MBEYA : WAENDESHA BAJAJ WAOPA KUZUNGUKA JIJI

CHAMA cha waendesha bajaji Isanga mkoani hapa
Kimeitaka serikali kuruhusu bajaji kufika katika maeneo mbalimbali 
Mkoani hapa

Akizungumza na Rock Fm, katibu wa umoja wa bajaji Bw Kenedy Kayange ameseama kuwa usafiri mkubwa unaotumiwa na watu wengi Jijini hapa ni bajaji, hivyo ameitaka serikali kuwaruhusu kufika katika maeneo mbalimbali ya jiji.

Bw Kenedy amesema kuwa barabara zinazo tumiwa na bajaji ni chache hali inayopelekea kuwa na msongamano mkubwa wa bajaji katika barabara hizo na kuwa chanzo cha ajali nyingi.