United watarajie nini kwa Victor Lindelof?

Kutoa kiasi cha euro 30.7m kumnunua mlinzi tena mwenye umri wa miaka 22 sio jambo dogo lakini Manchester United hawakujali na wametoa kiasi hicho cha pesa kumnunua mlinzi Victor Lindelof kutoka Benfica.
Wengine wamefurahia usajili huu huku wengine wakiuliza kwanini beki wakati tayari wana mabeki wengi, lakini kama ulikuwa hujui tu baasi jua kati ya aina wachezaji au walinzi ambao Mourinho anapenda baasi nia aina ya Lindelof.
Unaweza kuona safu ya ulinzi ya United ukiacha Eric Bailly na Dalley Blind klabu hii imekuwa na aina ya mabeki ambao wanajua tu kukaba lakini baada ya kufanikiwa kukaba wanapata tabu kujua sehemu sahihi ya kuupeleka mpira na mara nyingi wanapiga tu mipira mirefu mbele.
Lindelof pamoja na umri wake lakini ni mlinzi mwenye stamina na ana nguvu haswa na kitu cha ziada alichobarikiwa anapenda sana kukaa na mpira na kuanzisha mashambulizi kama ilivyo kwa Eric Bailly ambae nae ana nguvu na ujuzi wa kucheza na mpira.
Jarida moja nchini Ureno limeandika kuhusu mashabiki wa Benfica watakachomiss kwa Lindelof na mmoja kati ya mashabiki wanaoishi karibia na uwanja wa Benfica wa Estadio Da Luz amemuelezea Lindelof kama mchapakazi sana.
Lindelof ni mchezaji ambaye mara nyingi anawahi kufika mazoezini na ni wa mwisho kuondoka na hii ndio aina ya waoiganaji Mourinho anaowataka na kama akiwa katika kiwango alichokuwa nacho Benfica baasi hakika kuna ukuta mgumu sana unaenda kutengenezwa na Lindelof na Bailly.
Benfica walikuw wakimuita “Ice Man” kutokana na aina yake ya ukabaji wa nguvu nyingi sana na akili nyingi na inasemekana Benfica walipata ofa kubwa kutoka Italia lakini Lindelof alitaka kwenda kucheza United.
Tusubiri tuone pacha hii inavyoenda kuwa lakini ni wazi Mourinho anaonekana anataka atengeze ngome imara ya ulinzi kwani msimu uliopita haswa wakati unaanza baadhi ya walinzi waliigharimu United na Mou anajaribu kuzuia hilo lisijirudie.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2srntA4
via IFTTT