Showing posts with label June 08. Show all posts
Showing posts with label June 08. Show all posts
Neno la Morata lawatia uchizi mashabiki wa Manchester United.

Neno la Morata lawatia uchizi mashabiki wa Manchester United.

Baada ya jarida la Forbes kutoa taarifa kuhusu utajiri wa klabu ya Manchester United ni wazi kwamba kwa sasa wanataka kufanya manunuzi makubwa na kuwaonesha watu nguvu ya pesa waliyonayo haswa katika kipindi hiki ambacho wamekuwa hawana matokeo mazuri ndani ya uwanja.
Jose Mourinho anaonekana ni mtu sahihi kurudisha heshima ya United ambayo ilipotea tangu kocha Sir Alex Ferguson alipoamua kustaafu soka, msimu huu pamoja na kumaliza ligi wakiwa nafasi ya sita lakini wamepata ticket ya kucheza Champions League msimu ujao baada ya kuchukua ubingwa wa Europa.
Tayari Mourinho yuko katika mawindo ya kutafuta wachezaji wakubwa ili kuleta upinzani mkubwa katika msimu ujao wa ligi, kati ya wachezaji ambao United wanatajwa kuwataka kwa nguvu zote ni nyota wawili wa Real Madrid Alvaro Morata na James Rodriguez na inaonekana Mourinho anataka kuwachukua kwa pamoja.
Alvaro Morata jioni ya Jumatano aliingia kama sub na kuikoa Hisapania baada ya kuisawazishia bao katika mchezo dhidi ya Colombia ulioisha kwa sare ya bao mbili kwa mbili na baada ya mchezo huo Morata aliulizwa kuhusu James Rodriguez na ndipo jibu lake limewafanya mashabiki wa United roho kuwadunda na kuhisi kwamba wametajwa wao.
//pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js



(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
Morata alisema “Rodriguez ni mchezaji mzuri sana na nina uhakika mwakani pia nitakuwa naye timu moja” iko wazi kwamba Rodriguez anaondoka Real Madrid na jibu la Morata linaonesha pengine mahali ambapo Rodriguez anaenda ndipo ambapo Alvro Morata pia anakwenda.
Tayari United wameshatuma ofa ya kwanza kwa Alvaro Morata ambayo Real Madrid wameikataa lakini tetesi za chinichini zinaseam James Rodriguez ameshaanza kuulizia uwepo wa jezi namba 10 katika klabu ya Manchester United,ni suala la muda tu tusubiri tuone nini kitatokea.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rFqE6c
via IFTTT


Antonio Conte amtimua Diego Costa Chelsea.

Antonio Conte amtimua Diego Costa Chelsea.

Kumbe ule uliotajwa kama ugomvi kati ya Diego Costa na kocha wake Antonio Conte ambao ulitokea katika dirisha lililopita la usajili haujaisha, kama unakumbuka kulikuwa na tetesi kwamba Costa alilazimisha kuuzwa China jambo ambalo lilimkera Conte na kuamua kumuacha katika mchezo mmoja wa ligi.
Baadae mambo yalionekana kuwa sawa na Conte akasisitiza hakuna tatizo kati yake na Costa na kwamba mshambuliaji huyo anaipenda Chelsea na hana mpango wa kuondoka na kuanzia hapo taarifa za msuguano kati ya hao wawili zikazimwa na Costa akaendelea kucheza Chelsea na kwa kiwango cha juu kabisa.
Takribani mwezi sasa umepita tangu Chelsea watwae ubingwa na Diego Costa ameibuka na kusema kwamba kocha Antonio Conte amemtumia ujumbe na kumuambia “haupo kwenye mipango yangu”, Costa aliyasema hayo kwa kinywa chake wakati wa mchezo wa kirafiki kati ya Hispania na Colombia.
//pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js



(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
“Kama hawanihitaji nitaanza kutafuta timu mpya, kwenda Atletico itakuwa jambo jema kwangu lakini itabidi nifikirie upya, kombe la dunia limekaribia lazima niende sehemu ambayo nitapata muda mrefu wa kucheza siwezi kaa sehemu ambayo nitapewa miezi mitatu au minne tu kucheza” alisema Costa.
Tayari inaonekana Conte amesahau msaada mkubwa wa Costa kwani mabao 20 na assist 3 alizotoa msimu huu zilichagiza kwa kiasi kikubwa ubingwa wa Chelsea lakini Conte hana mpango naye tena na tayari ameanza kumtafutia mtu wa kukaa nafasi yake huku Romelu Lukaku akitajwa kuwa mbadala wa Costa.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sYlDDA
via IFTTT


Habari za usajili zilizotawala vichwa vya habari leo Alhamisi.

Habari za usajili zilizotawala vichwa vya habari leo Alhamisi.

Baada ya habari kubwa iliyotoka leo kuhusu Diego Costa kuambiwa na kocha wake Antonio Conte kwamba hahitajiki msimu ujao wa ligi tayari vilabu mbalimbali vimeshaanza kupiga hodi katika klabu ya Chelsea huku Ac Millan wakitajwa kuwepo mstari wa mbele kumnunua Costa.
Manchester City wamethibitisha kumnunua mlinda mlango wa Benfica Ederson Moraes kwa dau la euro 35m, Moares mwenye umri wa miaka 23 amesaini mkataba wa miaka mitano kukipiga katika klabu ya Man City.
Pamoja na klabu ya Liverpool kuiomba msahamaha Southampton kuhusu suala la kutaka kujaribu kumsaini mlinzi Virgil Van Dijk bila kuwasiliana nao, klabu ya Southampton bado imesisitiza kwamba Liverpool lazima wafikishwe mbele ya sheria na kuchukuliwa hatua.
//pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js



(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
Klabu ya Real Madrid imewaambia Monaco kwamba Kylian Mbape hana thamani ya zaidi ya euro 100m kama wanavyodai, na Real Madrid wanasema pesa kubwa ambayo wanaweza kutoa kumsaini Mbappe ni euro 85m.
Juanma Lopez ambaye ni wakala wa Alvaro Morata amesema mteja wake hana uhakika kucheza Real Madrid msimu ujao kwani anahitaji muda mwingi wa kucheza tofauti na ule anaopewa na Real Madrid na hii inaweza kuwa habari njema sana kwa Manchester United.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rZVRSu
via IFTTT


Hii ndio orodha ya magolikipa 10 ghali zaidi duniani.

Hii ndio orodha ya magolikipa 10 ghali zaidi duniani.

Soka ni pesa, zamani ilikuwa washambuliaji tu wanaonunuliwa kwa gharama kubwa lakini sasa hadi magolikipa bora ni ghali na ndio maana haishangazi United kukataa euro 66m kwa ajili ya David De Gea, hawa hapa ndio walinda milango ghali duniani kwa sasa.
10.Fraser Foster na Asmir Begovic. Foster ni golikipa wa klabu ya Southampton ambaye alisajiliwa kutoka katika klabu ya Celtic mwaka 2014, pesa iliyotumika kumnunua Fraser Foster haikuwa ndogo kwani Southampton walitumia euro 10m kumnunua lakini Chelsea nao wakatumia kiasi hicho cha pesa kumnunua Asmir Begovic kutoka Bournamouth.
9.Petr Cech. Mlinzi mkongwe ambaye alikuwa na kiwango bora sana alipokuwa Chelsea na ni lazima kumtoa katika klabu ya Chelsea kulihitaji kiasi kikubwa cha fedha na Arsene Wenger alitoa euro 10.9 kumnunua mwaka 2015.
8.Jan Oblak. Msimu huu yupo katika kikosi bora cha ligi ya Champions League na tayari vilabu vingi vinamtamani na klabu ya Atletico Madrid ilitumia kiasi cha euro 12.6m kutoka Benfica mwaka 2014.
7.Jasper Cillessen. Mwaka 2016 klabu ya Barcelona walimuona Cillessen kama mlinda lango bora, Cillessen alikuwa akiidakia Ajax ya nchini Uholanzi na klabu ya Barcelona iliamua kutoa kiasi cha euro 12.8m.
6.Angelo Peruzzi. Golikipa wa Lazio ambaye alinunuliwa mwaka 2000 kutoka katika klabu ya Inter Milan, Lazio walitoa kiasi cha euro 15.7m kumnunua Angelo Peruzzi ambapo akawa mlinda lango ghali katika klabu ya Lazio.
5.Claudio Bravo. Pamoja na kelele nyingi kuhusu makosa anayoyafanya Claudio Bravo lakini Manchester City walitumia kiasi kikubwa sana kumnunua kutoka Barcelona ambapo kiasi cha euro 17m kumnunua Bravo.
4.David De Gea. Labda kwa sababu Manchester United walitumia kiasi kikubwa cha fedha kumnunua De Gea mwaka 2011 kutoka Atletico Madrid ndio sababu wanataka kiasi kikubwa kutoka Real Madrid, United walimnunua De Gea kwa euro 18m.
3.Manuel Neuer. Kati ya magolikipa ambao kuna nyakati alitajwa kwamba anafaa kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia, Manuel Neuer alinunuliwa na Bayern Munich kutoka Schalke 04 mwaka 2011 kwa dau la euro 19m.
2.Gianluigi Buffon. Golikpa ambaye pamoja na ubora wake wote lakini ameshindwa kuchukua kombe la Champions League, Buffon alinunuliwa na Juventus kutoka Parma mwaka 2011 kwa dau la euro 33m.
1.Ederson. Usajili huu umekamilika rasmi leo ambapo Emerson amesaini mkataba wa miaka mitano kuitumikia klabu ya Manchester City, Emerson amenunuliwa kwa dau la euro 34m kutoka Benfica na anakuwa golikipa ghali zaidi duniani.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2r0eIt0
via IFTTT


Kategori

Kategori