- NOTO MBILI ZAKAMATWA KWA MKULIMA
ALIKUWA ANATAKA KUFANYA MANUNUZI
JESHI
la Polisi mkoiani Mbeya linamshikilia Mkulima Joseph Ngonyani (20) kwa tuhuma ya
kupatikana na Noti Bandia zenye thamani ya 20,000.
Noti
hizo zilikamatwa katika maeneo ya Mwanjelwa jijini Mbeya ambapo mtuihumiwa
alikuwa akitaka kuzitumia katika manunuzi.
Kamanda
wa polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athuman alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa
na noti mbili za za shilingi 10,000 bandia alizo kuwa akitaka kuzitumia kwa
manunuzi.
Alisema
kuwa mtuhumiwa alikamatwa na askali walio kuwa dolia na msako ndipo walipo
mkuta mtuhumiwa huyo akiwa na noti hizo.
Alisema
kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinafanywa ili
mkondo wa sheria kuchukua nafasi yake.
Athumani
ametoa wito kwa jamii ya watanzania na wafanya biashara kuwa makini na kufanya
uchunguzi wa pesa wanapo nunua ama kuchukua chenji.
