Ronaldo aibeba Ureno huku Mexico wakiitoa Newzealand

Akiwa anasubiria siku yake ya kutoa maelezo kuhusiana na kesi inayoendelea kumkabili ya ukwepaji kulipa kodi hakika leo Cristiano Ronaldo alikuwa na siku njema.
Ronaldo aliiongoza Ureno kuibamiza Russia bao moja kwa sifuri huku bao pekee la Ureno likiwekwa kimiani na mshambuliaji huyo katika kipindi cha kwa kwanza.
Baada ya mchezo huo kuisha kulipigwa mchezo mwingine kati ya Mexico na Newzealand ambapo hadi mchezo huo unaisha Mexico waliibuka kidedea kwa bao mbili kwa moja.
Walitangulia Newzealand katika dakika ya 42 kupitia kwa Chris Wood ambapo bao hilo lilidumu kwa kipindi kimoja kwani kipindi cha pili dakika ya 54 Raul Gimenez alisawazisha bao hilo kwa mkwaju mkali sana kabla ya Oribe Pelarta kuifungia Mexico la pili dakika ya 73.
Kwa matokeo hayo ya leo Ureno na Mexico wanakuwa wanalingana alama wote wakiwa na nne nne huku nafasi ya 3 ikishikiliwa na Urusi wenye alama 3 na Newzealand wanaburuza mkia wakiwa hawana alama hata moja na sasa wameaga rasmi mashindano hayo.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sTl2Xa
via IFTTT