Bodaboda walalamika kunyanyashwa na polisi Njombe


WAFANYABIASHARA ya usafirishaji pikipiki maarufu bodaboda mkoani Njombe wamekama na jeshi la polisi kwa kile kinachodaiwa wamefanya vurugu na kuchoma gari lililo sababisha ajali na kifo cha dereva wa pikipiki.

Jeshi la polisi  linaendesha msako wa kukamata waendesha bodaboda kwa siku ya tatu jana kwa lengo la kuchambua walio husika na tukio hilo huku walio kuwemo na wasio kuwemo kukamatwa wao pamoja na pikipiki zao.

Akizungumzia suala la kamatakamata hiyo kamanda wa polisi mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani amesema kuwa jeshi hilo linaendesha msako wa kuwakamata madeleva wa bodaboda kwa lengo la kuwabaini wale walo husika na matukio mawili ya kuchoma hali na kuvamia polisi na kuwarushia mawe.


“Taarifa za interijensia zinasema kuwa watu zaidi ya 200 walihusika katika tukio la kuvamia polisi waliokuwa wamekamata wezi wa pikipiki na tutaendelea kuwawaka mpaka tukakikishe walio husika na wengine wale waliohusika na uchomaji wa gari lililosababisha ajali lililokuwa na zaidi ya thamani ya shilingi milioni 34,” alisema Ngonyani.


Aidha kwa mujibu wa Kamanda wa polisi alisema kuwa wamekamata madereva bodaboda 18 na kuwa jeshi hilo linaendelea na kuwatafuta wengine na kuwa jeshi la polisi halijazuia biashara hiyo kuendelea licha ya kuwa vituo vyote vya bodaboda havina pikipiki na habari kutoka kwa vyanzo visivyo aminika zinasema kuwa watu zaidi ya 120 wanashikiliwa na jeshi la polisi.




Kwa upande wa madereva wa pikipiki wamelalamikia kitendo kinacho fanywa na jeshi hilo kwa kuwa kinakamata watu bila kujua ni dereva ama sio derevava.


Wakizungumza bila kutaja majina yao walisema: “Polisi sasa wanatunyanyasa hata ambao hatukuhusika kwani wakikukuta barabarani bila kukuuliuza wanakukamata na kukunyanganya pikipiki na ukikimbia wanakokopa pikipiki,” alisema Dereva huyo.


Alisema kuwa wanapokutwa njiani wanawakamata na kuwapiga virungu na kasha kuwanyang’anya pikipiki zao.


Alisema kuwa kuma mzee kutoka kijijini alikamatwa baada ya kukutwa akiwa katika kituo cha bodaboda akimsubiri dereva wa bodaboda ili ampeleke nyumbani baada ya kutoka vijijini.



Nae mwenyekiti wa madereva bodaboda Philimon Mwinuka alisema kuwa kitendo kinacho fanywa na jeshi la polisi ni uonevu na kuwa wanawanyima haki watuiaji wa usafiri huo kwa kuwa hakuna dereva anaye fanya biashara hiyo kwa zaidi ya masaa 48 tangu kuanzishwa kwa oparationi hiyo kwa kuwa wakiingia barabarani wanakutana na polisi wanao kamata bila kuulizwa.


Alisema kuwa jeshi la polisi lilitakiwa kuhakikisha wanakaa na uongozi wa wa bodaboda ili wawatajie walio husika kwaniu wanafahamiana kuliko kitendo kilicho fanywa na jeshi la Polisi.



  

Related Posts