WANARIAZA Nicodemus Hiiti na Banuelia Brighton wametwaa taji la ushindi katika Mbio za
“Mt. Kilimanjaro Marathon” zilizofanyika jana mjini Moshi wakiwatupa wamarekani
walioshiriki mbio hizo.
Nicodemus
(Arusha) na Banuelia Brighton (Moshi) walikimbia kilometa 42 kwa muda wa saa
2:39.40 na 3:12.22.
Klabu ya
Holili Youth Athletics (HYAC) katika mbio hizo za kilometa 42 iliweza kuchukua
nafasi za pili na tatu zilizokwenda kwa Andrew Boniface (2:39.09) na Procesius
Prosper (2:39.10).
Nafasi ya
pili kwa wanawake ilichukuliwa na Nicole Greene kutoka Marekani aliyekimbia kwa
muda wa saa 3:52.16. mmarekani mwingine kwa wanaume alikuwa Chad Greene
aliyemaliza nafasi ya 4 kwa muda wa 3:43.52.
Kilometa
21, wanaume katika Mt. Kilimanjaro Marathon ilichukuliwa na Pascal Mombo (HYAC)
aliyekimbia kwa muda wa saa 1:08.16, akichuana vikali na Elibariki Buko
(1:08.24) na Oswald Kahuruzi (1:08.40) wote kutoka klabu hapo.
Kwa upande
wa wanawake Kilometa 21
ilichukuliwa na wanariadha kutoka HYAC
ambao ni Furaha Sambeke aliyekimbia kwa muda wa saa 1:25.40, Irene Chima
(1:32.15) na Neema Mathias (1:36.20); huku mmarekani Nancy Loughlin akiingia
wanne (1:46.04).
Pia
kulikuwepo na mbio za kilometa 10 ambapo Hilary Hendry alishika nafasi ya
kwanza akifuatiwa na Ottoman Seki kwa wanaume waliokimbia kwa dakika 68.10 na
74.20.
Adelina
Audax na Lidiuna Godfrey kutoka HYAC walimaliza mbio hizo wakikimbia kwa muda
wa dakika 52.30 na 52.33 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Glory Mbise
aliyekimbia kwa muda wa dakika 53.24; wamarekani Hilary Hendron (Tenessee) na
Susan HawkesTeeter (New York) walimaliza kwa dakika 61.42 na 68.15
Mratibu na
Mwasisi wa Mbio hizo Mama Maria Frances (Washington DC) aliwataka watanzania
kuendelea kuutangaza Mlima Kilimanjaro kutokana na ukweli kwamba umekuwa
ukitumika kuwanufaisha mataifa mengine.
Aliongeza
kuwa wanariadha wanapaswa kujituma wanapokuwa katika mazoezi ili kuleta ufanisi
wakati pindi michuano inapokuja hivyo kutoa mwangaza wa maisha ya mwanariadha
kimataifa.
Mbio hizo
zilifanyika mjini Moshi zikitimiza miaka 23 tangu kuasisiwa kwake mwaka 1991
zikiwa na malengo ya kuutangaza mlima Kilimanjaro kuwa ni kivutio cha kipekee.