NEW YORK: ATAKAYE TOA TAARIFA ZA AL-SAHABAAB KUPATA DOLA MILIONI 33 (M. $ 33)



Serikali ya Marekani inatarajiwa kutangaza zawadi ya hadi dola milioni 33 hivi leo kwa mtu atakayetoa taarifa za wanachama wa ngazi za juu wa kundi la al-Shabaab nchini Somalia.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa mpango huo kutangaza zawadi kwa wanachama wa al-Shabaab, kundi lenye mafungamano na mtandao wa kigaidi wa al-Qaida na linalotuhumiwa kufanya mashambulizi ya kigaidi katika nchi za Somalia, Uganda na Kenya.

Mpango huo utatoa hadi dola milioni 7 kwa taarifa kuhusiana na muasisi wa al-Shabaab, dola milioni 5 kwa wasaidizi wake watatu na hadi dola milioni 3 kwa wanachama wengine wawili wa ngazi za juu wa kundi hilo.