MBEYA: WAANDISHI WATAKIWA KUSHIRIKIA NA POLISI


WAANDISHI wa habari mkoani Mbeya wametakiwa kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa mbalimbali ili kupambana na uhalifu


Akizungumza na waandishi  wa  habari ofisini kwake, kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Diwani  Athumani  amesema kuwa  wanaweza  kupiga  simu  moja  kwa  moja kwake ili  kuthisha matukio  mbalimbali  wanakutana  nayo waandishi.

Aidha  amesema  matarajio  yake  ni  kuhakikisha  Mbeya kunakuwa na  amani  na utulivu  katika  kuleta  maendeleo pia amesema  kuwa  kwa  kushirikiana  na  jeshi  la  polisi  atahakikisha  wahalifu  wote  wanashikiliwa.