Showing posts with label 2017 at 11:33AM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 11:33AM. Show all posts
CHELSEA WAWATAKA RADHI WACHINA BAADA YA KIUNGO WAO KUWAKASHIFU

CHELSEA WAWATAKA RADHI WACHINA BAADA YA KIUNGO WAO KUWAKASHIFU

=Chelsea wako nchini China kwa ajili ya mechi za kujiandaa na msimu mpya wa ligi lakini wakiwa nchini humo kiungo wao Kennedy amepata dhahma kubwa baada ya kuzomewa na raia wa nchi hiyo.
Kennedy ameingia katika matatizo hayo baada ya kusambaa kwa video ambayo ilimuonesha akiwadhihaki Wachina na nyingine inayoonesha kuwaita Wachina “wapumbavu” suala lililowaudhi sana raia hao.
Baada ya tukio hilo klabu ya Chelsea wametoa taarifa ya wazi kuomba msamaha kwa tukio alilofanya kiungo huyo na wakasisitiza kwamba hakuwa na nia ya kuwakosea heshima Wachina.
“Chelsea tunaomba radhi kwa video alizopost Kennedy jana jioni, hii ni tabia ambayo hatukuitarajia kwa mchezaji wetu lakini na yeye mwenyewe anajutia kwa tukio lililotokea tunaomba msamaha kwa hilo”
“Kila mtu katika klabu yetu ana heshima kwa taifa la China kwani wamekuwa wenyeji wema kwetu na wametuonesha upendo na uungwana wa hali ya juu, tunaomba msamaha” ilisema taarifa ya klabu ya Chelsea.
Hii leo Chelsea walikuwa na mechi zidi ya Arsenal ambapo wameibuka na ushindi wa mabao matatu kwa nunge mabao yakifungwa na Mitchy Batshuayi aliyefunga mbili na Willian akifunga lingine.

from Blogger http://ift.tt/2eFigQk
via IFTTT


MANJI AONDOLEWA MUHIMBILI USIKU CHINI YA ULINZI MKALI

MANJI AONDOLEWA MUHIMBILI USIKU CHINI YA ULINZI MKALI

Mfanyabishara maarufu nchini Tanzania Yusuf Manji ameondolewa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alipokuwa akitibiwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi na kupelekwa Gereza la Keko lililopo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la MTANZANIA zilizothibitishwa na wakili wake, Manji anayetuhumiwa kwa mashtaka 7 ya uhujumu uchumi na usalama wa taifa ambayo hayana dhamana aliondolewa hospitali hapo juzi usiku.
Taarifa kutoka Gereza la Keko na ndani ya JKCI alikokuwa akitibiwa zimethibitisha kuwa Manji ambaye pia ni Diwani wa Mbagala kwa tiketi ya CCM, amepelekwa Keko.
Gazeti hilo limeeleza zaidi kuwa, jana viunga vya taasisi hiyo ya matibabu havikuwa vimezungukwa na Askari kama ilivokuwa siku za nyuma Manji alipokuwa ndani.
Alipotafutwa Mkurugenzi Mkuu wa JKCI, Prof. Janab alikataa kuzungumzia suala hilo akisema kuwa ni kinyume na maadili ya kazi kutoa taarifa za mgonjwa.
Alipoulizwa wakili anayemtetea Manji, Hudson Ndusyepo alisema ni kweli ameruhusiwa (Manji) kutoka hospitali na kuthibitisha kuwa ni kweli yupo Gereza la Keko lakini yeye hajui ni muda gani aliporuhusiwa kutoka.
Manji pamoja na wenzake watatu mapema wiki huu (Julai 5) walisomewa mashtaka 7 chini ya sheria ya uhujumu uchumi na usalama wa taifa baada ya kukutwa na vitambaa vya sare za jeshi pamoja na mihuri mali zinazodaiwa kupatikana kinyume na sheria lakini pia kutishia usalama wa taifa.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Quality Group, Deogratius Kishinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Thomas Fwere (43).
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sXN14n
via IFTTT


Anna Mgwira Ajivua Uanachama wa ACT Wazalendoโ€ฆ.

Anna Mgwira Ajivua Uanachama wa ACT Wazalendo….

Taarifa Kwa vyombo vya habari 
Mimi Anna mgwira nimejivua uwanachama wangu ACT-Wazalendo ili nikaweze kuwatumikia wana Kilimanjaro 
Kwakua nimejivua uwanachama mwenyewe moja Kwa moja nyadhifa zangu zote zitakuwa hazipo 
Namshukuru sana mh zitto Zuheri kabwe na wanachama wote ACT-Wazalendo kwakuniamini na kunipa nafasi ya kuwaongoza 
Hivyo kuanzia Leo tarehe 4/6/2017 Mimi sio mwanachama tena wa ACT-Wazalendo 
Kazi yangu sasa ni kuwatumikia wananchi kupitia nafasi yangu ya sasa ya Ukuu wa Mkoa Kilimanjaro 
Hii ni heshma kubwa kwangu na Kwa familia yangu Kwa ujumla 
Mungu awabariki 
Anna mgwira 
Leo 4/6/2017: saa7:30 mchana

from Blogger http://ift.tt/2suxV7p
via IFTTT


Kategori

Kategori