=Chelsea wako nchini China kwa ajili ya mechi za kujiandaa na msimu mpya wa ligi lakini wakiwa nchini humo kiungo wao Kennedy amepata dhahma kubwa baada ya kuzomewa na raia wa nchi hiyo.
Kennedy ameingia katika matatizo hayo baada ya kusambaa kwa video ambayo ilimuonesha akiwadhihaki Wachina na nyingine inayoonesha kuwaita Wachina “wapumbavu” suala lililowaudhi sana raia hao.
Baada ya tukio hilo klabu ya Chelsea wametoa taarifa ya wazi kuomba msamaha kwa tukio alilofanya kiungo huyo na wakasisitiza kwamba hakuwa na nia ya kuwakosea heshima Wachina.
“Chelsea tunaomba radhi kwa video alizopost Kennedy jana jioni, hii ni tabia ambayo hatukuitarajia kwa mchezaji wetu lakini na yeye mwenyewe anajutia kwa tukio lililotokea tunaomba msamaha kwa hilo”
“Kila mtu katika klabu yetu ana heshima kwa taifa la China kwani wamekuwa wenyeji wema kwetu na wametuonesha upendo na uungwana wa hali ya juu, tunaomba msamaha” ilisema taarifa ya klabu ya Chelsea.
Hii leo Chelsea walikuwa na mechi zidi ya Arsenal ambapo wameibuka na ushindi wa mabao matatu kwa nunge mabao yakifungwa na Mitchy Batshuayi aliyefunga mbili na Willian akifunga lingine.
Mfanyabishara maarufu nchini Tanzania Yusuf Manji ameondolewa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alipokuwa akitibiwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi na kupelekwa Gereza la Keko lililopo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la MTANZANIA zilizothibitishwa na wakili wake, Manji anayetuhumiwa kwa mashtaka 7 ya uhujumu uchumi na usalama wa taifa ambayo hayana dhamana aliondolewa hospitali hapo juzi usiku.
Taarifa kutoka Gereza la Keko na ndani ya JKCI alikokuwa akitibiwa zimethibitisha kuwa Manji ambaye pia ni Diwani wa Mbagala kwa tiketi ya CCM, amepelekwa Keko.
Gazeti hilo limeeleza zaidi kuwa, jana viunga vya taasisi hiyo ya matibabu havikuwa vimezungukwa na Askari kama ilivokuwa siku za nyuma Manji alipokuwa ndani.
Alipotafutwa Mkurugenzi Mkuu wa JKCI, Prof. Janab alikataa kuzungumzia suala hilo akisema kuwa ni kinyume na maadili ya kazi kutoa taarifa za mgonjwa.
Alipoulizwa wakili anayemtetea Manji, Hudson Ndusyepo alisema ni kweli ameruhusiwa (Manji) kutoka hospitali na kuthibitisha kuwa ni kweli yupo Gereza la Keko lakini yeye hajui ni muda gani aliporuhusiwa kutoka.
Manji pamoja na wenzake watatu mapema wiki huu (Julai 5) walisomewa mashtaka 7 chini ya sheria ya uhujumu uchumi na usalama wa taifa baada ya kukutwa na vitambaa vya sare za jeshi pamoja na mihuri mali zinazodaiwa kupatikana kinyume na sheria lakini pia kutishia usalama wa taifa.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Quality Group, Deogratius Kishinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Thomas Fwere (43).
UAMUZI wa vyombo vya habari kumsusia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kufanya naye kazi kumepongezwa na wadau.
Wakizungumza na JAMBO LEO kwa nyakati tofauti jana, wadau wa habari nchini walisema uamuzi huo umechelewa na kushauri kuwa ungehusu Serikali nzima kwa wanachodai kuwa anapewa kiburi na wakubwa zake.
Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alisema kwa mtazamo wake anapongeza hatua hiyo, huku akisisitiza kuwa ingekuwa vema kutofanya kazi na Serikali nzima.
Sugu alisema kwa welewa wa kawaida inaonesha dhahiri anachofanya Makonda ni maagizo ya wakubwa wake wa kazi hivyo hakuna sababu ya kufanya kazi nao wote.
“Makonda ni sawa kutoandikwa ila naamini anachofanya si kwa uamuziwake, kuna watu wanamtuma ambao ndio wamempa nafasi hiyo inapaswa nao wasiandikwe,” alisema.
Mbunge huyo alisema haiwezekani Makonda kuchukua askari wote aliokwenda nao katika televisheni ya Clouds Media bila mkuu wake kuhusika, hivyo itakuwa vema nao kutoandikwa.
Alisema katika ulimwengu huu wa sasa ambao demokrasia inatakiwa kutamalaki, haingii akilini kuona tukio kama alilofanya Makonda likichekewa kwani linaweza kusababisha jamii kupotoka.
Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu Tanzania (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema uamuzi huo ni wakuungwa mkono na watu huo ili kuhakikisha kuwa mamlaka husika zikichukua hatua.
Dk Bisimba alisema pia angependa kuona zikiwepo hatua nyingine za kisheria kama kwenda mahakamani ili kuhakikisha kuwa haki inatamalaki nchini kwa watu wote.
Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene alisema uamuzi wa vyombo vya habari ungepaswa kufanyika tangu kupitishwa Sheria ya Huduma kwa Vyombo vya Habari ambayo ililalamikiwa na jamii nzima.
Alisema anachofanya Makonda ni kosa kisheria na hakiwezi kuvumiliwa na mtu yeyote na kwamba kila kona inalalamika kwa Serikali kushindwa kusimamia haki.
“Vyombo vya habari vimechelewa sana kuchukua uamuzi huu kwani wangepaswa kufanya hivyo katika mchakato wa sheria yenu ambayo imepitishwa hivi karibuni,” alisema.
Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyuo Vikuu CCM, Daniel Zenda alisema haungi mkono uamuzi wa vyombo vya habari kutoandika habari za kikazi zinazomhusu Makonda na kwamba anaamini kuwa ni kutowatendea haki wananchi.
Alisema ni vema uamuzi huo ukawa ni kuzuia habari zake binafsi ili wananchi waweze kujua nini kinachoendelea katika mkoa huo.
Chanzo: Jamboleo
TAZAMA HARMORAPA ALIVYO TIMUA MBIO BAADA YA KUIONA BASTOLA