VIDEO:Tundu Lissu Afunguka Mazito Asema ACT Wameanzishwa Kuua Upinzani

Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Tundu Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki amefunguka kwa kusema chama ACT-Wazalendo kinatumiwa katika kuvunja upinzani uliopo nchini na serikali ya CCM.
Lissu amebainisha madai hayo baada ya Rais Magufuli kumteua aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro aliyeapishwa jana katika viunga vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.
“Hao siyo wapinzani hawajawahi kuwa wapinzani, walianzishwa kwa kazi maalumu ya kuua upinzani imeshindikana sasa wanapewa zawadi. ACT na Anna Mghwira walikuwa wakabariane na Lowassa nasiyo CCM walipata kura chache hata laki moja hazikufika. Huu ukuu wa Mkoa ni zawadi tu, Ukatibu Mkuu wa Kitila Mkumbo ni zawadi tu wanawazawadia watu wao hawa siyo wapinzani” alisema Lissu.
Aidha, Lissu amesema Serikali ya Chama cha Mapinduzi haijawahi kuwa na shida ya aina yeyote na viongozi wa ACT bali shida yao kubwa ni CHADEMA na CUF.
“Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM), haijawahi kuwa na shida na ACT wala Kitila Mkumbo, haijawahi kuwa na shida na Anna Mghwira na hao wanaojiita wapinzani wote, shida yao kubwa ni CHADEMA na CUF ndiyo wapinzani wengine wote hawa ni wana CCM” alisisitiza Lissu.
Pamoja na hayo, Lissu amesema haitoweza kuja kutokea kwa Rais Magufuli kuja kumteua yeye kwa nafasi yeyote na endapo itatokea hivyo basi atamtaka kwanza abadilishe katiba mpya ili waweze kutengeza nchi mpya.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2s7uU07
via IFTTT