Showing posts with label Chadema. Show all posts
Showing posts with label Chadema. Show all posts
Mwalongo Mshinde kesi ya kupinga matokeo jimbo la Njombe kusini

Mwalongo Mshinde kesi ya kupinga matokeo jimbo la Njombe kusini


MAHAKAMA kuu kanda ya Iringa imemtangaza Edward Mwalongo Kuwa mbunge wa jimbo la Njombe kusini katika kesi iliyo kuwa ikimkabili ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyo funguliwa na aliye kuwa mgombea ubunge kupitia Chadema Emmanuel Masonga.

Akisoma hukumu hiyo ya kesi namba 5 ya uchakuzi mwaka 2015 jaji wa mahakama hiyo Jaji Jacob Mwambegele alisema kuwa baada ya kupitia ushahidi ulio tolewa mahakamani hapo unaonyesha kuwa mlalamikaji hakupeleka malalamiko yake katika kamati ya ya maadili ya uchaguzi ya jimbo.

Alisema kuwa mahakama yake haiwezi kutengua ushindi uliomtangaza mbunge wa jimbo la Njombe Kusini kwa kuwa mdai hakupeleka malalamiko yake katika kamati ya maadili kama sheria inavyo sema.

Jaji Mwambegele alisema kuwa licha ya mahakama yake kubaini kuwapo kwa kampeni zilizo kuwa zemekiuka misingi ya kimaadili na kuendeshwa kwa udhalilishaji lakini mlalamikaji hakufuata sheria ya uchaguzi.

Alisema kuwa kigezo cha kuto peleka malalamiko katika kamati ya maadili Masonga inamnyima haki ya kupinga matokeo hayo kwa kuwa kamati ya maadili ilikuwepo na kuunyima ushahidi wake nguvu ya kushinda.

Jaji Mwambegele alisema kuwa uchaguzi huo uliendeshwa kwa uhuru na haki na kuwa hawezi kumtegua mshinde aliye shinda katika uchaguzi huo.

Kesi hiyo ilisikilizwa mashahidhi zaidi ya 30 kutoka pande zote za walalamikaji na washitakiwa na kusikilizwa kwa zaidi ya miezi 3 huku baadhi ya wiki kuendeshwa mfurulizo bila kupumzika na kufanya kesi hiyo kuisha haraka.

Katika ukumbi wa mahakama wafuasi wa Chadema walionekana kuwa wengi kuliko wale wa Chama cha mapinduzi CCM ambao walifika kusikiliza hukumu hiyo.

Aidha mbunge Mwalongo alitoa shukrani zake kwa mahakama Kuu kwa kumtangaza mshinda katika kesi hiyo ya kupinga matokeo.


Octoba 25 mwaka huu kulifanyika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani ulimtangaza Edward Mwalongo kuwa mshindi wa kiti cha ubunge katika jimbo la Njombe Kusini ambako kulikuwa na wagombea wane ambao walisimamishw ana Vyamba vya CCM, Edward Mwalongo kura 27285, Chadema Emmanuel Masonga kura 23003, Act Wazalendo Emilian Msingwa kura 3888 na DP William Myegeta. kura 94 katika kata zake 13
CHADEMA KUELEKEA iKULU WAPIGWA MKWALA

CHADEMA KUELEKEA iKULU WAPIGWA MKWALA


Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limepiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanyika hapo kesho na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuelekea Ikulu jijini Dar es salaam kushinikiza kurejeshwa ka matangazo ya moja kwa moja ya Bunge.
Akizungumza leo jijini Dar es salaam, Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Naibu Kamishna wa Polisi Simon Siro amesema Chama hicho kinatakiwa kutumia mbinu nyigine ya kushinikiza kurejeshwa kwa matangazo hayo ya Televisheni ya Taifa na sio kupitia maandano.

Katika hatua nyingine jeshi hilo limesitisha kazi za vikundi vya ulinzi shirikishi katika kituo cha kati kutokana na kufanyika kwa vitendo vyenye harufu ya rushwa, kutofuata sheria za ukamataji pamoja na kutumia nguvu kupita kiasi huku Naibu Kamishna Siro akianisha kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kukamata wanaokiuka taratibu.

HII NDO KAULI YA ZITO KABWE MALA BAADA YA HALIMA MDEE KUTEULIWA KUWA Waziri Kivuli Fedha na Mipango



VIONE VITU LIVILYO MTIA WASIWASI MSAMBICHAKA MGOMBEA UBUNGE LUDEWA WA CHADEMA

MGOMBEA wa ubunge jimbo la Ludewa kupitia Chadema anawasiwasi wa matokeo yaliyotangazwa kutokana na sababu mbili alizo zitaja kuwa huenda lilipunguza kura na kufanya uchaguzi kuwa sio wa huru.

Mgombea huyo Batromayo Msambichaka alisema kuwa sababu ambazo zinamfanya kuwa na wasiwasi na matokeo ni pamoja na baadhi ya mawakala walio wateua kukataliwa na vuruguzilizo tokea usiku wa kuamukia uchaguzi.

Msambichaka ambaye kura zake hazikutosha katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Ludewa, kwa kupata kura 7,956 dhidi ya mbunge mteulia wa CCM Deo Ngalawa aliye pata kura 23861 na kutangazwa mshindi.

Alisema kuwa wakati wa kupelewa mawakala kwa msimamizi wa uchaguzi baadhi yao walikataliwa kushiriki kusimamia uchaguzi huo hiyo anasema kuwa ni moja ya sababu ambayo huenda imempunguzia kura katika uchaguzi huo.

Alisema kuwa “Tulipeleka mawakala kwa msimamizi wa uchaguzi ili awathibitishe kuwa mawakala wangu katika uchaguzi huo lakini walikataliwa kwa kigezo walikuwa wametoka mbali wakati hao ndio chama kiliwasimamisha,”

Alisemam kuwa mbali na kuwapo kwa pingamizi la mawakala wa chama  hicho katika uchaguzi pia chama hicho siku moja kabla ya uchaguzi wafuasi wake walipigwa na wafuasi wanao daiwa kuwa ni wa chama cha mapinduzi.

“Usiku wa kuamukia siku ya uchaguzi wanachama wangu walivamiwa na wanachama wa CCM na kupigwa vibaya na kulazwa katika Hospitali ya misheni ya Lugalawa hii nayo ni sababu inayo sema kuwa uchaguzi huu siku lidhika nao,” alisema Msambichaka.

Msambichaka alisema kuwa vijana watatu wauasi wa Chadema walivamiwa na Wauasi wa CCM na kusema kuwa wauasi saba wa CCM walishikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na tukio hilo.

Kushusi kukubari ama kukataa matokeo alisema kua anashauriana na wiongozi wa chama hicho na atatoa maamuzi ya kukubali ama kukataa matokeo.

Hata hivyo Kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe Wilbrod Mutafungwa alithibitisha kuwakamata watu saba wanao daiwa kuwa ni wafuasi wa CCM siku ya Jumapili kuhusisha na tukio usiku wa kuamkia siku ya kupiga kura.

Kuhusiana na kuzuiwa kwa mawakala wa chama hicho msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Ludewa, William Waziri alisema kuwa wakala wa anatakiwa kutoka katika eneo la jimbo la uchaguzi na sio nje ya jimbo hilo suala hilo lipo kisheria.
Msambichaga Bathromeo wa Chadema alikuwa mgombea wa Ubunge jimbo la Ludewa

Kategori

Kategori