MAGRETH Nnziwa amechaguliwa
kuwa Spika wa Bunge la Tatu la Afrika Mashariki (EALA) kwa kupata kura 33 huku
aliyekuwa mpinzani wake, Dora Byamukama, akipata kura 12.
Wabunge hao wote wanatoka
chama tawala nchini Uganda,
(NRA) na Magreth anakuwa mwanamke wa kwanza kuongoza chombo hicho.
Uchaguzi huo umefanyika
kwenye ukumbi wa Bunge hilo ulioko kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha
jijini Arusha (AICC) na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa EAC, Dk. Richard
Sezibera, viongozi mbalimbali wa kiserikali kutoka nchi wanachama wakiwemo
mawaziri pamoja na mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere.
