pia awe mchapakazi na mwenye malengo ya mbele. Mwanaume wa aina hiyo ni rahisi sana kumthamini mke wake, kutambua mwanaume mwenye upendo wa dhati si ngumu kwani unaangalia maisha yake binafsi anaishije na ndugu ,jamaa na marafiki” amesema Joketi.
Pia mrembo huyo amesisitiza kuwa suala la dini si kikwazo kwake kwani amezungukwa na watu wa imani tofauti.
Kwa takribani mwaka mmoja Jokate amekuwa akihusishwa kuwa na mahusiano na mwanamuziki Alikiba ingawa hakuna kati yao aliyewahi kuthibitisha hilo.

from Blogger http://ift.tt/2qTOTKh
via IFTTT