WAFANYABIASHARA WATISHIWA KUVUNJIWA SOKO WASIPO CHAGUA CCM

WAFANYABIASHARA mkoani Njombe katika soko kuu wametakiwa kutokuwa na wasiwasi wa kuichagua Chadema kutokan ana tishilo walilotishiwa aliyekuwa meya wa mji wa Njombe Edwin Mwanzinga wakati akimnadi mgombea utiwani CCM sokoni hapo.

Hayo yalebainishwa katika kampeni za chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema na mgombea, chama hicho jimbo la Njombe kusini Emmanuel Masonga alisema kuwa soko hilo ni la serikali na kuwa hakuna anaye weza kulivunja akishindwa uchaguzi.

Masonga aliyasema hayo baada ya kuwepo kwa kauli za kuvunjwa kwa soko kuu la Njombe kama hawata mchagua diwani wa chama cha mapinduzi CCM huku wafanyabiashara wakiachwa midomo wazi.

Alisema kuwa meya huyo hana mamlaka ya kuvunja soko la Njombe mjini na kuwa soko hilo sio la chama kwa kuwa ni soko la mji wa Njombe.

Aliongeza kuwa Wananchi wakiichagua Chadema  kutakuwa na maendeleo katika soko hilo na kukamilisha ujenzi wa mageti katika soko hilo na kuepusha wizi usio wa lazima kutokana na kuto kuwepo kwa mageti sokoni hapo.

Hata hivyo alisema kuwa Haita wezekana mtu aliye shindwa kwenda kuvunja soko kwa kuwa haya kuwa madarakani.

Alisema Chama hicho kitafanya mpango wa kurejesha vitu vyo te vilivyo jengw ana wananchi wakati wa chama kimoja na kumilikishwa CCM na kuwa kama chama kinataka kuwa na mradi kiatakiwa kutumia fedha zake na sio nguvu za wananchi wote katika ujenzi wa mali za vyama.


Alisema hata Chadema wakitaka kuwa ma mradi watarazimika kutumia nguvu zao na sio kutumia nguvu za wananchi katika ukamilishaji wa miradi hiyo.