MZEE AGONGWA MPAKA KUFA NA GARI ISIYO FAHAMIKA



MZEE mmoja amekufa papo hapo baada ya kugongwa na gari ambayo hajijafahamika katika maeneo ya Kijiji cha Mbugani wilani Chunya mkoani Mbeya.
 
Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 1:30 jioni katika maeneo ya Mbugani tarafa ya Kiwanja wilayani chunya ambapo gal;I isiyo fahamika ilimgonga mtembea kwa miguu, Omari mwangosi (75).

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athuman alisema kuwa gari ambayo ilisababisha ajali hiyo ilitokomea kusiko julikana baada ya kutokea kwa tukioa hilo.

Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari hiyo ambayo ilisababisha kifo cha mzee huyo papo hapo.