UPELELEZI wa kesi ya
wawekezaji wa mashamba ya kapunga walioshitakiwa kwa kumwaga sumu katika
mashamba ya wananchi umekamili na kesi yao
kupangiwa siku ya kuanza kusikilizwa.
Kesi hiyo inayowakabili raia
wa Afrika Kusini wawekezaji wa mashamba ya Kapunga Rice ya wilayani Mbarali,
wakili wa serikali Lugano Mwakilasa, akiwa na mwenzake, amesema upelelezi wa
kesi hiyo umekamilika na kuanza kusikilizwa hivi karibuni.
Hakimu mfawidhi wa mahakama
ya hakimu mkazi ya Mbeya, Seif Kulita, amesema, kesi hiyo itatajwa tena tarehe
20 kwa ajiri ya kupangiwa siku ya kuanza kusikilizwa.
