KONGO: ONYO LATOLEWA KWA WAMAREKANI


Msemaji wa kundi la waasi  la M23 katika Jamhuri ya Kidemopkrasi ya Kongo  amelionya jeshi la  Umoja wa mataifa nchini humo Monusco, kutoliunga mkono jeshi la taifa katika mapigano na waasi hao. 

Msemaji huyo Kanali Kazarama Vianey ametahadharisha juu ya urukaji ndege katika  maeneo yanayodhibitiwa na waasi  wa M23 akisema zitadunguliwa. 

Wakati huo huo, Waziri mkuu wa Congo Matata Ponyo amemaliza ziara yake katika  eneo la Mashariki mwa nchi hiyo, akisisitiza kwamba jeshi la Congo litamaliza vita vinavyoendelea katika eneo hilo.