MAGEREZA nchini zinakabiliwa
na msongamano wa wahalifu kutokana na kuwapo watu 38,000 wakati magereza hayo
yana uwezo wa kuchukua waharifu 29,522.
Hayo yamebainishwa mjini
Morogoro na Kamishana Jenerali wa Magereza, Augustino Nanyaro, baada ya
kuwavisha nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Nne maofisa na askari magereza
37 katika sherehe iliyofanyika katika viwanja vya gereza la Mtego wa Simba
Kingorwila mkoani Morogoro.
Amesema kukosekana kwa
magereza katika baadhi ya wilaya kunachangia kwa kiasi kikubwa msongamano huo
ambapo wahalifu wake wanalazimika kuwekwa katika magereza za wilaya za jirani.
